Shirikisho
la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limetuma salamu za rambirambi kwa Mwenyekiti
wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Mbeya kutokana na kifo cha mchezaji wa
zamani Tanzania Prisons, Young Africans na timu ya Tanzania ‘Taifa Stars’.
Taarifa
kutoka Mbeya, zilizothibitishwa na uongozi wa Mkoa zinasema kwamba mchezaji
huyo alifariki dunia usiku wa kuamkia leo Ijumaa Februari 17, 2017 kwenye
Hospitali ya Wilaya ya Rungwe.
TFF
itawakilishwa na Katibu wa Chama cha Soka Mkoa wa Mbeya, Seleiman Haroub ambaye
kwa sasa atashirikiana na familia kufanya taratibu za mazishi ambayo taarifa
zaidi zitatangazwa baadaye mara baada ya vikao vya uamuzi.
Katika salamu zake za
rambirambi, TFF imewataka ndugu wa marehemu kuwa na uvumilivu kwa kipindi hiki
kigumu cha msiba huo mzito kwa Bonny ambaye nyota yake iling’ara zaidi wakati
Taifa Stars inafundishwa na Mbrazil Marcio Maximo.
Bwana ametoa, Bwana
ametwaa jina lake lihimidiwe.
No comments:
Post a Comment