Thursday, February 2, 2017

WANA USALAMA WA CUF YA PROFESA LIPUMBA WATOA ONYO KALI KWA WANAOTAKA KUKIHUJUMU CHAMA HICHO

 Mkurugenzi wa Usalama wa Chama cha Wananchi (CUF), Masoud Mhina, akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo mchana, kuhusu madai ya hujuma zinazopangwa kufanywa dhidi ya chama hicho. Kushoto ni Ofisa  Dawati wa CUF, Awadhi Mdoe.(Imeandaliwa na mtandao wa www.habari za jamii.com-simu namba 0712-727062)
 Ofisa  Dawati wa CUF, Awadhi Mdoe, akizungumza katika mkutano huo. Kutoka kulia ni Naibu Kamanda wa Blue Gurd, Wilaya ya Kinondoni,  Mohamed Kiotola, Mkurugenzi wa Haki za Binadamu, Zainabu Mdolwa, Mkurugenzi wa Usalama wa Chama cha Wananchi (CUF), Masoud Mhina na Mkurugenzi wa Blue Gurd wa Wilaya ya Temeke, Saidi Mtumbwe.
Wafuasi wa chama hicho wakiwa kwenye mkutano huo.


TAARIFA KWA UMMA


Wahe,Waandishi wa Habari,nimewaiteni hapa leo kwa ajili ya kuwapa Taarifa za hujuma zinazopangwa kufanywa dhidi ya chama chetu.


Kama mnavyofahamu kwamba,Chama chetu kiko katika sintofahamu ya Mgogoro wa Kiuongozi.


Hata hivyo pampja na hali hiyo kuwepo,tunaimani kwamba,sintofahamu hii ya Kiuongozi tutaumaliza wana CUF wenyewe.


Mara nyingi huwa siyo kawaida yangu kusimama hadharani kuzungumzia hali ya chama kupitia Vyombo vyenu vya habari,lakini kwa hali ilivyo nimewajibika kutokeza hadharani kuzungumza nanyi.


Kwa mujibu wa Katiba ya CUF Ibara ya 88 (2)   Nanukuu.Katibu wa Kamati ya Ulinzi na Usalama atakuwa na wajibu Ufuatao,Mwisho wa kunukuu.


Ibara ya  88 (2) (a) Atakuwa Mtendaji Mkuu wa Kamati ya Ulinzi na      Usalama ya Chama Ibara ya 87 (1)Wajibu wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Taifa ni kuhakikisha Usalama wa Chama Nchini kote


Nimeona ninukuu vifungu hivi vya Katiba ya CUF ili kuweka sawa uhalali wangu katika kutoa Taarifa hii kwenu ninyi Waandishi wa Habari.


Tunazo Taarifa kwamba,Katibu Mkuu wetu anafanya Vikao mbalimbali na Viongozi wa Chadema vyenye muelekeo wa kuhujumu harakati za chama chetu  pamoja na baadhi ya Viongozi wa CUF upande wa Tanzania Bara.


Napenda kuchukua fursa hii kumsihi Katibu Mkuu wa Chama changu,Mhe,Maalim Seif,kwamba aache kufanya hivyo kwani vikao hivyo havina tija kwake ziadi ya kujenga Uhasama dhidi ya Wanachama na Viongozi wa CUF wa Bara na Zanzibar.


Nimshauri Katibu Mkuu wangu kwamba,Viongozi wa Chadema anaowatumainia kama ndiyo wataweza kumsaidia katika dhamira zake,atakuwa anapoteza muda wake bure.


Tunazo Taarifa kwamba kuna Vijana wanaandaliwa kuja kuvamia Ofisi Kuu za CUF Buguruni  kwa ajili ya kufanya Uharibifu wa Mali za Chama.


Nichukue fursa hii pia kutoa ONYO KALI kwamba Vijana hao wasithubutu wala kujaribu kufanya kitu kama hicho kwani Ulinzi wa Chama umejipanga vyema kukabiliana vikali na Kikundi chochote ambacho kina dhamira ya kufanya hujuma yeyote dhidi ya chama chetu cha CUF.


Kuhusu kuwafanyia hujuma baadhi ya Viongozi wa Chama chetu,tunawaambia kwamba,wote wanaotaka kufanya Vitendo hivyo tunawajua mmoja mmoja na anapoishi,ila kwa sababu maalum,sitoweza kuwataja kwa sasa,lakini kwa kuwa,chama chetu kinafanya kazi kwa mujibu wa sheria za Nchi,Tayari tumevitaarifu Vyombo vya Ulinzi na Usalama vya Serikali juu ya Vitisho ya vitendo dhalimu vinavyokusudiwa kufanywa na Wasaliti wa Chama chetu dhidi ya Viongozi wetu wa Chama upande wa Tanzania Bara.


Lakini pia napenda kuchukua fursa hii kutoa Onyo pia kwa wale wanaojiita ni Viongozi wa CUF halafu wanazungumzia Uchochoroni na kuwatukana Viongozi halali wa Chama cha CUF,kwamba waache mara moja,tumewavumilia sana kiasi cha kutosha sasa dawa yao iko jikoni mmoja mmoja baada ya mwingine tutawajibika nao.


Waheshimiwa Wanahabari nawashukuru,asanteni sana kwa kunisikiliza.



HAKI SAWA KWA WOTE


Masoud Omar Mhina



MKURUGENZI WA ULINZI NA USALAMA CUF TAIFA.


No comments: