Thursday, October 25, 2012

MWALIMU WA TLC ASEMA HAWAKO TAYARI KUWAONGEZEA WANAFUNZI SIKU ZA KUSOMA

 



asisitiza wasiokuwa na gazeti tando (blog)ita kula kwao.

    >awasifu  wanafunzi kwa kuonyesha nidhamu kwa kipindi chote cha mafunzo..

Mara baada ya uvumi uliokuwa ukisambazwa  na baadhi ya wanafunzi, wanaopata mafunzo kwa vitendo katika kituo cha mafunzo kwa vitendo( TLC). Uvumi huo  umepingwa  vikali na mmoja wa viongozi wa kituo hicho kwa kubainisha kuwa hawafikirii, na hawana mawazo ya kuongeza muda kwa madai kuwa wao wanafanya kazi kwa kufata ratiba ya utendaji kazi wa kituo hicho.

Akizungumza na mwandishi wa habari jana ofisini kwake jijini Dar es salaam, meneja biashara wa kituo hicho Bw. Dastan Kamanzi  alisema kuwa uvumi huo hauna chembe hata moja ya ukweli, kwa kuwa wao wanafanya kazi kwa kufuata ratiba ya kituo hicho” swala hilo la kuongeza muda halina ukweli wowote kwa sababu tunafata ratiba na tunakazi  nyingi za kufanya pia muda uliokuwa umepangwa umekwisha na tutakuwa na kazi ya  kuandaa matokeo ya wanafunzi “alisema kamanzi.na kuongeza kuwa wao hawana lengo la kumfelisha  mtu bali haki itatendeka kwa kila kazi iliyofanywa na mwanafunzi.

Akizidi kufafanua kwa undani zaidi  jinsi mafunzo yalivyoendeshwa kwa kipindi   cha miezi mitatu, kamanzi alisema  kuwa wamefundisha kila kitu ambacho walitakiwa kukifundisha  hivyo hakuna mada iliyoachwa kwani wao wanafundisha kwa kufuata mtaala, “kila mwalimu amefundisha mada zote kama inavyotakiwa. Akitolea  mfano kwenye somo la new media kila mwanafunzi  kafundishwa jinsi ya kufungua blog, sasa kuna haja gani ya kuongeza muda wakati kila kitu kimefundishwa” alisema kamanzi, pia alikemea tabia ya wanafunzi wanaofungua blog kwa lengo la kupata alama pasipo kujua kuwa zina faida kubwa kwao kama wakiziendeleza“ kuna wanafunzi wakisha sahihishiwa na kupewa alama zile blog zao wanaziacha hivyo si vizuri kwani  blog wakiziendeleza  wanaweza kujipatia kipato kwa kuweka matangazo ya watu mbalimbali  lakini wao hawalijui hilo” aliongeza kamanzi.

Akiendelea kutoa ufafanuzi kwa undani zaidi na jinsi wanavyopata  changamoto walizokutana nazo Bw. Kamanzi alisema kuwa darasa la awamu hii halikuwa na matatizo, kama ya awamu iliyopita kutokana na wanafunzi kuwa na nidhamu ya hari ya juu. Na kutolea mfano suala  la wizi na kugombana matatizo ambayo yalijitokeza katika awamu iliyopita, pia alitoa wito kwa wanafunzi wasio kuwa na brog kuwa nazo kwani kutokuwa nazo kutawapunguzia alama na  kuwataka wanafunzi ambao hawajamaliza kazi zao kukamilisha na kuzipeleka kwa walimu husika.

Nae mwanafunzi  wa kituo hicho Exuad Mtei alisema kuwa uvumi huo haukumuathili  kitu chochote kitaaluma kwa kuwa hadaiwi kazi yoyote na mwalimu” mimi waongeze muda  wasiongeze sina shida kazi kwao ambao kawajamaliza kazi za walimu wao. Pia naunga mkono kauli ya kutoongeza mda kwa sababu hata mimi nina shughuli zangu za msingi  nahitaji  kuzifanya wakiongeza muda wataniharibia ratiba” alisema Bw. Mtei, huku baadhi ya wanafunzi  wakikataa kulizumngumzia suala hilo.

Kituo cha mafunzo kwa vitendo kwa wanafunzi wa chuo cha uandishi wa habari TIME (TSJ) kilianzishwa  mnamo mwaka  2010, chini ya udhamini wa mwaka mmoja kutoka Tanzania Media Fund ( TMF).Nia na Madhumuni  na lengo la kuwafundisha wanafunzi kwa vitendo. Katika Nyanja mbalimbali za Utangazaji,kama vile Radio, Television production, Printing na photo journalism kwa wanafunzi wa Stashada ya nne.   

 

No comments: