Monday, July 24, 2017

VIDEO MPYA YA RICH MAVOKO FT FID Q - SHERI

Tukizungumzia wasanii wanaofanya muziki mzuri kwenye game ya Bongo basi hatuwezi kumuacha Rich Mavoko, ni miongoni mwa wasanii wenye uwezo mkubwa wa kutumia sauti zao kwa kuweka vionjo vinavyopendezesha wimbo.

Mavoko ambaye muda sio mrefu sana alijiunga na kindi la WCB Wasafi linaloongozwa na Diamond Platnumz huu ni wimbo wake wa tatu kuachia akiwa kwenye kundi hilo, wimbo wa kwanza ukiwa Ibaki story na wa pili ni Kokolo na sasa amekuja na Sheri wimbo aliyomshirikisha Fid Q.

No comments: