Thursday, July 6, 2017

AJALI - UPENDO COACH LAUA WAWILI NA WENGINE ZAIDI YA WANNE KUJERUHIWA MBALARI MBEYA


MBALARI, MBEYA: Watu wawili wamefariki dunia na wengine wanane kujeruhiwa baada ya basi walilokuwa wakisafiria la kampuni ya Upendo kuacha njia na kupinduka eneo la Malimboji-Igawa wilayani Mbalari.


Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Augustino Senga amesema ajali hiyo imetokea leo (Julai 6) saa 2:15 asubuhi.

Amesema chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi wa dereva ambaye alikimbia baada ya ajali kutokea. Basi hilo lilikuwa likitoka Mbeya kwenda Dar es Salaam.

Senga amewataja waliokufa kuwa ni Emmanuel Obeid mkazi wa Chimala mkoani Mbeya na mwingine aliyetambuliwa kwa jina moja la Shahib, mkazi wa jijini Mbeya.

Amesema majeruhi wamepelekwa katika Hospitali ya Misheni ya Chimala na ya Wilaya ya Mbarali iliyopo mjini Rujewa kwa matibabu.

Katibu wa Afya wa Hospitali ya Misheni Chimala, Shadrack Kasiba amesema wamewapokea majeruhi wanne na maiti mmoja.

No comments: