Saturday, May 31, 2014

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AZINDUA WIKI YA MAZINGIRA DUNIANI KWA KUPANDA MITI KATIKA KAMBI YA KIKOSI CHA JESHI LA KUJENGA TAIFA RUVU.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipanda mti katika eneo la Kambi ya Jeshi la Kujenga Taifa, JKT Ruvu, ikiwa ni sehemu ya uzinduzi wa Wiki ya mazingira Duniani. jumla ya miti 8,000 inatarajia kupandwa katika eneo hilo. Picha na OMR

Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mwantum Mahiza, akipanda mti katika eneo la Kambi ya Jeshi la Kujenga Taifa, JKT Ruvu, ikiwa ni sehemu ya uzinduzi wa Wiki ya mazingira Duniani. jumla ya miti 8,000 inatarajia kupandwa katika eneo hilo. Picha na OMR

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiweka Jiwe la msingi baada ya kupanda mti katika eneo la Kambi ya Jeshi la Kujenga Taifa, JKT Ruvu, ikiwa ni sehemu ya uzinduzi wa Wiki ya mazingira Duniani. jumla ya miti 8,000 inatarajia kupandwa katika eneo hilo. Picha na OMR

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na baadhi ya maafisa wa Kambi ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT Ruvu, wakati akiondoka eneo hilo baada ya kupanda miti kama ishara ya uzinduzi wa Wiki ya Mazingira Duniani, leo Mei 31, 2014. Picha na OMR

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na Maafisa wa Jeshi wa kambi ya JKT Ruvu baada ya kupanda miti. Picha na OMR

HABARI ILIYOTIKISA JIJI---RAIS KIKWETE ATAJWA KUHUJUMU MCHAKATO WA KATIBA MPYA,WANANCHI WASEMA AMEWASALITI.SOMA KIUNDANI HAPA

Wachokoza mada katika mdahalo huo ambao umemalizika muda mchache uliopita,mwanzo ni awadhi ally,Ayubu Rioba,Onesmo olenguruma,na Mwesiga baregu
 Na Karoli Vinsent

        WANANCHI mbalimbali wamtaja Rais Jakaya kikwete kuwa ni kikwazo kikubwa cha upatikanaji wa Katiba Mpya ,kutokana na kushindwa kusimammia misimamo yake mwanzo ambayo ilikuwa inamalengo ya kupatikana katiba mpya ya Wananchi.

        Hayo,yamegundulika mda huu kwenye Mdahalo wakujadili Katiba mpya,uliondaliwa na Umoja wa Asasi za kirai (AZAKI)uliofanyika jijini Dar es Salaam,mdahalo huo ambao uliwahusisha Wananchi wa Kawaida pamoja na Wasomi Mbalimbali.

       Katika Mdahalo huo wananchi wameonekana Dhahiri kumshutumu Rais jakaya Kikwete kwakushindwa kusimamia misimamo yake ya mwanzo ambayo ilikuwa  inalengo la kupatikana Katiba mpya ya Wananchi  bila Upendeleo,ambapo sasa ameonekana kubadilika na kuanza kushikilia Misimamo yake ya Chama  cha Mapinduzi CCM, ambayo inakuwa kinyume na sasa.
Watanzania waliojitokeza katika mdahalo huo
          Kwa upande wake Msomi na mchambuzi wa Masuala ya kisiasa Nchini kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino Profesa Mwisiga Baregu.alisema Rais kikwete amefanya usaliti mkubwa sana kwa wananchi kwa kitendo chake kuanza kufuata maoni ya chama chake.
“Kiukweli mimi sikutegemea Rais kikwete angefanya usaliti namna hii kwenye mchakato huu wakatiba, wakati mimi sikutegemea .Kwanza wakati kila hatua tuliyokuwa tunaifanya kwenye mchakato huu wakatiba tulikuwa tunamjulisha halafu na yeye alikuwa anaungana na sisi kwa kazi tuliokuwa tuanafanya”

       “Lakini tunashangaa yeye amebadilika na kuanza kufuata misimamo ya chama chake,na huku ndiko alipoanza kuharibu mchakato mzima wa ujio wa Katiba mpya.Alisema Baregu.
Baregu,ambaye ni Kada kutoka Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA,alizidi kusema kitendo cha wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba kutoka Chama cha Mapinduzi CCM.
Kuendelea  kujadili Rasimu ya Muundo wa Serikali mbili ni kuvunja kanuni ya mabadiliko ya katiba kifungu cha 25,ambacho kinataka wajumbe wa Bunge hilo kutojadili Rasimu ya Kwao.
Kwa Upande wake Mwenyekiti wa Jukwaa la katiba Nchini,Deus Kibamba,aliwataka wananchi kushirikiana na AZAKI ,kutetea katiba yao na kutowaacha wanasiasa kuhodhi mchakato mzima wa Katiba.
Vilevile Mwanasheria na mwenyekiti wa chama cha Wanasheria Zanzibar Hawadhi Ally, ambapo yeye alikuwa miongoni mwa  Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba,alisema Rais Jakaya Kikwete ndio mtu wa kulaumiwa kwa wananchi kwa kitendo chake cha kuanza kufuata matakwa ya Chama chake ambao wamekuwa kinara wakubwa wakipinga maoni ya tume ya Jaji warioba.
Mwenyekiti wa jukwaa la katiba tanzania Deus Kibamba akitoa maoni yake kama mwananchi katika mdahalo huo uliomalizika muda mfupi uliopita
  
Naye Mwenyekiti wa Taasisi isiyokuwa ya kiserikali,inasimamia Muenendo wa Shuguli za Bunge nchini,Marcus Albanile,aliwataka wananchi kuacha upole wa kuigopo Serikali ya Rais Kikwete,  ambayo imekuwa hikihalibu mchakato wa katiba mpya na akawataka wananchi kuandamana na kulala barabarani na kudai katiba mpya.
Ikumbukwe, Midahalo hii ya kuwapa wananchi fursa ya kujadili katiba mpya imeandaliwa na Umoja Asasi zisizokuwa za Kiserikali AZAKI,ambao umoja huo unawakilisha Asasi hizo zaidi ya mia tano.


Friday, May 30, 2014

KITUO CHA DALADALA MWENGE KUFUNGWA RASMI JUMAPILI HII YANI KESHO

Wamiliki, madereva na abiria wote mnatangaziwa kuwa kituo cha daladala Mwenge kitafungwa rasmi siku ya Jumapili jioni tarehe 01.06.2014. Kuanzia siku ya jumatatu asubuhi tarehe 02.06.2014 kituo kitakachokuwa kinatumika ni Makumbusho tu.

KAMA ULIKOSA HOTUBA YA WIZARA YA NISHATI NA MADINI JANA HII HAPA

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI TAR 31.05.2014 VICHWA VIKUBWA BUNGE LISITUMIWE NA MAFISADI,VIJISENTI VIMEVURUGA WABUNGE NA UZEMBE SERIKALINI UNAKERA-KINANA

BREAKING NEWZZ : GEORGE TYSON AFARIKI DUNIA KATIKA AJALI MBAYA YA GARI MKOANI MOROGORO--TZAMA PICHA ZA GARI LAO NA PICHA ZAO KABLA YA AJALI--R.I.P TYSON

George Tyson

George Tyson
Muongozaji mkongwe wa filamu nchini Tanzania  mwenye asili ya Kenya, George Tyson amefariki Dunia baada ya kupata ajali mbaya ya gari   wakati wakitokea kwenye hafla ya kuadhimisha miaka miwili ya kipindi cha luninga cha The Mboni Show mkoani Dodoma kufuatia gari walilokuwa wakisafiria aina ya Toyota Noah kupasuka matairi   na kuangukaeneo la Gairo mkoani Morogoro majira ya saa moja jioni.
Katika gari hilo walikuwa watu 8 ila yeye pekee ndio aliyepoteza maisha na wengine kupata majiraha mwilini pamoja na dereva wa gari hilo. Kwa sasa mwili wa marehemu umehifadhiwa hapa Morogoro katika  hospital ya mkoa Morogoro, baadae asubuhi mwili utaanza safari ya kurudi Dar es Salaam
Awali Tyson aliwahi kuwa mume wa muigizaji nyota wa kike wa Bongo Movie, Yvonne Cherry ‘Monalisa’ aliyeza nae mtoto mmoja wa kike anayeitwa Sonia.
Atakumbukwa kwa ucheshi, ukarimu na busara zake, Mungu ailaze Roho ya Marehemu Mahali pema peponi Ameen.

Gari alilopata nalo ajali Director George Tyson na picha za saa 4 kabla ya tukio

Dj Choka ambae kwa sehemu kubwa alikua kwenye safari moja ya Dodoma na Marehemu George Tyson, ameandika kwenye
Screen Shot 2014-05-31 at 3.46.30 AM
Screen Shot 2014-05-31 at 3.46.12 AM
Screen Shot 2014-05-31 at 3.46.38 AM
Screen Shot 2014-05-31 at 3.46.50 AM
Kwenye hii safari, George Tyson aliambatana na mtangazaji Mboni Masimba wa The Mboni show.
Screen Shot 2014-05-31 at 3.46.58 AM


KAMA ULISKIA ILE STORY YA KATIBU MKUU WA CCM KINANA KUGOMBEA URAIS MWAKANI--UNDANI WAKE HUU HAPA

Na Karoli Vinsent

       KATIBU wa chama cha Mapinduzi CCM,Abdulrahman Kinana,anatarajiwa Kugombea Urais kwenye Uchaguzi mkuu mwakani  2015.

Taarifa hizo ambazo Mtandao huu umedokezwa,zinasema  kitendo cha Katibu mkuu huyo kuingia kwenye Kinyanganyiro hicho zinalenga Kuwanyamazisha Makada mbalimbali ndani ya Chama hicho ambao wamekuwa wakitumia kila Njia kuhakikisha wanashika nafasi hiyo ya Urais kwenye uchaguzi mkuu mwakani.

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AKUTANA NA WAZIRI WA MAMBO YA CHI ZA NJE WA UTURUKI

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Uturuki, Ahmet Dovutoglu, baada ya mazungumzo yao yaliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, leo Mei 30, 2014. Picha na OMR
 Makamu wa Rai wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Uturuki, Ahmet Dovutoglu, aliyeongozana na ujumbe wake wakati walipofika Ofisini kwa Makamu Ikulu jijini Dar es Salaam kwa mazungumzo leo, Mei 30, 2014.  Katika mazungumzo yao walisisitiza juu ya ushirikiano katika Nyanja mbalimbali baina nchi hizi mbili .  Waziri huyo yupo nchini kwa ziara ya Kiserikali iliyoandaliwa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ya Tanzania kwa kushirikiana na Wizara ya Mambo ya Nje ya Uturuki. Picha na OMR


HALFA YA KUKABIDHI MTAMBO WA MFUMO WA MAWASILIANO WA MASAFA MAREFU KWA JESHI LA MAJI YAFANYIKA

Balozi wa Marekani Nchini Lt.Kevin Balisky akisoma risala mbele ya mgeni rasmi Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani Pereira Silima wakati wa halfa ya kukabidhi  mtambo wa mfumo wa mawasiliano wa masafa marefu kwa jeshi la maji, masaada huo umetolewa na Serikali ya Marekani kupitia mradi wa AFRICO,leo jijini Dar es salaam.
pix 3 (1)Naibu Waziri wa Mambo ya ndani, Pereira Silima (kulia) akizindua mfumo wa mawasiliano wa masafa marefu kwa kikosi cha askari wa maji katika halfa iliyofanyika  leo jijini Dar es Salaam, kushoto ni  Balozi wa Marekani nchini, Lt. Kevin Balisky,mtambo huo umetolewa na Serikali ya  Marekani kupitia mradi wa AFRICO kwa ajili ya kusaidia kudhibiti uhalifu wa majini na kuweza kutambua vyombo na shughuli zote zitakazofanyika katika maji.

KATIBU MKUU KIONGOZI AKUTANA NA NCHI WASHIRIKA WA MAENDELEO JIJINI DAR ES SALAAM LEO

 Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue akibadilishana mawazo na mabalozi na wawakilishi wa nchi washirika wa maendeleo kabla ya  mkutano aliowaandalia leo Mei 30, 2014 katika hoteli ya Hyatt Kilimanjaro hotel jijini Dar es salaam kuzungumzia  michango katika Kapu la Afya (Health Basket Fund) pamoja na mpango wa serikali wa kuiingiza sekta ya afya katika  kutekeleza Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN)
se3Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue (wa saba kutoka kushoto) akiwa katika mazungumzo  na mabalozi na wawakilishi wan chi washirika wa maendeleo katika mkutano aliowaandalia leo Mei 30, 2014 katika hoteli ya Hyatt Kilimanjaro hotel jijini Dar es salaam kuzungumzia  michango katika Kapu la Afya (Health Basket Fund) pamoja na mpango wa serikali wa kuiingiza sekta ya afya katika  kutekeleza  Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN)
PICHA NA IKULU

BANK YA POST YAINGIA MAKUBALIANO NA SIMBA NA YANGA MCHANA HUU,CHEKI PICHA HAPA--RAGE AONEKANA

Benk ya posta tanzania imeingia makubaliano na timu ya simba na yanga katika kushirikiana katika malipo kupitia washabiki na wapenzi wa timu hizo ambapo kila shabiki wa timu hizo watakuwa na kadi za benk hiyo,jambo ambalo mashabiki hao watakuwa wakuchangia michango yao kupitia benk hiyo,BAADHI YA PICHA

Tutashirikiana

Mwenyekiti wa Simba, Isimal Aden Rage wapili kulia na Makamu wa rais wa Yanga, ClementSanga, wakifungua pazia kuashiria ukuzindua rasmi wa wanacha wa timu mbili hizo kutumia kadi za Benki ya Posta kushoto ni Naibu Waziri wa  Utamaduni na michezo, Juman Mkamia, uzindi huo umefanyika Dar es Salaam leo

JUKATA WATOA TATHMIN YAO JUU YA UCHAGUZI WA MALAWI NA AFRICA YA KUSINI.SOMA HAPA

Mwenyekiti wa JUKATA DEUS KIBAMBA akizungumza na wanahabari mapema leo jijini dar es salaam
        Jukwaa la katiba Tanzania JUKATA leo limetoa tathmini  yake juu ya chaguzi mbili zilizofanyika katika nchi za Malawi na Africa ya kusini mwezi uliopita huku wakionyesha kuipongeza sana nchi ya Africa ya kusini kwa kufanya uchaguzi wa haki na huru tofauti na nchi ya Malawi
        
        Akizungumza leo jijini dare s salaam mwenyekiti wa jukwaa  hilo DEUS KIBAMBA amesema kuwa wao kama jukwaa waliweka kambi katika nchi hizo mbili,kwa lengo la kuangalia uchaguzi huo
Kaimu mwenyekiti wa jukata HEBRON MWAKAGENDA
          KIBAMBA anasema kuwa ni wazi kuwa hali ya nchi hizo mbili kiuchumi ni tofauti sana jambo ambalo pia limechangia kufanya chaguzi zao pia kutofautiana sana,ikiwa ni pamoja na tume ya uchaguzi ya Malawi kuonyesha kuwa haikuwezeshwa kiswasawa katika kusimamia uchaguzi huo jambo ambalo nchini Africa ya kusini halikuwa hivyo.
        
         “Tume ya uchaguzi ya Africa ya kusini imeonyesha kuwajali sana wapiga kura hadi kufikia hatua ya kuwajali walemavu ambao wasingeweza kufika vituoni na kuwafwata walipo ili wapige kura.”amesema KIBAMBA
          
         Kuhusu hamasa ya wananchi ya kupiga kura JUKATA wamesema kuwa wananchi wa Africa ya kusini walikuwa na hamasa sana tofauti na wale wa Malawi jambo ambalo limechangiwa na hamasa pia iliyofanywa na serikali kwa ujumla.
Wanahabari wakisikiliza kwa makini
             Akizungumzia  swala la rais wa Malawi kufuta matokeo na kutangaza uchaguzi kurudiwa  JUKATA wamesema kuwa wameshangazwa sana na hali hiyo ambapo wameipongeza sana mahakama ya nchini Malawi kwa kuonyesha ukakamavu wao katika kupingana na matakwa ya rais banda na kuamuru matokeo yahesabiwe tena ambapo amesema kuwa kama hilo lisingefanyika basin chi ya Malawi ingeingia katika machafuko makubwa sana.

Thursday, May 29, 2014

EXCLUSIVE--BAADA YA JANA KAMBI YA UPINZANI KUMTUHUMU ZITTO KABWE KWA UFISADI MKUBWA TANAPA NA NSSF,SASA ZITTO AMEJIBU,SOMA MANENO HAYA YA ZITTO HAPA

Maelezo yangu kuhusu kazi za Kigoma

AllStars/LEKADUTIGITE kwa NSSF na TANAPA. 

Leo tarehe 29 Mei, 2014 Msemaji wa Kambi ya Upinzani kuhusu Habari, Michezo, Vijana na Utamaduni amenituhumu kuhusika na kinachoitwa ufisadi katika Shirika la TANAPA na NSSF. 

Nasikitika kwamba katika hali niliyonayo ya kumwuguza mama yangu naingizwa kwenye siasa za majitaka. Kwa sasa nitatoa maelezo kwa ufupi ili kuondoa upotoshaji. 

Kampuni ya LekaDutigite inamilikiwa na wasanii 15 ambapo kila mmoja ana hisa 5% ambazo niliwalipia ili waweze kushirikiana katika kazi zao. Hisa 25% zilizobakia zinamilikiwa na kampuni ya Gombe Advisors ambayo ni kampuni isiyofanya faida (Company limited by guarantee) na haina maslahi yeyote ya kibiashara (not for profit company). Hivyo Mimi binafsi sina maslahi yeyote ya kifedha zaidi ya kuwasaidia wasanii hawa katika kazi zao mbalimbali. 

MAGAZETI YA LEO IJUMAA MAY 30,YAKO HAPA


HABARI ILIYOWAHUZUNISHA WATANZANIA WENGI LEO--MSANII RECHO AAGWA VIWANJA VYA LEADERS KATIKA PICHA

Wasanii wa Bongo muvi ambao walikuwa ni watu wa karibu wa Recho
Wasanii wa Bongo muvi ambao walikuwa ni watu wa karibu wa Recho.
Sehemu lilipowekwa jeneza la msanii Recho.
Sehemu lilipowekwa jeneza la msanii Recho.
Mwenyekiti wa Bongo muvi akitoa hotuba wakati wa kumuaga msanii Recho
Mwenyekiti wa Bongo muvi akitoa hotuba wakati wa kumuaga msanii Recho

habari kuu toka bungeni----HOTUBA YA MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI MHESHIMIWA JOSEPH O. MBILINYI (MB) KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA WIZARA YA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO KWA MWAKA WA FEDHA 2014/2015

1.0           UTANGULIZI
                 Mheshimiwa Spika, napenda kuchuku nafasi hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa afya njema na kwa kunitumia kama chombo cha mabadiliko hasa katika kutetea haki za wanahabari, vijana, wanamichezo na wasanii. Namshukuru Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Mhe. Freeman 

TP MAZEMBE YAWAACHIA SAMATTA NA ULIMWENGU KUJA STARS


SAMATA, ULIMWENGU KUIONGEZEA NGUVU STARS
Klabu ya TP Mazembe imewaruhusu wachezaji wake Mbwana

Samata na Thomas Ulimwengu kujiunga na timu ya Taifa (Taifa Stars) ambayo tayari imewasili Harare, Zimbabwe kwa ajili ya mechi ya michuano ya Afrika.


Taifa Stars itacheza na Zimbabwe (Mighty Warriors) katika mechi ya marudiano raundi ya mchujo kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Afrika zitakazofanyika mwakani nchini Morocco. Mechi hiyo itachezwa Jumapili (Juni 1 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa jijini Harare.

Samata na Ulimwengu watawasili Harare kesho (Mei 30 mwaka huu) saa 3.40 usiku kwa ndege ya Kenya Airways. Watajiunga na TP Mazembe mara baada ya mchezo huo ambapo Juni 2 mwaka huu watakwenda moja kwa moja Ndola, Zambia ambapo timu yao imepiga kambi kwa ajili ya mechi za Ligi ya Mabingwa Afrika.


BONIFACE WAMBURA
OFISA HABARI NA MAWASILIANO

SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

HOTUBA YA WAZIRI WA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO, MHE. DKT. FENELLA E. MUKANGARA (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA 2014/2015

   A.  UTANGULIZI

1. Mheshimiwa Spika, kufuatia taarifa iliyowasilishwa leo kwenye Bunge

lako Tukufu na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii sasa naomba kutoa hoja ya kwamba Bunge lako Tukufu lipokee, lijadili na kupitisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo na Asasi zake kwa mwaka wa fedha wa 2014/2015.

2. Mheshimiwa Spika, awali ya yote napenda kutumia fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunilinda na kunipa nguvu ya kutekeleza majukumu yangu na kuniwezesha kusimama mbele ya Bunge lako Tukufu kuwasilisha bajeti hii.

MBEYA CITY FC WATINGA ROBO FAINALI YA CECAFA NILE BASIN CUP MJINI KHARTOUM

 MBEYA City imetinga Robo Fainali za michuano ya CECAFA Nile Basin Cup inayoendelea nchini Sudan baada ya  sare ya bila kufungana na Enticelles ya Rwanda usiku wa jana katika Uwanja wa Khartoum.
Matokeo hayo yanaifanya Mbeya City imalize hatua ya makundi kwa kujikusanyia  pointi nne baada ya mechi tatu, lakini ipo katika nafasi ya pili nyuma ya miamba ya soka nchini Kenya, AFC Leopards walioongoza kundi kwa pointi 9.
Mchezo wa mwingine wa usiku, AFC Leopard walishinda bao 1-0 dhidi ya Academie Tchite ya Burundi na kushinda kwa asilimia 100 katika kundi lao.