Thursday, November 30, 2017

SARAKASI ZA UCHAGUZI MDOGO ZAWASHANGAZA LHRC,WAIBUKA NA HILI HAPA

Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimeibuka na kusema wamebaini uvunjifu mkubwa wa haki za Binadamu  katika uchaguzi huo ambapo Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimeshinda kata 42 huku Chadema ikiambulia ushindi wa kata moja.
Kaimu Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu Bi. Anna Henga akiongea na waandishi wahabari mapema leo kuhusu uchaguzi mdogo wa madiwani ulifanyika hivi karibuni.
Pia Kituo hicho kimeitahadharishwa serikali kuwa kama isipokemea vitendo hivyo vya uvunjifu wa Haki za Binadamu ,kutasababisha athari  mbaya kwenye uchaguzi wa serikali za Mitaa utakaofanyika 2019 pamoja na uchaguzi mkuu wa mwaka 2020.

Akizungumza na Waandishi Habari leo Jijini Dar es Salaam,Kaimu Mkurugenzi wa (LHRC),Anna Henga wakati wakitoa tathmini ya Uchaguzi huo, amesema kituo hicho kimefuatilia kwa ukaribu uchaguzi mdogo wa marudio wa kuchagua madiwani katika kata 43  zilizopo  halmashauri  takribani 36 kwenye mikao 19 nchini na kubaini uchaguzi ulikuwa na kasoro lukuki zilizochangia uvunjifu wa haki za binadamu.

Amesema  pamoja na ukweli kwamba baadhi ya kata uchaguzi ulifanyika kwa uhuru na haki lakini bado kituo hicho wamebaini pia uchaguzi huo kutawaliwa matukio ya watu kutekwa na watu wasiojulikana ,watu kupigwa ,kukamatwa na kujeruhiwa kwa lengo la kuharibu na kuvuruga  uchaguzi na kuwatia hofu wapiga kura.

"Vitendo hivi  vimefanywa  na Vyombo vya Dola,watu wasiojulikana na watu wanaosadikika kuwa wafuasi wa vyama siasa ikiwemo CCM na CHADEMA na vyama vingine vya Upinzani "Amesema Bi Henga.

 Bi Henga ameyataja matukio hayo ni tukio la kukamatwa na kutekwa kwa watu  katika kata ya Kitwiru  ,Iringa Mjini , kuliko fanywa na vijana wana ulinzi wa CCM maarufu kwa jina la Green Gurd.

"Yapo matukio ya ikiwemo kwenye Kata ya Makiba wakala wa Chadema ,Rashid Jumanne na Mwenyekiti wa Chadema  Tawi la Valeska,Nickson Mbise walijeruhiwa vibaya baada ya kushambuliwa  kwa mapanga  mapema asubuhi  walipokuwa wakielekea katika vituo vya kupiga kura"
Kaimu Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu Bi. Anna Henga akionyesha picha za baadhi ya matukio yaliyotokea wakati wa uchaguzi  mdogo wa Madiwani uliofanyika hivi karibuni baadhi ya maeneo hapa nchini.
"Lhrc tumebaini pia kuna matukio yameripotiwa kuhusu viongozi wa vyama vya viasa na Mawakala wa Vyama Kukamatwa mathalani katibu wa Chadema wilaya ya Ubungo ambaye alikuwa mratibu Mkuu wa Uchaguzi wa kata ya Saranga ,Perfeck Mwasiwelwa ambaye alikamatwa na Jeshi Polisi,"

Bi Henga ameendelea kuyataja matukio hayo ni tukio la kukamatwa kwa Meya wa Ubungo na Mwenyekiti  wa Chadema Wilaya ya Ubungo .Boniface Jacob ambaye alikamatwa siku ya uchaguzi ambaye alikuwa ndiye atakayeapishwa kuwa Wakala Mkuu kwenye majumuisho ya kura za Mwisho katika kata.

ARUSHA.
Bi Henga amesema kituo hicho kimebaini rafu katika kata 6 za Jimbo la Arumeru Mashariki ,kata ya Ngobobo,Makiba,Luguruki,Ambureni,Mroroni na Musa ambapo sehemu hizi mawakala wote wa Uchaguzi walitolewa nje ya Vituo vya Kupiga kura wakati zoezi la kupiga kura likiendelea.

Amesema kitendo cha Mawakala wa Vyama vya Siasa kutolewa nje  siku ya Uchaguzi mazingira haya ni viashiria  vya kufanya uchaguzi usio na huru na haki kwani wagombea walikosa haki yao kisheria ya kuwakilisha kuwakilishwa na Mawakala.

Pamoja na hayo,Bi Henga amesema  Kituo Cha Sheria  kinaona matendo hayo sio mazuri ,na yana viashiria vyote vya kukandamiza Demokrasia nchini .

"Kuna hatari ya kukuza utamaduni wa kulipana Visasi kwa Chuki za Kisiasa ambacho kitapelekea uvunjifu wa Amani "Amesema Bi Henga ambaye pia ni Wakili  Msomi.
Baadhi ya waandishi wa habari walioudhuria mkutano huo, wakifuatilia kwa umakini tamko linalotolewa na kituo cha Sheria na Haki za Binadamu mapema leo jijini Dar es salaam
Bi Henga ametoa wito kwa Serikali pamoja na vyombo vya Dola kufanya uchanguzi  wa kina na kuchukua hatua kali za kisheria kwa watakao bainika kuhusika kwa namna moja katika uvunifu wa haki za binadamu na uvurugaji wa Uchaguzi.

"Matukio haya yasipokemewa na Jamii nzima ni kiashiria kibaya na msingi mbaya utakao athiri chaguzi zijazo .Hii itapelekea kutishwa kwa wapiga kura wasijitokeze kutekeleza haki zao za kimsingi za kuchagua viongozi wao,kuchochea uhasama miongoni mwa wananchi na wadau wengine wa uchaguzi pamoja na kufifisha Imani ya wananchi juu vya Vyombo vya Usimamizi wa Uchaguzi na Dola kwa ujumla"Amesema Henga

NAGMA GIGA- AWATAKA WAZAZI KUPINGA UDHALILISHAJI WA KIJINSIA.

Na Is-haka Omar, Zanzibar.

NAIBU Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Nagma Giga amewataka wazazi na walezi kuunga mkono juhudi za serikali na wanaharakati katika kupinga vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia kwa wanawake na watoto nchini.
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi Zanzibar ,  Nagma Giga akifungua mkutano Mkuu wa Uchaguzi wa Jumuiya hiyo uliofanyika Amani Unguja.
Kauli hiyo ameitoa wakati akifungua mkutano Mkuu wa uchaguzi wa Wazazi katika Mkoa wa Mjini, uliofanyika Amaani Unguja.

Alisema wazazi ndio walezi na waangalizi wa malezi ya makundi yote katika jamii hivyo ni lazima wawe mstari wa mbele kupinga vitendo vyote vinavyoensda kinytume na maadili, mila desturi na utamaduni visiwani humo.

Alifafanua kwamba ushindi dhidi ya vitendo vya udhalilishaji itafanikiwa endapo jamii itakuwa tayari kushirikiana na Serikali na vyombo vingine vya kisheria ili kudhibiti uhalifu huo unaochafua heshima na sifa ya nchi kitaifa na kimataifa.

"Hii ni vita yetu sote kila mzazi amuone mtoto wa mwenziwe kama wake hapo ndipo tutakapoweza kuwalinda watoto wetu ili wakue katika malezi bora yasioyokukuwa na vikwazo vya kukatisha malengo yao ya baadae.
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Amani, Abdi Ali Mzee “Mrope” akiwasalimia wajumbe wa mkutano huo wa uchaguzi jumuiya ya wazazi Mkoa wa Mjini.
Wanawake na watoto wengi wamekuwa ni wahanga kubakwa,kulawitiwa na kutelekezwa hali inayosababisha wengi wao kuathirika kisaikolojia ” Alieleza  kwa uzuni Nagma.

Pia aliwasihi wazazi, viongozi wa dini na wanasiasa nchini kuhakikisha wanakemea kuporomoka kwa maadili kwa baadhi ya vijana wanaovaa nguo zinazokwenda kinyume na utamaduni sambamba na kutumia lugha zisizofaa katika jamii.

Akizungumzia Uchaguzi wa Mikoa mbali mbali ya jumuiya hiyo, Nagma aliwasisitiza wajumbe wa mikutano hiyo kuwachagua viongozi imara na wenye dhamira ya kweli katika kuleta mabadiliko ya kimaendeleo ndani ya jumuiya na Chama Cha Mapinduzi kwa ujumla.

Aliwasisitiza wasimamizi wa uchaguzi huo kutenda haki na wapiga kura kuwa na uadilifu wakati wa kutekeleza wajibu wao wa kidemokrasia kwa kuchagua viongozi wanaowataka bila ya kufanya vurugu.
PICHA IMG-0254-Katibu wa CCM Mkoa wa Mjini Mohamed Omar Nyawenga(kushoto) Naibu katibu Mkuu wa Jumuiya ya wazazi Zanzibar Nagma Giga (katikati) na viongozi wengine wa jumuiya ya wazazi.
Naibu Katibu Mkuu huyo, alisema Jumuiya hiyo ina majukumu mawili makubwa ya kuhakikisha CCM inashinda na kubakia madarakani kupitia uchaguzi mkuu wa Dola sambamba na kusimamia mwenendo wa elimu, malezi, utamaduni na mazingira kwa jamii.

Alisema nchi zilizoendelea Ulimwenguni ni zile zilizowekeza katika sekta ya elimu inayozalisha wataalamu wa fani mbali mbali za kuleta maendeleo ya haraka katika kukuza uchumi wa nchi kupitia mfumo wa uzazilishaji mali katika sekta za viwanda vinavyotegemea mfumo wa sayansi na teknolojia.

“Kila wana CCM anatakiwa kuchukua jukumu la kuwaelimisha vijana wetu wasome kwa bidii ili Chama na jumuiya zetu ziwe na wanachama wengi wenye uwezo mzuri wa kitaaluma watakaoweza kusimamia maslahi ya taasisi zetu bila kuyumba.

Mikakati hiyo itafanikiwa kama tutapata viongozi makini kupitia uchaguzi huu ambao ni wapambanaji wasiochoka wala kukata tama katika uwanja wa kisiasa.” Alifafanua Naibu Katibu Mkuu Giga.
BAADHI ya wajumbe wa Mkutano huo wakisikiliza kwa makini hotuba ya ufungunguzi ya mgeni rasmi.
Naye Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Amani ambaye ni mjumbe wa Mkutano huo, Abdi Ali Mzee ‘’Mrope’’ alisema wakati umefika wa Chama cha Mapinduzi na jumuiya zake kuwa na ajenda moja ya kutumia vizuri rasilimali zinazomilikiwa na Chama kuanzisha miradi mikubwa itakayozalisha kipato na kutoa ajira za kudumu kwa vijana.
Kwa upande wake mjumbe wa Mkutano huo, Salma Abdi Ibada aliwashauri viongozi watakaochaguliwa kupitia uchaguzi huo wawe mfano wa kuigwa katika  kuleta maendeleo ndani ya jumiya na kupiga vita vitendo vya rushwa na makundi ya kuhatarisha uhai wa Chama.

Uchaguzi huo umefanyika katika mikoa yote jumuiya ya Wazazi nafasi ambazo zinagombewa ni Wenyeviti wa Mikoa,  nafasi ya Mkutano mkuu taifa /Baraza la wazazi taifa, nafasi mkutano mkuu wa CCM mkoa, pamoja na nafasi za Baraza kuu la wazazi Mikoa kutoka kila Wilaya.


Asya Idarous Khamsin kuonesha mitindo yake Desemba 9, Oakland California Marekani

Mkongwe katika mitindo nchini Tanzania na Marekani Mama wa mitindo Bi. Asya Idarous Khamsin anatarajiwa kuonyesha mitindo yake mbalimbali ya ubunifu wa mavazi katika sherehe ya maalum  ya Watanzania itakayofanyika tarehe 9 Desemba,2017 huko Oakland California Nchini Marekani.
Kwa mujibu wa Mama wa Mitindo, Bi. Asya Idarous Khamsin ameweka wazi kuwa, onyesho hilo litakuwa la aina yake kwani watu watakaojitokeza watashuhudia mitindo mipya kabisa ya mavazi ambauyo itaonyesha kwenye jukwaa maalum siku hiyo sambamba na Chakula maalum cha kuchangia watu wenye tatizo la ugonjwa wa Kansa nchini Tanzania.

“9 Desemba,2017  tumewaandalia onyesho maalum la mavazi. Watu wajitokeze kwa wingi kushuhudia mavazi ya ubunifu. Pia kutakuwa na ‘fundraising dinner’  ya kukusanya fedha kwa ajili ya (partnering to tackle cancer to Tanzania) ambayo inafanyika kila mwaka.

Sherehe hizo ni pamoja na kusherehekea Shamla shamla za Uhuru wa (Tanganyika) ambayo sasa ni Tanzania” Alieleza Asya Idarous Khamsin.


MHE MWANJELWA AMUAGIZA MKURUGENZI KUMSIMAMISHA KAZI MSIMAMIZI WA ZAO LA PARETO KUPISHA UCHUNGUZI

Naibu Waziri Wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa  akizungumza wakati wa Mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Jojo Kata ya Santilya akiwa kwenye ziara ya kikazi Katika Mikoa ya Nyanda za Juu kusini Kwa Tanzania, Jana Novemba 29, 2017. Picha zote Na Mathias Canal
 Naibu Waziri Wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa  akisisitiza jambo wakati wa Mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Jojo Kata ya Santilya akiwa kwenye ziara ya kikazi Katika Mikoa ya Nyanda za Juu kusini Kwa Tanzania, Jana Novemba 29, 2017.
 Naibu Waziri Wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa  akizungumza wakati wa Mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Jojo Kata ya Santilya akiwa kwenye ziara ya kikazi Katika Mikoa ya Nyanda za Juu kusini Kwa Tanzania, Jana Novemba 29, 2017.
 Baadhi ya wakazi wa Kijiji cha Jojo Kata ya Santilya wakimsikilkiza Naibu Waziri Wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akitoa maelekezo ya serikali kuhusu zao la Pareo akiwa kwenye ziara ya kikazi Katika Mikoa ya Nyanda za Juu kusini Kwa Tanzania, Jana Novemba 29, 2017.
 Mbunge wa Jimbo la Mbeya Vijijini Mhe Oran Njeza akizungumza katika mkutano huo kufikisha kilio cha wananchi mbele ya Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Mary Mwanjelwwa kuhusu zao la Pareto na matatizo la wafanyabiashara kujaza Lumbesa kwenye uuzaji wa mazao mbalimbali likiwemo zao la viazi wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika Kijijini Jojo Kata ya Santilya, Jana Novemba 29, 2017.
Baadhi ya wakazi wa Kijiji cha Jojo Kata ya Santilya wakimsikilkiza Naibu Waziri Wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akitoa maelekezo ya serikali kuhusu zao la Pareo akiwa kwenye ziara ya kikazi Katika Mikoa ya Nyanda za Juu kusini Kwa Tanzania, Jana Novemba 29, 2017.

Na Mathias Canal, Mbeya

Naibu Waziri Wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa Jana Novemba 29, 2017 amemuagiza Mkurugenzi Wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya kumsimamisha kazi Afisa Kilimo Wilaya ya Mbeya anayesimamia zao la Pareto Ndg Emmanuel Halinga ili kupisha uchunguzi.

Mhe Naibu Waziri ametoa agizo hilo wakati wa Mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Jojo Kata ya Santilya akiwa kwenye ziara ya kikazi Katika Mikoa ya Nyanda za Juu kusini mwa Tanzania mara baada ya Mhe Mbunge wa Jimbo hilo Mhe Oran Njeza na Wananchi wote waliokuwepo kwenye mkutano huo wa hadhara kumrushia shutuma nzito na kumkataa mtaalamu huyo wa kilimo mbele ya Naibu Waziri.

Alisema kuwa pamoja na zao hilo la Pareto kuwa la kwanza kwa uzalishaji katika nchi za Afrika huku likiwa zao la pili kwa uzalishaji Duniani lakini bado halijamkomboa Mkulima nchini jambo ambalo linaonyesha namna ambavyo baadhi ya wataalamu Wa Kilimo wameshindwa kutekeleza majukumu yao ipasavyo.

Alisema kuwa wataalamu wa kilimo walipaswa kusimamia kwa kiasi kikubwa zao hilo kwani Pato lake ni wastani wa tani 2000 kwa mwaka sawa na Bilioni 12 mpaka 14 ambapo katika kipindi hili bei ya kuanzia Mkulima analipwa shilingi 2300 kwa kilo lakini inapanda mpaka shilingi 3300 kulingana na ubora wa zao hilo ambalo mkulima amelima.

Alisema kuwa serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na Mhe Rais Wa Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli inaamini katika kazi ambazo matokeo yake yanapaswa kuonekana hivyo Mkulima kushindwa kunufaika na mazao ya Kilimo ni uzembe wa baadhi ya wataalamu Wa Kilimo unaosababishwa na kufanya kazi kwa mazoea.

Aidha, Mhe Mwanjelwa ametoa siku saba kwa Kaimu Mkurugenzi wa Bodi ya Pareto nchini Ndg Lucas Ayo kutoa sababu za kwanini mnunuzi ni mmoja wa zao hilo jambo ambalo linaonyesha kuwa na harufu ya rushwa au kupelekea kudumaza solo la zao hilo kwa kuwa na mnunuzi mmoja asiyekuwa na ushindani.

Ili kuongeza ufanisi wa zao hilo Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa ameelekeza wakulima Kuanzisha vikundi vya vyama vya ushirika vya msingi ambavyo vitakuwa na usajili serikalini kwani vitasaidia kuwa na mjadala wa jinsi ya kuwa na ubora wa zao la pareto jambo litakalopekea kuanzisha viwanda vidogo ambavyo ni ishara ya kuunga mkono juhudi za Rais Magufuli kuwa na Tanzania ya Viwanda.

"Mkishaanzisha tu vikundi vya vyama vya ushirika mtoe taarifa mapema iwezekanavyo na serikali kupitia mrajisi itatoa Elimu ya ushirika" Alikaririwa Mhe Mwanjelwa

Ameagiza zao la Pareto kuwa huru ili mkulima awe huru kuuza kwa mnunuzi anayemtaka kwani kwa sasa kuna mnunuzi mmoja tu ambaye anajipangia mwenyewe namna ya kununua zao hilo kwa gharama atakazo pasina kupingwa.

Pia alielekeza wakulima Kuingia kwenye Kilimo cha mkataba kati yao na Chama cha msingi (AMCOS) jambo litakalorahisisha kupata mikopo ya Kilimo kupitia Benki ya Kilimo nchini (TADB).

Kuhusu Lumbesa, aliwataka wafanyabiashara wa wanaojaza Lumbesa badala ya kujazwa kilo 100 kwa gunia lakini linajazwa mpaka kilo 120 kuacha haraka tabia hiyo kwani wanakwenda kinyume na sheria hivyo kwa yeyote atakayebainika atachukuliwa hatua Kali za kisheria.


TANESCO: HITILAFU KWENYE GRIDI YA TAIFA

MAJIRA ya saa 7:20 leo hii Alhamisi Novemba 30, imetokea hitilafu kwenye Gridi ya Taifa na hivyo kusababisha umeme kukatika takriban kwenye mikoa yote iliyounganishwa kwenye Gridi hiyo.


Kwa mujibu wa Kaimu Meneja Uhusiano wa TANESCO, Bi. Leila Muhaji, mafundi na wataalamu wa Shirika la Umeme Tanzania TANESCO wameanza kufuatilia kujua chanzo chake hasa ni nini na taarifa Zaidi zitatolewa kila baada ya muda ili kuufahamisha umma na watuamiaji wa umeme.

Wednesday, November 29, 2017

MAMBO 10 UNAYOTAKIWA KUYAFAHAMU KUHUSU UKIMWI

Na Jumia Travel Tanzania

Wakati dunia ikielekea kuadhimisha siku ya UKIMWI kila ifikapo Desemba mosi ya kila mwaka, bado Virusi Vya UKIMWI (VVU) na ugonjwa huo unabaki kuwa ni changamoto muhimu ya kiafya ndani ya jamii hususani kwenye nchi zenye kipato cha chini na kati.

Kutokana na maendeleo yaliyofikiwa sasa katika upatikanaji wa tiba ya mchanganyiko wa dawa zinazotumika kuzuia VVU kuongezeka mwilini (antiretroviral therapy - ART), watu waliogundulika kuwa na VVU wanaishi kwa muda mrefu na maisha yenye afya. Kwa kuongezea, imethibitishwa kwamba dawa hizo zinazuia kuendelea kuongezeka kwa VVU.

Katika kukupatia elimu zaidi juu ya ugonjwa huu, Jumia Travel ingependa kukufahamisha juu ya mambo yafuatayo ambayo yamebainishwa na Shirika la Afya Duniani (WHO), ambalo huunga mkono nchi mbalimbali katika kuunda na kutekeleza sera na programu ili kuboresha na kuongeza jitihada za kuzuia VVU, matibabu, huduma na kutoa msaada kwa watu wote wanaohitaji msaada.

Taafirifa hizi zinatoa takwimu zilizopo sasa kuhusu ugonjwa huu pamoja na njia za kuuzia na kuutibu:

VVU huambukiza seli za kwenye mfumo wa kinga za mwili. Maambukizi husababisha kuendelea kuzorota kwa mfumo wa kinga ya mwili, huvunja uwezo wa mwili kuweza kuepuka baadhi ya maambukizi na magonjwa. UKIMWI hujulikana kuwa ni hatua ya juu kabisa ya VVU ambapo hujipambanua kwa kujitokeza kwa maambukizi kati ya zaidi ya 20 au saratani zinahusiana na virusi hivyo.   

VVU vinaweza kuambukizwa kwa njia kadhaa. VVU vinaweza kuambukizwa kupitia: kujihusisha na ngono isiyo salama; kuhamishiwa damu au bidhaa inayohusiana na damu au kufanyiwa upandikizaji ambao sio salama; kushirikiana kutumia vifaa vya kutobolea mwili (sindano) na vimiminika au vya kuchorea michoro mwilini (tattoo); kutumia vifaa vya upasuaji na vinginevyo vyenye ncha kali; na maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto mchanga wakati wa ujauzito, kujifungua na kunyonyesha.   
Zipo njia kadhaa za kuzuia maambukizi ya VVU. Njia muhimu za kuzuia maambukizi ya VVU ni: kufanya ngono salama kama vile kutumia kondomu; kupima na kupatiwa matibabu kwa magonjwa yaliyoambukizwa kupitia ngono, ikiwemo VVU ili kuzuia maambukizi kuendelea; hakikisha kwamba damu au bidhaa yoyote inayohusiana na damu unayotaka kuitumia imepimwa VVU; chagua njia salama ya kimatibabu wakati wa tohara endapo unatoka katika nchi ambazo huchangia vifaa; kama una VVU anza mara moja kutumia dawa za kusaidia kupunguza virusi kuongezeka mwilini kwa manufaa yako na pia kuzuia kuambukiza VVU kwa mwenza au mtoto wako (kama ni mjamzito au unanyonyesha).  
Watu milioni 36.7 duniani wanaishi na VVU. Duniani kote, inakadiriwa kuwa watu milioni 36.7 (milioni 34.0 - 39.8) walikuwa wanaishi na VVU mwaka 2015, na kati ya hawa milioni 1.8 (milioni 1.5 - 2.0) walikuwa ni watoto. Idadi kubwa ya watu wanaoishi na VVU wanapatikana kwenye nchi zenye kipato cha chini na kati. Inakadiriwa watu milioni 2.1 (milioni 1.8 - 2.4) walipata maambukizi mapya ya VVU mwaka 2015. Inakadiriwa watu milioni 35 mpaka sasa wamefariki kutokana na VVU, wakiwemo milioni 1.1 (940,000 mpaka milioni 1.3) mwaka 2015.    
Mchanganyiko wa dawa za ART huzuia virusi hivyo kuongezeka mwilini. Endapo kuzaliana kwa VVU kukikoma, basi seli za kinga za mwili zitaweza kuishi kwa muda mrefu na kuupatia mwili kinga dhidi ya maambukizi. Ufanisi wa dawa za ART hupelekea kupungua kwa virusi, kiasi cha virusi mwilini, kwa kiasi kikubwa hupunguza kuambukiza virusi kwa watu walio kwenye mahusiano ya kimapenzi. Endapo mmojawapo wa wapenzi kwenye mahusiano anatumia dawa za ART ipasavyo, kuna uwezekano wa maambukizi ya njia ya ngono kwa mwenza ambaye hana VVU kupungua kwa kiasi cha takribani 96%. Kupanua wigo wa matibabu ya VVU kunachangia katika jitihada za kuzuia VVU.   
Katikati ya mwaka 2016, watu milioni 18.2 duniani walipokea dawa za kusaidia kuzuia VVU kuongezeka mwilini. Kati ya hawa zaidi ya milioni 16 wanaishi kwenye nchi zenye kipato cha chini na kati. Mwaka 2016, WHO ilitoa toleo la pili la “Miongozo juu ya matumizi ya dawa za kusaidia kuzuia kuongezeka VVU mwilini ili kutibu na kuzuia maambukizi ya VVU.” miongozo hii imetoa mapendekezo kadhaa, ikiwemo pendekezo la kutoa dawa za kusaidia kuzuia VVU kuongezeka mwilini kwa watoto kwa kipindi chote cha maisha yao, vijana na watu wazima, wakiwemo wanawake wajawazito na wanaonyonyesha waishio na VVU, licha ya idadi ya CD4 walizonazo mara baada tu baada ya kugundulika.          

Kupima VVU kunasaidia kuhakikisha matibabu kwa watu wenye uhitaji. Upatikanaji wa huduma ya kupima VVU na madawa unatakiwa kuongezeka kwa kasi ili kufikia lengo la kutokuwa na ugonjwa wa UKIMWI kufikia mwaka 2030. Upimaji wa VVU bado ni mdogo, ambapo inakadiriwa kwamba 40% ya watu wenye VVU au zaidi ya watu milioni 14 bado hawajatambulika na hawafahamu hali ya maambukizi yao. WHO inapendekeza ubunifu kwenye mbinu za kujipima wenyewe VVU na wenza wao ili kuongeza huduma za kupima VVU kwa watu ambao hawajagundulika.    
Inakadiriwa watoto milioni 1.8 duniani wanaishi na VVU. Kwa mujibu wa takwimu za mwaka 2015, wengi wa watoto hawa wanaishi katika nchi zilizopo kusini mwa jangwa la Sahara na waliambukizwa kutoka kwa mama zao wenye VVU wakati wa ujauzito, wakati wa kuzaliwa au kunyonyeshwa. Karibu watoto 150,000 (110,000 - 190,000) walipata maambukizi mapya ya VVU mwaka 2015.
Kuondoa maambukizi ya VVU kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto inawezekana. Ufikiwaji wa hatua za kuzuia maambukizi ya VVU umekuwa ni mdogo kwenye nchi zenye kipato cha chini na kati. Lakini jitihada zimeendelea kufanyika kwenye baadhi ya maeneo tofauti kama vile kuzuia maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto pamoja na kuokoa maisha ya akina mama. Mwaka 2015, karibu wajawazito 8 kati ya 10 wanaoishi na VVU au sawa na wanawake milioni 1.1 walipokea dawa za kuzuia VVU kuongezeka mwilini. Mwaka 2015, Cuba ilikuwa ni nchi ya kwanza kutangazwa na WHO kufanikiwa kuzuia maambukizi ya VVU na Kaswende kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto. Mwaka 2016, nchi zingine tatu: Armenia, Belarus na Thailand nazo zilithibitishwa kulifanikisha hilo.        
VVU ni sababu kubwa inayopelekea kupata ugonjwa wa Kifua Kikuu (TB). Katika mwaka 2015, inakadiriwa kuwa watu milioni 1.2 (11%) kati ya watu milioni 10.4 duniani waliopata TB walikuwa ni waathirika wa VVU pia. Mwaka huohuo takribani vifo 390,000 vilivyotokana na TB vilitokea miongoni mwa watu waliokuwa wanaishi na VVU. Nchi za Kiafrika ambazo zilizo chini ya WHO zilizidi karibu 75% ya idadi ya vifo vilivyokuwa vinahusiana kati ya TB na VVU.
UKIMWI ni janga ambalo linaikumba dunia nzima Tanzania ikiwemo, licha ya ugonjwa huu kutzungumziwa kwenye kampeni tunazozisikia lakini ukweli ni kwamba bado upo, ni tatizo, unaathiri na kuua nguvu kubwa ya taifa. Katika kuelekea kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya UKIMWI duniani, Jumia Travel ingependa kuikumbusha jamii inapaswa kutambua kwamba jukumu la kuupiga vita ugonjwa huo bila ya kutegemea taasisi binafsi au mashirika ya nje.   

Heineken's First Africa Inspired Fashion Collection Co- created with Talented Designers a great Success



Many fashion industry experts have often labelled Africa as an epicentre for buzzing creative energy. True to the word we have seen vibrant colourful designs being exhibited across the globe with origins stemming from Africa.

In its latest bid to absorb and adopt such creativity and inspiration, global beer brand, Heineken® sought far and wide across East Africa for emerging creatives through a week long engaging boot camp that featured ten fashion finalists in which two were crowned overall winners. 

The winners Lulu Mutuli and Azra Walji and quite obviously Africa’s hottest emerging design talents were given the ultimate opportunity to design Heineken’s first-ever African fashion collection, unveiled on the catwalk at Lagos Fashion and Design Week.

According to the man behind all design and concept development for Heineken worldwide, Mark van Iterson – Heineken Global Design Director, Heineken® Africa Inspired Fashion (HAIF) initiative is the next chapter in Heineken’s ‘Open Design Explorations’, a global co- creation programme that connects emerging creatives and gives them a platform to showcase their talent.

“Our brand is not just about the beer alone, as we are also invested in the full consumer experience. With the support of the Lagos Fashion and Design Week, we have a platform to present this unique collection to the world,” he said.

The Collection itself is a fusion of the two designers’ concepts and is the first of many design apprenticeships that the brand will roll out across the world, going next to Asia.

It is also about creativity - which is what pushes the Heineken brand forward and keeps it alive.
There’s a lot creative energy buzzing in Africa. As a global brand, we are always willing to absorb and adopt such creativity and inspiration.
For instance, the winners, Mutulo and Walji will go on to benefit from a year-long programme of coaching from the designers, known for eye-catching print design and innovative corporate fashion. The designs will be produced at scale across Africa to be worn by Heineken ambassadors throughout Tanzania, East Africa and beyond.
Lulu Mutuli, 24, whose work gives traditional African apparel a futuristic edge, has worked in top fashion houses in New York including RHIE and OMONDI. She said, “My designs took inspiration from the role African fashion has played in the culture of my country. Combining this rich heritage with the progressive character of the Heineken brand was a challenge I couldn’t resist. I used the bold Heineken colour palette, but I added a grey tone and used technical orientated patterns for a modern twist. The asymmetric shapes you can see were a way of incorporating practical elements whilst creating striking and stylish silhouettes.”

Azra Walji, 27, is known for her feminine shapes and African inspired elegance, reflected in her winning designs with Heineken. She said, “I am so grateful to Heineken. Sharing my work at Lagos Fashion at Design Week is a career-defining opportunity. I really enjoyed playing with the bold red and green colours – they are so iconic to the brand but also synonymous with the vibrancy of Africa. My designs are inspired by traditional African apparel but with a twist – I love the modern femininity of the trousers and short dresses.”

Nurturing Budding  Talent is  Key
Njeri MBURU, Heineken East Africa Marketing Manager said, “Identifying and empowering talent remains a critical part of our global agenda. We are constantly seeking new co- creation opportunities, to connect with young emerging designers and give them a global stage to showcase their talent, so we are delighted that this initiative has put a spotlight on such talent.
Lagos Fashion and Design Week is growing hub for creativity and is helping to influence and define the global fashion landscape. We look forward to extending the programme to other key markets next year.
Overall the African Inspired Fashion Competition had 10 finalists from East Africa including budding talent from Tanzania Bijoux Trendy and Anissa Mpungwe.” she added.

Lagos Fashion and Design Week 2017 is a multiday fashion extravaganza at the Eko Atlantic, Victoria Island, Lagos, Nigeria, where global designers including Maki Oh (whose fans include Michelle Obama and Beyoncé) take centre stage to celebrate African fashion and culture.

The judges for Heineken’s Africa Inspired Fashion challenge in Nairobi which brought Mutuli and Walji to Lagos, included fashion powerhouse and founder of the Lagos Fashion and Design Week Omoyemi Akerele, top Nigerian fashion designer Gloria Wavunno and Tanzanian stylist Rio Paul.




SERIKALI YA AWAMU YA TANO YA RAIS DKT. JOHN POMBE MAGUFULI YAFANIKIWA KATIKA UKUSANYAJI MAPATO KIELEKTRONIKI

Tangu kuzinduliwa Dirisha la Ukusanyaji Kodi kidigitali June mosi 2017 (Electronic Revenue Collection System - eRCS) ambalo lilizinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano  wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiongozana na Makamu wa Rais Mhe. Mama Samia Suluhu Hassani pamoja na Rais wa Zanzibar Mhe. Dkt. Mohamad Shein,  mawaziri kadhaa wa serikali za Muungano na serikali ya Mapinduzi; Kwa mara ya kwanza serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imejipatia bila bugudha Ushuru mkubwa wa bidhaa na kodi ya Ongezeko la Thamani zitokanazo na makampuni ya simu.
Mfumo huu uliosukwa na vijana wa Kitanzania wazalendo, umefanikisha kuongeza mapato litokanalo na mtandao (Ciber Space) kwa Zanzibar kwa 51% kwa robo ya tatu ya mwaka 2017 ukilinganisha na miezi kama hiyo 2016. Uchunguzi uliofanyika katika robo hiyo (tatu) ya mwaka 2017 (Julai,August na Septemba 2017), umebaini Zanzibar imelipwa kupitia mfumo wa eRCS Tsh Bil 7.2 ambayo imeongezeka kwa 51% ukilinganisha na miezi kama hiyo mwaka 2016 ambapo makusanyo ya jumla ya kodi yalikuwa  Tsh Bil 3.5 pekee.
Kwa mujibu wa vielelezo vya makusanyo wa TRA, miezi mitatu kabla ya mfumo huu kuzinduliwa rasmi (April,May na June); Makampuni ya simu yalilipa jumla ya kodi ya  Tsh Bil 101.7 lakini baada ya kuzinduliwa rasimi kwa mfumo huu wa eRCS na makampuni ya simu (TTCL, HALOTEL, AIRTEL, VODACOM, ZANTEL, SMART na TIGO) kuugwa ndani ya mfumo; Kwa kipindi cha miezi mitatu pekee ( Julai,Agost na Septemba 2017), yameweza kulipa kwa njia ya kielektroniki Tsh Bil 128.9 kukiwa na ongezeko la Sh Bil 27.2 sawa na 21% huku ongezeko la kodi ya thamani ikipanda kwa 9% yaani Tsh. Bil 4.7 sambamba na ongezeko la Ushuru wa Bidhaa 29% yaani Tsh. Bil 22.
Taarifa za kiuchunguzi zimebaini serikali inafuatilia kwa kina udanganyifu wowote utakao ama uliojitokeza kabla na baada ya mfumo hasa taarifa za makampuni ya simu katika matumizi yaoya kila mwezi.
Mpaka sasa, benk kadhaa nchini zimekamilisha taratibu za kuungwa katika mfumo huu na kuanza kulipa kodi kielectroniki.  Huu ni ushindi mkubwa kwa mkakati wa Rais Magufuli katika kupata njia bora za kukusanya mapato nchini. 
Ikumbukwe wajenzi wa mfumo huu ni vijana wazalendo walioaminiwa na serikali ili kuokoa kiasi kikubwa cha fedha ambazo zingetumika katika ujenzi wa mfumo huo kutumia wataalamu na makampuni ya kigeni.
Hivi ndivyo mapato yanavyoonekana katika Dashibodi ambazo viongozi wakuu wa nchi wanaona mapato yanavyokusanywa kielectroniki kwa kutumia mfumo  wa eRCS kila sekunde.
Jedwali hili linaonyesha  Mabenk yaanza kulipa baada ya yale yaliyokamisha kujiunga na ERCS ambyo ni BANK M na AMANA BANK Tanzania ina Mabenk zaidi  ya 20