Saturday, April 15, 2017

Breaking News-Sakata la Ben Saanane Latua Umoja wa Mataifa,sasa Kuwasili Nchini Kuchunguza

 Ikiwa sakata la Kupotea kwa aliyekuwa Msaidizi wa Menyekiti wa Chadema Freman Mbowe,Ben Saanane linaendelea kugubikwa na Utata mubwa huku kila Mtanzania akitamani Kusikia kijana Huyo alipo hatimaye sakata hilo limetua Meza ya Umoja wa Mataifa ili kuwapa nafasi na wao kufanya Uchunguzi wake ili kubaini ukweli.

Leo Jijini Dar es Salaam umoja wa kizazi cha kuhoji Tanzania UTG wamezungumza na wanahabari kuhusu kupotea kwa aliyekuwa Kiongozi mwenzao katika Umoja huo ambapo yapata miezi mitano sasa hajulikani alipo huku kila Mtanzania akiwa na hofu kubwa.

Mwenyekiti wa Umoja huo Malisa Godlisen amewaeleza wanahabari kuwa wamekuwa wakifanya Juhudi kubwa za kumtafuta mwezao Bila mafanikio ikiwa ni pamoja na kuwasiliana na Jeshi la polisi kila wakati japo ameeleza kuwa wamekuwa hawapati ushirikiano mzuri unaoonyesha matumaini ya kupatikana kwa Ndugu yao Jambo linalowapa Hofu kama wanaweza kumpata Ben Saanane akiwa salama.
Malisa amesema baada ya Jitihada zao nyingi wameamua kuwasiliana na vyombo vingine vya haki Tanzania ikiwa ni pamoja na Tume ya haki za binadamu na utawala bora ambapo wamewaaandikia Barua ya kuomba wafanye uchuguzi wa wananchi wanaotekwa na wengine kukutwa wameuawa mitaani pamoja na swala la kupotea kwa kiongozi Huyo wa Chadema Ben Saanane.

Kuhusu Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu nchini Kinachoongozwa na Bi Hellen Kijo Bisimba, Malisa amesema kuwa wamefanya mazungumzo na Mkurugenzi wa kituo hicho na kukubaliana kuwaandikia malalamiko yao Umoja wa mataifa kuonyesha Ushahidi wa Kupotea kwa utata kiongozi huyo na kama wataridhika watakuja kufanya uchunguzi wao.
“Mama Helen Kijo Bisimba Juzi alihudhuria mkutano wa umoja wa mataifa ambapo aliibua Hoja ya wananchi Tanzania wanaopotea kiutata na wengine kuuawa na alijenga Hoja yake kwa Mfano wa Ben na umoja wa mataifa walishutushwa sana na Hali hiyo kwani hawakutaraji yanaweza Kutokea Tanzania,Hivyo kupitia kwa kitengo chao cha uchunguzi wa ukiukwaji wa haki cha OBSERVER wanajipanga kuanza kufanya uchunguzi wao”.ameeleza Malisa.

Malisa amesema kuwa Hadi leo Tayari wameshaandika na kutuma Barua ya malalamiko yao Umoja wa Mataifa na wanasubiri majibu ili kama wataridhika na ushahidi wao waje nchini kuchunguza sakata Hilo.


No comments: