Wednesday, August 2, 2017

ALICHOKIAMUA DC HAPI KWENYE MGOGORO WA WAKAZI ZAIDI YA 3900 WA WAZO

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Ally Salum Hapi ametoa miezi mitatu kwa kampuni ya upimaji wa ardhi ya Afro Map kuhakikisha wanamaliza upimaji wa ardhi kwa eneo la Nakelekwe, Mtaa wa Nakasangwe Kata ya Wazo ambalo limekuwa na mgogoro wa ardhi kwa muda wa miaka 13 tangu mwaka 2004 baina ya wakazi wa eneo hilo na wamiliki wa mashamba.


DC Hapi ameongeza kuwa wananchi wa maeneo hayo wasiyauze maeneo hayo mpaka upimaji utakapo fanyika, na wale ambao maeneo yao hayo kuwa katika mgogoro wafanye hivyohivyo.

Vilevile DC Hapi ameeleza kuwa serikali haiwezi kuacha wakazi 3900 wakipoteza maeneo kisa uwepo wa mashamba, ndiyo maana ameamua kuzikutanisha pande zote mbili ili waweze kutatua migogoro hiyo, na upimaji utakapofanyika vitapatikana viwanja 6000 ambapo pande zote mbili zitanufaika bila kubagua na maeneo mengine yatatengwa kwaajili ya huduma za jamii ikiwemo zahanati, shule na miundombinu ya barabara.

Pia DC Hapi amewataka viongozi wa kisiasa kuacha kuchochea migogoro ya ardhi kwa maslahi yao ya kisiasa na endapo wakiendelea kufanya hivyo atachukua hatua stahiki dhidi yao.





No comments: