Shirikisho la Mpira wa
Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikito taarifa ya kifo cha Nahodha
wa timu ya 94 Green Warriors, Ikongo Julius Mbaga aliyefariki dunia leo
alfajiri (Februari 17, 2017) kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) ambapo
alikuwa amelazwa.
Mchezaji huyo
alijeruhiwa kwenye ajali ya gari ya timu yake iliyotokea Februari 13, 2017
Ihumwa mkoani Dodoma wakati ikiwa njiani kwenda Shinyanga kucheza mechi ya Ligi
Daraja la Pili (SDL) dhidi ya Bulyanhulu FC.
Taratibu za mazishi ya
Marehemu ambaye mwili wake umehamishiwa Hospitali Kuu ya Jeshi (GMH) ya Lugalo
jijini Dar es Salaam zinafanywa na familia yake kwa kushirikiana na klabu ya 94
Green Warriors. Taarifa rasmi za mazishi zitatolewa baadaye.
TFF imetuma salamu za
rambirambi kwa familia ya Marehemu, klabu ya 94 Green Warriors na Chama
cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) na kuwataka kuwa na uvumilivu
kwa kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito.
Kwa Msiba huu, Rais wa
TFF Jamal Malinzi ametuma salamu za rambirambi kwa Mwenyekiti wa 94 Green
Warriors, familia ya marehemu, ndugu, jamaa na marafiki kwa msiba huo mkubwa wa
mpendwa wao.
Bwana ametoa, Bwana
ametwaa jina lake lihimidiwe.
No comments:
Post a Comment