Tuesday, September 20, 2022

Viongozi wa Siasa Wakumbushwa Kuacha Kuwagawa Wananchi Kwa Maslahi yao Binafsi.

Na Vicent Macha

Wito umetolewa kwa Wanasiasa nchini kuacha tabia ya kuwagawa wananchi nabadala yake waendeleze misingi ya Aamani,Umoja na Maendeleo iliyoachwa na Muasisi wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Wito huo umetolewa leo Dar es salaam na Jaji Mstaafu Joseph Sinde Warioba kwenye kikao cha kubadilishana Uzoefu na Ujuzi kilichoandaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere nakuwakutanisha wadau mbalimbali ikiwemo viongozi wa vyama vya siasa,lengo likiwa  ni kujadili misingi iliyoachwa na viongozi wa Taifa tangu kupata uhuru mwaka 1961.

Amesema kuwa viongozi wa kitaifa walifanya imani kuwa wananchi wote ni sawa ,nakwamba baada ya kupata uhuru viongozi hao  hawakuona umuhimu wa nchi kuwa huru huku wananchi wakiwa hawako huru,hivyo walihakikisha wanasimamia misingi ya Amani,Umoja na Maendeleo ili kulifanya Taifa la Tanzaia kuwa na Umoja.

"Tusiwagawe wananchi,tuhakikishe tunalinda misingi ya amani,umoja na maendeleo iliyoachwa na Viongozi wetu wa kitaifa waliopambana hadi tukapata uhuru,hivyo tunapaswa kuwa na nchi huru yenye watanzania huru."amesema Jaji Warioba.

Awali Mwenyekiti wa Taasisi hiyo Joseph Butiku amesema kwamba Hayati baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere enzi ya uhai wake amekuwa akisimamia misingi ya Amani,Umoja na Maendeleo hivyo viongozi wa vyama vya siasa hawana budi kushirikiana kwa pamoja kuondoa changamoto zinazowakwaza watanzania katika kuwaletea maendeleo.

Kwa upande wake kadhalika Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM ) Bara Christina Mndeme amewambia waandishi wa habari kuwa mdahalo huo ulioandaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere umewasaidia kupata mawazo ya namna yakuendeleza  misingi ya amani,Umoja na Maendeleo iliyoachwa na Hayat baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
\
                                                                   Habari Picha.
Jaji Mstaafu Joseph Sinde Warioba akiongea na Baadhi ya Wajumbe kutoka vyama mbalimbali katika Kongamano liliandaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere mapema leo Mkoani Dar es salaam.
Mwenyekiti wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere Joseph Butiku akiongea katika Kongamano lililoandaliwa na Taasisi hiyo.
Baadhi ya Viongozi wa dini wakifuatilia matukio katika Kongamano lililoandaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere mapema leo mkoani Dar es salaam.
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM ) Bara Christina Mndeme akiongea katika kongamano la kubadilishana uwezo kati ya Viongozi wa vyama mbalimbali vya Siasa na Asasi za Kijamii.
Kongamano likiendelea.




\



Friday, September 9, 2022

TALGWU yaiomba Serikali kufanya Mabadiliko Tozo Miamala ya Kibenki

Na Isaac Thadeo

CHAMA cha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa Tanzania (TALGWU) kimeiomba Serikali kufanya mabadiliko katika sheria ya tozo za miamala ya kibenki ili kuepuka malipo ya mara mbili kwenye mshahara wa mtumishi wa umma. 
Mkuu wa Idara ya Habari na Uhusiano wa Kimataifa wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa Tanzania (TALGWU) Shani Kibwasali akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam.
Ombi hilo limetolewa leo Jijini Dar es Salaam na Mkuu wa Idara ya Habari na Uhusiano wa Kimataifa-TALGWU Shani Kibwasali akizungumza na waandishi wa habari kuhusu taarifa ya utekelezaji wa shughuli za Chama kwa kipindi cha Januari hadi Juni 2022.

Shani amesema tozo hizo zinazidi kumbebesha mzigo na kumkandamiza mfanyakazi huku ikizingatiwa mishahara wanayopata haikidhi mahitaji ya kila Siku na familia zao. 

“Pia naomba nizungumzie suala la tozo za kibenki lililoanza kutekelezwa hivi karibuni. Tozo hizi zinawaathiri sana wanachama Wetu. Ikumbukwe kwamba watumishi wa umma kila mwezi wanalipa Kodi kwa kukatwa katika mishahara yao,” amesema Kibwasali na kuongeza kwamba,

“Lakini sasa kuanza kuanza kutekelezwa kwa tozo ya Serikali kwa miamala ya kutoa na kuhamisha fedha katika benki inamfanya mtumishi wa umma kutozwa zaidi ya mara mbili katika Pato moja kwa mwezi,”.

Kuhusu suala la nyongeza ya mishahara, amesema ni ukweli usiofichika kwamba wanachama wao ambao ni wahanga wakubwa kwani bado wanamanung’uniko na TALGWU kama msemaji wao hawajaridhika kabisa kwa jinsi nyongeza ya mshahara ilivyofanyika.

“Ila naomba niwatoe hofu wanachama wetu kwamba suala hili linashughulikiwa na Chama kwa kushirikiana na shirikisho la vyama huru vya Wafanyakazi nchini (TUCTA),” ameeleza Kibwasali.

Akizungumzia kuhusu mafanikio ya TALGWU kwa kipindi cha Januari hadi Juni mwaka huu, amesema kwamba hadi kufikia Juni 2022 walikuwa na jumla ya kesi 140 ambapo mawakili wa Chama wanasimamia kesi 100, mawakili wa nje wanasimamia kesi 13, na rufaa zilizopo Tume ya Utumishi wa Umma ni 27.

Kwamba Chama kiliandaa utetezi kwa watumishi 12 waliokuwa wamepewa mashataka na waajiri. Hivyo amesema kati ya kesi 140 walizonazo zilizoisha zilikuwa ni 39 na chama kimeshinda jumla ya kesi 35 na kushindwa kesi nne huku kesi nyingine zikiendelea Mahakamani.

Kibwasali amebainisha kuwa katika kipindi hicho pia TALGWU ilikuwa na jukumu jingine kubwa la kushughulikia haki na stahiki za wanachama ambazo kimsingi zipo kwa mujibu wa sheria ya Utumishi wa Umma na kanuni zake.

Hivyo amesema TALGWU inajivunia kuona Serikali imetekeleza maombi yao katika maeneo ya upandiahaji vyeo na mishahara, malipo ya malimbikizo ya mishahara na utawala Bora.