Thursday, July 6, 2017

Halmashauri Zashauriwa Kuiunga Mkono Serikali Katika Tanzania ya Viwanda

Halmashauri nchini zimetakiwa kutumia vyema fedha zinazotengwa kwa ajili ya kundi la vijana na wanawake katika kuunga mkono dhamira ya Serikali ya Awamu ya Tano ya kuifanya Tanzania inakuwa nchi ya Uchumi wa Kati na Viwanda.

Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Charles Mwijage akiwatambulisha Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam Mhe. Issaya Mwita (kulia) na Meya wa Manispaa ya Kinondoni Mhe. Benjamin Sitta kwa ugeni kutoka Oman walipotembelea katika Maonesho ya 41 ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam (DITF) leo.

Hayo yamebainishwa leo na Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam alipotembelea Maonesho ya 41 ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam (DITF) mabapo katika ziara hiyo aliambatana na Mstahiuki Meya wa Manispaa ya Kinondoni Bw. Benjamin Sitta.

“Taasisi za kifedha zinao wajibu mkubwa katika kufikia adhima hii ya Serikali, lakini sisi Serikali za mitaa, Halmashauri ziano wajibu mkubwa kuhakikisha zilie asilimia tano za vijana na tano za wanawake zinakuwa sehemu ya kuchochea ufanikishaji wa dhamira njema ya Serikali,” alisema Mhe. Mwita.

Aidha Mhe. Mwita ametoa pongezi kwa uongozi wa Tantrade kutokana na jitihada zao za kuhakikisha wanasaidia ukuaji wa bidhaa za ndani hasa bidhaa za ngozi ambapo alisisitiza ni vyema wakaendelea kuweka mkazo katika eneo hilo kabla ya kuangalia maeneo mengine.

Kwa upande wake Meya wa Manispaa ya Kinondoni Mhe. Benjamin Sitta amesema kuwa Maonesho hayo ya Sabababa yamekuwa na manufaa kwa wafanyabiashara wengi na hata kwa wananchi kuja kujifunza.

Aliongeza kuwa pamoja na wananchi kuja kujifunza lakini pia imekuwa ni fursa kwa wafanyabiashara kutengeneza mahusiano na wafanyabiashara wenzao kutoka nchi nyingine jambo ambalo katika biashara ni muhimu sana.

Nae, Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE) Edwin Ratageruka amesema kuwa dhamira yake ni kuhakikisha bidhaa za ndani zinakuwa na soko la uhakika ndani na nchi ya nchi.

Ameongeza kuwa kwa kuanzia wamejikita zaidi katika bidhaa za ngozi ikiwa ni njia pia ya kuwainua wafugaji ambao mazao ya mifugo yao yanatumika katika kutengeneza bidhaa mbalimbali za ngozi.

 “Serikali inatambua umuhimu wa kuthamini bidhaa za ndani, ndiyo sababu Ofisi ya Waziri Mkuu iliratibu zoezi ambalo jumla ya vijana 1000 walipatiwa mafunzo ya usindikaji na ushonaji wa ngozi, katika mafunzo yaliyofanyika Chuo cha Teknolojia Dar es Salaam tawi la Mwanza,” alisema Rutageruka.

Rutageruka ameongeza kuwa katika kuendeleza jitihada hizo Gereza la Karanga (Moshi) na Kampuni ya Woisso ya Jijini Dar es Salaam zinatarajia kuanzisha viwanda kwa ajili ya kutengeneza sole ili kuachana na utaratibu wa kuagiza skutoka nje.


Maonesho ya 41 ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam yanafanyika huku azma ya Serikali ya Awamu ya Tano ikiwa ni kuhakikisha Tanzania inakuwa nchi ya uchumi wa kati na viwanda, kutokana na dhamira hiyo maonesho haya yamepewa kauli mibu isemayo; “Ukuzaji wa Biashara kwa Maendeleo ya Viwanda.”


Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni Benjamin Sitta akisalimiana na Meneja Masoko na Mawasiliano wa Mfuko wa Pensheni wa Serikali za Mitaa (LAPF), Bw. James Mlowe alipotombelea banda la Mfuko huo wakati wa Maonesho ya 41 ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam (DITF) leo. Katikati ni Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam Mhe. Issaya Mwita.

Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam Mhe. Issaya Mwita akimwelezea jambo Mkurugenzi Mkuu wa SIDO Tanzania Mhandisi. Profesa Sylivester Mpanduji alipotembelea banda lao katika Maonesho ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam (DITF) leo. Kushoto ni Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni Mhe. Benjamin Sitta.

Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam Mhe. Issaya Mwita na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni Mh. Benjamin Sitta wakitazama ramani ya miradi ya makazi inayojengwa katika eneo la Kigamboni na Kampuni ya Internatinal Property walipotembelea banda la Kampuni hiyo katika Maonesho ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam (DITF) leo. Kulia ni Afisa Uhusiano wa Kampuni hiyo Bw. Saleh Omar Saleh

Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam Mhe. Issaya Mwita na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni Mh. Benjamin Sitta wakipata maelezo ya huduma mbalimbali zinazotolewa na Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) walipotembelea banda la Kampuni hiyo katika Maonesho ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam (DITF) leo

Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam akipata huduma ya kupima urefu mara baada ya kupima presha alipotembelea banda la Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) katika Maonesho ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam (DITF) leo

Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam Mhe. Issaya Mwita(kulia) na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni Mh. Benjamin Sitta (kulia kwake) wakisikiliza namna mfumo wa Automotive unavyofanyakazi banda la VETA  katika Maonesho ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam (DITF) leo. Katikati ni Meneja Uhusiano wa VETA Bw. Peter Sitta.



No comments: