Friday, June 2, 2017

TGNP MTANDAO YAWAPIKA MADIWANI WA KATA ZA JIJI LA DAR ES SALAAM


Leo ikiwa ni tarehe 2 ya mwezi wa 6 mtandao wa jinsia nchini TGNP umeandaa ziara fupi kwa madiwani wa kata mbalimbali za jiji la Dar es salaam lengo likiwa ni kuwapa elimu ya ujasiriamali na utawala bora. ziara hiyo ilianzia makao makuu ya mtandao huo yaliyopo mabibo jijini Dar es salaam na kwenda mpaka Kipunguni huko waliweza kupokelewa na mwenyeji wao ambeye ni diwani wa kata hiyo Bw. Mohamed R. Msophe.

Katika ziara hiyo waheshimiwa madiwani waliweza kujifunza mambo mbalimbali yahusuyo kilimo kama kilimo rahisi cha mboga mboga ambacho hakichukui nafasi kubwa na mboga hizo zinapandwa kwenye viroba vyenye mchanga mfano wa maua. Lakini pia waliweza kuona kilimo cha pili pili miwa pamoja na mahindi .
Baadhi ya madiwani wakipewa elimu na mwenyekiti wa sauti ya jamii kipunguni bw.Selemani Bishagazi juu ya upandaji wa mbogamboga kwa kutumia viroba, mifuko ya kawaida na plastiki za maji
Akiongea na waandishi wa habari pamoja na madiwani hao Mh. Mohamed Msophe ambaye ni Diwani wa kata hiyo alisema kuwa kata ya kipunguni imekuwa na maendeleo kutokana na ushirikiano uliopo kati ya viongozi na wananchi. Na wananchi wameweza kufichua maovu mengi kama kuna baadhi ya watu walikuwa wakiendeleza shughuli za ukeketaji, na pia kuweza kutoa ripoti ya gesti bubu na hatimaye aliweza kuzifunga kutokana zimesababisha mimba kwa watoto wengi na baadhi ya maovu mengine yaliyokuwa yakiendelea katika kata hiyo.
Madiwani walipotembela kituo cha Taarifa na maarifa waliendelea kupewa elimu na Bw. Selemani Bishagazi hususani ufanyaji kazi wa kituo hicho.
Lakini pia waliweza kuunda vikundi mbalimbali vya wakina mama, vijana pamoja na wananchi wote kwa ujumla lengo likiwa ni kuweza kusaidiana wote kwa kuweka fedha na baadae wanachama kuja kukopa. Hii ilisaidia kumpa nguvu diwani kwenda kuwaomba wadau mbalimbali wa sharia kuja kuwasaidia kujua haki zao na mambo mengine yanayowazunguka. Lakini pia kubwa zaidi aliweza kumtafuta mfadhili kwa ajili ya kilimo na ufugaji wa samaki kwa nguvu walionyesha mfadhili aliaidi kutoa fedha kwa mradi huo.

Katibu wa wakulima wa mbogamboga kata ya Kipunguni mtaa wa Amani Bi. Tausi S. Msangi akiwaelezea Madiwani  jinsi walivyoweza kufanikiwa katika kikundi chao kwa kutumia picha. 
Na kingine diwani huyo aliweza kuwaunganisha vijana ambao walikuwa hawana kazi na wengine walikuwa vibaka kuweza kuwapa fedha kwa ajili ya kilimo na kwa sasa wameshanunua shamba morogoro na kilimo kinaendelea. Pia  vijana wa boda boda na bajaji aliweza kuwatengenezea umoja ambao umekuwa na faida kubwa na unaweza kuwaingizia faida ya hadi laki na nusu kwa mwezi kwa michango yao ya shilingi elfu moja kwa kila mwanachama katika kikundi hicho.

Madiwani hao waliweza kushukuru mtandao wa jinsia Tanzania (TGNP)kwa kitu kizuri walichokifanya na walisema wamejifunza mengi sana na kuaidi kuyafanyia kazi waliyoyapata kwenye semina na mpaka kwenye ziara hiyo. Na pia wametoa ahadi ya kuleta mrejesho endapo wataitwa tena mwakani ili kuweza kuwajuza wanamtandao mafanikio watakayoyapata kutokana semina hiyo.

Madiwani na viongozi wengine wakifuatilia kwa umakini mchanganuo wanaopewa na muwezeshaji
Deogratius Temba muwakilishi wa TGNP kushoto na Diwani wa kata kipunguni kati Bw. Mohamed R. Msophe na Daniel Malagashimba kulia wakifuatilia kwa umakini shuhuda zilizokuwa zikitolewa na wananchi wa kata hiyo.
Diwani wa kata ya Kipunguni Bw. Mohamed Msophe akiongea na madiwani pamoja na waandishi wa habari mapema leo katika kata yake kipunguni jijini dar es salaam
Diwani wa kata ya Makongo Bi.Ndeshukurwa Tungaraza akitoa ushuhuda kuhusu alichojifunza katika semina hiyo.
Rose A. Moshi akielezea alichokipata kwenye semina pamoja na ziara hiyo iliyoanadaliwa na TGNP mtandao.
Mjumbe wa TGNP mtandao Bw. Deogratius Temba akifunga mkutano huo uliofanyika mapema leo Kipunguni jijini Dar es salaam
Picha ya pamoja kati ya Madiwani toka kata mbalimbali za jiji la Dar es salaam na wakazi wa kata ya kipunguni

Pili pili ni miongoni mwa mazao yanayolimwa kipunguni huu ni mfano mzuri wa kuigwa kwa wakazi wa maeneo mengine.

Shamba la migomba na pili pili kipunguni Dar es salaam




No comments: