Wednesday, December 31, 2014

MWAKYEMBE AMWAGA CHOZI TRL LEO,AFUKUZA MABOSI KIBAO,SOMA HAPA


Pichani ni WAZIRI wa Uchukuzi, Dk Harisson Mwakyembe
akizungumza na mamia ya wafanyakazi wa Shirikala la reli
(TRL) leo jijini Dar es Salaam


NA KAROLI VINSENT

HUKU ikiwa imebaki Miezi kumi ili Rais Jakaya Kikwete amalize mada wake,Sasa WAZIRI wa Uchukuzi, Dk Harisson Mwakyembe ametema Cheche Baada ya leo  Kuibuka na kuwasimamisha pamoja na kuwafukuza kazi watumishi 12 wa Kampuni la Reli Tanzania (TRL), kwa tuhuma za kuhujumu shirika hilo huku akiagiza wachukuliwe hatua za kisheria  pamoja na kufulisiwa.
            
Hatua hiyo ni mwendelezo wa Waziri Mwakyembe kusafisha wafanyakazi wanaojihusisha na vitendo vya ubadhilifu, vinavyokwenda kinyume na jitihada za serikali kutaka TRL kujiendesha kwa faida na kuondokana na utegemezi ambao shirika hilo limekuwa mzigo kwa sasa kwa serikali kutokana na ufisadi huo.
  
  Akizungumza na waandishi pamoja na wafanyakazi wa TRL,leo Jijini  Dar es Salaam ,ambapo Waziri Mwakyembe aliwataja wafanyakazi waliofukuzwa kazi ni Stanley Makunja, Stanley Edward, Jason Moses, B. Luoga, Edward Benedict, na Lucy Ntinya ambapo wanadaiwa kugushi malipo ya tiketi za abiria na kuitia hasara TRL.



Wafanyakazi wa Shirika la Reli nchini pamoja na Waaandishi wa Habari wakimsikiliza kwa makini Waziri Mwakyembe

TIZAMA HISTORIA YA ZITTO NA LIPUMBA WALIYOWEKA MTWARA LEO


PROFESA LIPUMBA na ZITTO KABWE WAANDIKA REKODI KTK MKUTANO MKUBWA WA CUF VIWANJA VYA MTWARA MJINI,,,Magwiji ya siasa nchini Prof. Lipumba na Zitto Kabwe na wabunge watano wa CUF wameutikisa mji wa Mtwara kwa umati mkubwa wa watu.
Mkutano huo ambao umetajwa kuweka historia katika mji wa mtwara umeshughudia manguli hao wakizungumzia na kuchambua mambo mbali mbali yanayolikabili taifa kwa sasa hususani sakata la ESCROW. 
HAPA TUNAKUPA BAADHI YA PICHA ZA MKUTANO HUO,NYINGINE ZITAKUJIA BAADAE

HUYU NDIYE KOCHA MPYA WA SIMBA,ASAIN MWAKA MMOJA

GORAN AMWAGA WINO KWA MWAKA MMOJA KUINOA SIMBA

KOCHA mpya wa Simba raia wa Serbua Goran Kopunovic amemwaga wino wa mwaka
mmoja kuinoa timu hiyo ya Msimbazi.


Mmoja wa viongozi wa Simba aliiambia blog ya jamii kuwa kocha huyo aliyewasili leo
asubuhi na kufikia kwenye hotel ya Double Tree Masaki ataondoka kesho kwenda
Zanzibar kujiunga na timu hiyo ya wekundu wa Msimbazi inayoshiriki michuano ya Kombe
la Mapinduzi.


Naye Kopunovic akizungumza muda mfupi baada ya kukanyaga hardhi ya Tanzania 
alisema "Nimekuja kufanya kazi, naamini nitapata ushirikiano kutoka kwa viongozi wa 
Simba, wachezaji na mashabiki, Simba ni timu kubwa, naamini nitawapa 
mafanikio."alisema

Kocha huyo, amechukua mikoba ya Patrick Phiri aliyefungashiwa virago baada ya uongozi 
wa Simba chini ya mwenyekiti wake Evans Aveva kufanya tathmini ya mwenendo wa timu 
ambapo ametoka sare mechi sita, ameshinda mechi moja na kupoteza moja hivyo kuona 
hastaili kuendelea kuinoa timu hiyo ya mtaa wa Msimbazi huku akidaiwa kukaidi agizo la 
viongozi la kutowachezesha Waganda katika mechi dhidi ya Kagera walionyukwa bao 1-0

JESHI LA POLISI LIMEJIPANGA KIKAMILIFU KUHUSU MKESHA WA MWAKA MPYA WA 2015

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limepanga mikakati madhubuti ya kuhakikisha kwamba mkesha kuelekea Mwaka Mpya 2015 unakuwa salama, sherehe za mwaka mpya, kuandamana, baadhi ya watu wachache hasa vijana hupenda kuchoma matairi barabarani, kulipua fataki na vurugu za kila aina kwa lengo la kuonyesha furaha yao ya kuingia mwaka 2015.

Hali kama hiyo haitavumiliwa na Jeshi la Polisi kwa sababu badala ya sherehe hugeuka vitisho, vurugu, na kisha kuwatia hofu wananchi wasiokuwa na hatia. Katika harakati hizo Jeshi limeweka mpango kazi utakaowashirikisha askari wa vikosi vyote pamoja na wadau mbalimbali watakaojihusisha na ulinzi siku hiyo. Watakaojihusisha na ulinzi ni pamoja na kikosi cha Zimamoto, kampuni binafsi za Ulinzi, na katika Jeshi la Polisi kutakuwa na kikosi cha FFU na kikosi cha Mbwa na Farasi.

TIZAMA MATUKIO MAKUBWA YALIYOTIKISA NCHI MWAKA 2014


 Kundi lililoitwa Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA),wakiongozwa na Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba.
KUZALIWA KWA UKAWA Baada ya Rais Jakaya Kikwete kuridhia zoezi la uandikwaji wa Katiba Mpya, Tume ya kukusanya maoni chini ya uenyekiti wa Jaji Joseph Warioba ilifanya kazi yake vizuri na mwaka huu katiba hiyo ilipelekwa Bungeni ambako Bunge Maalum la Katiba lilikutana ili kupitia vifungu vyake kabla ya kuipeleka kwa wananchi kwa ajili ya kuipigia kura ya kuikubali au kuikataa.
Kulitokea malumbano makali kati ya wajumbe wa Bunge hilo juu ya vipengele kadhaa, hasa muundo wa serikali ya Jamhuri ya Muungano. Wajumbe waliotokana na Chama Cha Mapinduzi, walipendezwa na muundo wa serikali mbili kama ilivyo hivi sasa, wakati wapinzani walitaka serikali tatu.
Misimamo hiyo ilileta utengano mkali kiasi kwamba wajumbe wa upinzani wakiongozwa na Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba kuamua kususia vikao hivyo, wakipinga kile walichokiita uchakachuaji wa rasimu ya katiba ya Jaji Warioba. Ususiaji huo ulisababisha kuanzishwa kwa kundi lililoitwa Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA).
Jaji Warioba
Kuanzishwa kwa umoja huo uliovihusisha vyama vya Chadema, CUF, NCCR-Mageuzi na NLD, kulisababisha kundi hilo kukubaliana kusimamisha mgombea mmoja katika chaguzi zijazo, wakianzia na uchaguzi wa serikali za mitaa uliofanyika katikati ya mwezi huu.
JAJI WARIOBA APIGWA Baada ya wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba kumaliza kazi yake na kuikabidhi katiba pendekezwa kwa Rais Jakaya Kikwete tayari kwa ajili ya kuipeleka kwa wananchi ili kupigiwa kura ya maoni, kulikuwa na mkanganyiko miongoni mwa watu juu ya kilichomo ndani ya katiba hiyo, baadhi wakipinga kuondolewa kwa vifungu vingi vilivyokuwa na masilahi kwa nchi.
Miongoni mwa wanaoongoza harakati za kupinga kuondolewa kwa baadhi ya vifungu vilivyowasilishwa na Tume hiyo, ni Taasisi ya Mwalimu Julius Nyerere ambayo mara kadhaa imeandaa mijadala ya wazi, lakini wakimtumia Jaji Warioba kama msemaji wake mkuu.
Kitendo hicho kimesababisha Warioba kuonekana kama yupo katika mgogoro na chama chake na siku aliyofanyiwa fujo na kupigwa katika ukumbi wa mikutano wa Ubungo Plaza, wanaodaiwa kuwa makada wa CCM wanatajwa kuhusika.

Viungo vingi vya binadamu vikiwa vimetupwa katika machimbo ya kokoto yaliyopo Bunju, Dar.
VIUNGO VYA BINADAMU VYASHTUA Jumatatu ya Julai 21, 2014, nchi ilipatwa na mshtuko mkubwa baada ya kusambaa kwa habari kuwa viungo vingi vya binadamu vilikutwa vikiwa vimetupwa katika machimbo ya kokoto yaliyopo Bunju, Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Watu wengi waliamini viungo hivyo vimetokana na mauaji ya halaiki, hasa baada ya kukutwa kwa mabaki ya mikono, miguu, mafuvu, viganja na vingine vingi. Lakini baadaye ikaja kuthibitika kuwa viungo hivyo vilitupwa kimakosa na Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Tiba na Teknolojia (IMTU), ambacho pia kinaendesha hospitali.
Viungo hivyo mbalimbali vya binadamu vilikuwa vikitumiwa kimasomo na madaktari wanafunzi, ambavyo vilipaswa kuteketezwa baada ya matumizi. Kitendo hicho kilisababisha serikali kukisimamisha kwa muda chuo hicho kutokana na uzembe huo. Viungo hivyo vya binadamu, hupatikana katika maiti mbalimbali zinazokosa ndugu wa kuwazika na hutolewa na hospitali ya Taifa Muhimbili.
Aliyekuwa mshindi wa miss Tanzania 2014, Sitti Mtemvu kabla ya kuvuliwa taji.
Kitendo hicho pia kilikosolewa na wachambuzi wa habari za kisiasa wakidai ulikuwa ni udhalilishwaji wa mtu aliyewahi kuwa Makamu wa Rais na Waziri Mkuu wa Tanzania na hivyo kuhoji ulinzi wake.MISS
TANZANIA YAFUNGIWA MIAKA 2 Shindano la Miss Tanzania limejijengea heshima kwa muda mrefu tokea lilipoanza tena mwaka 1994. Ingawa kumekuwa na malalamiko ya chinichini juu ya kuwepo kwa hila, safari hii lilijikuta likipata aibu kubwa, baada ya mshindi wake wa mwaka huu, Sitti Mtemvu kudaiwa kudanganya umri hivyo kuibua sauti zilizotaka kunyang’anywa kwa taji hilo.
Baada ya skendo hiyo kuchachamaa, Baraza la Sanaa la Taifa liliendelea na uchunguzi wake dhidi ya malalamiko mengi yaliyowahi kuripotiwa na katika tukio ambalo halikutarajiwa, shindano hilo limesimamishwa kwa miaka miwili kutofanyika na sababu nyingine iliyosababisha hatua hiyo, ni kugundulika kuwepo kwa rushwa ya ngono katika hatua mbalimbali za shindano hilo linaloanzia vitongojini.

HABARI KUBWA DAR--APIGWA RISASI AKIKIMBIA MAHAKAMANI KISUTU ASUBUHI HII,NI MTUHUMIWA WA MADAWA YA KULEVYA


Mtuhumiwa wa madawa ya kulevya raia wa Sierra Leone akiwa amepigwa risasi baada ya kutaka kuwatoroka askari magereza katika Mahakama ya Kisutu jijini Dar es Salaam.Habari zaid zinaswema kuwa mtuhumiwa huyo alifikishwa katika makhakama hiyo ya kisutu kwa ajili ya kusomewa mashtaka yake ndipo alipoamua kuwatoroka askari na kutaka kukimbia ndipo alipokutana na zahama hiyo.
Taarifa ambazo tunazipata ni kuwa inasemekana kuwa mtuhumiwa huyo amefariki dunia lakini bado hakuna yeyote aliyedhibitisha juu ya kifo hicho na mtandao huu upo makini kuhakikisha unapata ukweli wa taarifa hizi na endapo tutazipata tutakuwekea hapa.PICHA ZAIDI ZIPO CHINI

Tuesday, December 30, 2014

MJANE WA MWANAMUZIKI GURUMO APIGWA JEKI NA NSSF

Ofisa Uhusiano Mwandamizi wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Juma Kintu (wa pili kushoto) akimkabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya sh. mil 2 kwa mjane wa marehemu Muhidini Gurumo, Pili Kitwana.katikati ni Shirikisho la Muziki nchini (SHIMUTA),Addo November

Hatimaye mjane wa marehemu Muhidini Gurumo, Pili Kitwana amepokea Sh2 milioni kutoka Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii NSSF kwa ajili ya ununuzi wa Bajaji.


NSSF ilitoa fedha hizo ikiwa ni juhudi za Shirikisho la Muziki nchini (SHIMUTA), ambapo walimuahidi kumpatia mjane huyo kiasi cha fedha ambacho kitamuwezesha kununua bajaji imsaidie kuendesha maisha yake.

SIRI YA PHIRI KUTIMULIWA SIMBA SC HII HAPA.SOMA

Wachezaji wa Simba raia wa Kiganda ndio wamemponza kocha Mzambia
Patrick Phiri kufungashiwa virago ndani ya klabu hiyo ya Msimbazi huku Mserbia Goran
Kopunovic akitarajiwa kutua rasmi kesho Jumatano.


Habari za uhakika kutoka Simba zinasema kuwa uongozi wa klabu hiyo chini ya
mwenyekiti wake Evans Aveva uliketi juzi usiku majira ya saa mbili na kikao kumalizika
saa saba usiku kwa maazimio ya kumfukuza Phiri na jana jioni alikabidhiwa rasmi barua
yake ya kuachishwa kazi na nafasi yake kuchukuliwa na Serbia, Goran Kopunovic.

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AAGANA NA MABALOZI WA URUSI, CANADA NA ALGERIA

unnamedMakamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Balozi wa Urusi nchini Tanzania, Mhe. Alexander Rannkikh, wakati alipofika Ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Desemba 30, 2014 kwa ajili ya kumuaga baada ya kumaliza muda wake wa kazi nchini. Picha na OMR

AZAM, MTIBWA, SIMBA, YANGA KUCHEZA MAPINDUZI

tff_LOGO1
Timu za Azam, Mtibwa Sugar, Simba na Yanga zitashiriki michuano ya Kombe la Mapinduzi inayofanyika kisiwani Zanzibar kuanzia Januari 1 hadi 13 mwakani.
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetoa ruhusa kwa timu hizo kucheza mashindano hayo baada ya kuhakikishiwa na Chama cha Mpira wa Miguu Zanzibar (ZFA) kuwa kesi iliyofunguliwa dhidi ya viongozi wake imeondolewa mahakamani.
Kutokana na timu hizo kushiriki Kombe la Mapinduzi, mechi zao za raundi ya tisa na kumi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) zitachezwa katikati ya wiki baada ya kumaliza mechi zao za michuano hiyo.
Hivyo mechi za VPL ambazo hazitachezwa wikiendi hii ni kati ya Azam na Mtibwa Sugar, Mbeya City na Yanga, na ile kati ya Mgambo Shooting na Simba. Mechi za wikiendi ijayo zinazopisha michuano hiyo ni kati ya Kagera Sugar na Azam, Coastal Union na Yanga, Mbeya City na Simba, na Mtibwa Sugar na Tanzania Prisons.

URAIS CCM RUSHWA WAZI WAZI ,SOMA MAKALA HII ILIYOJICHUKULIA UMAARUFU LEO

Picha na maktaba,MAKALA HII MEANDKWA NA GAZETI LA MWANACHI 
 Ikiwa imebaki miezi 10 tu kabla ya kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu mwakani, CCM kinaonekana kuteswa na tuhuma za rushwa inayodaiwa kutolewa na makada wake wanaotajwa kutaka kuwania nafasi mbalimbali ukiwamo urais.
Hali hiyo inabainishwa na kauli za baadhi ya makada wa chama hicho katika ngazi mbalimbali ambao wameamua kulalamika waziwazi ama kupitia vyombo vya habari au kwenye mitandao ya kijamii.
Moja ya kauli hizo ni ile iliyotolewa juzi na Mbunge wa Bukoba Mjini, Balozi Khamis Kagasheki kwenye akaunti yake ya Twitter akisema: “Mgawo wa Xmass na Mwaka Mpya kwa wajumbe husika wa CCM ni kucheza na ugumu wa maisha uliopo. Ni ununuzi wa nafasi na si uwezo wa uongozi. Aibu.”
Alipotakiwa kufafanua kauli yake, Kagasheki alisema kwenye maoni yake hakutaja mtu licha ya kwamba wapo wengi wanaotoa zawadi, lakini baada ya kuandika katika mtandao ameandamwa na baadhi ya watu huku wengine wakimtolea lugha chafu.

MBONI SHOW SASA YAHAMIA TBC ONE

Mkurugenzi wa Mboni Show, Mboni Masimba (wa pili ktoka kulia) akizungumza na waandishi wa habari jana katika  ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo jijini Dar es Salaam wakati akitangaza kuanza kwa msimu wa tatu wa kipindi chake ‘The Mboni Show’ kinachotarajia kuanza Jan 2, 2015. Kushoto ni kiti Simpompa na kuanzia kulia ni Afisa Masoko wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (PSPF) Magira Werema na Kaimu Mkurugenzi wa Masoko TBC,Bw.Fadhili Chilumba.
Kutoka Kulia Afisa Masoko wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (PSPF) Magira Werema akizungumza wakati wa uzinduzi kipindi cha Mboni Show uliofanyika katika Ukumbi wa Idara Habari Maelezo jijini Dar es Salaam. Pembeni ni Kaimu Mkurugenzi wa Masoko TBC,Bw.Fadhili Chilumba pamoja na Mkurugenzi wa Mboni Show, Mboni Masimba.

michezo--PSPF KUWAKUTANISHA WACHEZAJI WA ZAMANI WA YANGA NA SIMBA

SIMBA
MFUKO wa Pensheni wa PSPF umedhamini mchezo wa kirafiki utakaowakutanisha wachezaji waliowahi kuwika katika timu kongwe nchini Simba na Yanga.

Mchezo huo unatarajiwa kufanyika tarehe 1 Januari 2015 katika uwanja wa chuo cha Bandari, Tandika jijini Dar es Salaam, kiingilio kitakuwa bure ikiwa ni zawadi ya mwaka mpya kutoka PSPF. 

Katika mchezo huo baadhi ya wachezaji wa Simba wanaotarajiwa kushuka uwanjani ni Thomas Kipese, George Lucas, Bita John, George Masatu, Mustafa Hoza, Emmanuel Gabriel, Idd seleman. Timu ya Simba inafanya mazoezi katika uwanja wa Leaders uliopo Kinondoni, ipo chini kocha mchezaji Kasongo Athuman. 

Monday, December 29, 2014

MVUA KIDOGO DAR IMEJAA MAJI,TIZAMA HAPA

Mvua iliyonyesha maeneo mbalimbali ya jiji la dar es salaam imesababisha maeneo mengi kujaa maji na kusababisha usumbufu mkubwa wa wakazi wa jiji hilo,picha kadhaa zinaonyesha hali halisi ya maeneo kadha ya jiji la Dar es salaam kwa sasa

JUKATA--RAIS KAMA UNAMPENDA MUHONGO MPE KAZI SHAMBANI KWAKO SIO UWAZIRI

Makamu mwenyekiti wa jukwaa la katiba Tanzania JUKATA ndugu HEBRON MWAKAGENDA akizungumza na wanahabari mapema leo kuhusu mambo mablimbali yaliyojiri mwaka 2014
 Jukwa la katiba nchini Tanzania JUKATA limemtaka  rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete kuwachkulia hatua mara moja wahusika wote waliotajwa kuchota pesa za account ya TEGETA ESCROW ikiwa ni pamoja na waziri wa nshati na madini nchini Tanzania Sospeter Muhongo.

        Hayo yamesemwa leo jijni Dar es salaam na makamu mwenyekiti wa jukwaa hilo ndugu HEBRON MWAKAGENDA wakati akizungumza na wanahabari juu ya matukio mbali mbali ya kikatiba yaliyojitokeza nchni Tanzania kwa mwaka 2014 tukiwa tunaelekea kuuanza mwaka mpya wa 2015.
Amesema kuwa vitendo vya wizi wa mabilioni na ufisadi mkubwa nchini ni doa kubwa kwa sura ya nchi ambapo rais anapaswa kuchukua hatua mara moja bila kujali chama wala itikadi,wala urafiki na mtu yoyote.
        
          “lazima rais awe mkali kama anampenda sana waziri muhongo na anapenda kumpa kazi basi akampe kazi ya kulima kwenye mashamba yake huko ila sio hii ya kuwaongoza watanzania kwani imeonekana wazi kuwa ameshindwa kulitumikia taifa”.amesema makagenda

        Aidha akzungumzia uchaguzi wa serikali za mitaa uliomalizika hivi karibuni nchini Tanzania amesema kuwa uchaguzi huo ulikumbwa na vitendo vya ukiukwaji wa sheria ambapo vilishughudiwa katika maeneo mengi, na maeneo mengine watu wakitoroka na masanduku ya kura jambo ambalo amesema kuwa sio ishara nzuri kwa nchi ya kidemocrasia kama hii.

         Aidha amesema kuwa vitendo hivi vyote ikiwa ni pamoja na  fujo sizizo na msingi katika chaguzi,pamoja na ufisadi wa escrow vyote hivi ni kuporomoka kwa maadili kwa watanzania ambapo amesema kuwa rasimu iliyokataliwa na bunge ilikuwa inapendekeza vifungu vya maadili lakini vifungu hivyo vyote vimenyofolewa katika katiba pendekezwa.
Katika hatua nyingne akizunguzia mchakato wa upatikanaji wa katiba mpya amesema kuwa sasa jukwaa la katiba Tanzania linapendekeza kuwa hatua zote zilizobaki za mchakato huu ziahirishwe hadi baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2015,ambapo itakuwa ni jukumu la rais mpya ajaye kuanza upya mchakato huo,ambapo amesema kuwa sababu kubwa za kuahirisha mchakato huo ni kutokana na ukweli kwamba Tanzania sasa inakabiliwa na  michakato muhimu kama uandikishwaji wa vitambulisho vya taifa,sakata la escrow,pamoja na uandikishwaji wa daftari la kudumu la wapiga kura kwa mfumo mpya wa BVR.



Saturday, December 27, 2014

MH. LOWASSA AMTEMBELEA WAZIRI WA MAMBO YA NDANI WA ZAMANI, MH. ALI AMEIR MOHAMED


Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa (kushoto) akielezwa jambo na Waziri waMambo ya Ndani wa zamani,Mh. Ali Ameir Mohamed wakati alipomtembelea nyumbani kwake eneo la Kichaviani, Jimbo la Donge, Zanzibar.Mh. Lowassa yuko visiwani humo kwa ajili ya mapumziko ya Krismasi.

JOKATE MWEGELLO ATOA MSAADA KITUO CHA YATIMA CHA EXTREM CHA TANDALE

2
 Miss Tanzania namba mbili 2006, mwanamitindo na mcheza filamu, Jokate Mwegello, akicheza na mmoja wa watoto wanaolelewa katika Kituo cha Yatima cha Extrem cha Tandale kwa Bi Mwamvua Jumanne, alipotembelea kuwapa zawadi ya Sikukuu ya Krismas na Mwaka Mpya. Zawadi alizotoa ni mchele, unga wa sembe, sabuni na ndala zenye nembo za Kidoti.  Picha na Jumanne Juma
7
Miss Tanzania namba mbili 2006, mwanamitindo na mcheza filamu, Jokate Mwegello, akimpa zawadi ya ndala mmoja wa watoto wanaolelewa katika Kituo cha Yatima cha Extrem cha Tandale kwa Bi Mwamvua Jumanne, alipotembelea kuwapa zawadi ya Sikukuu ya Krismas na Mwaka Mpya. Zawadi alizotoa ni mchele, unga wa sembe, sabuni na ndala zenye nembo za Kidoti.  Picha na Jumanne Juma
IMG_2647
Miss Tanzania namba mbili 2006, mwanamitindo na mcheza filamu, Jokate Mwegello, akiwa katika picha ya pamoja na watoto wanaolelewa katika Kituo cha Yatima cha Extrem cha Tandale kwa Bi Mwamvua Jumanne, alipotembelea kuwapa zawadi ya Sikukuu ya Krismas na Mwaka Mpya. Zawadi alizotoa ni mchele, unga wa sembe, sabuni na ndala zenye nembo za Kidoti.  Picha na Jumanne Juma

TANDALE SACCOS WAFANYA MKUTANO WAO MKUU WA MWAKA

Maelfu ya wanachama wa TANDALE SACCOS waliojitokeza katika mkutano wake mkuu uliofanyika leo jijini Dar es salaam 
Chama cha akiba na mikopo SACCOS kilichopo Dar es salaam kinachokwenda kwa jina la TANDALE SACCOS leo kimefanya mkutano wake mkuu wa mwaka ambao mkutano huo umefanyika katika hoteli ya lunch time magomeni jijini Dar es salaam mkutano ambao pia umetumika kuchagua viongozi wapya wa chama hicho ambacho kinatajwa kama SACCOS bora ndani ya jiji la Dar es salaam

Katibu wa bodi ya SACCOS ya TANDALE SACCOS Bi ZENA KAITILA akizungumza na wanahabari wakati wa mkutano wa mwaka wa chama hicho ambapo amesema kuwa chama hicho sasa kimetimiza zaidi ya wanachama hai elfu tisa,,ambapo ni idadi kubwa sana kulinganisha na baadhi ya SACCOS nyingine jijini dae es salaam.

Bi ZENA amesema kuwa hadi sasa wana mtaji wa zaidi ya bilioni moja na wanachama wake kwa sasa wana uwezo wa kukopa hadi milioni hamsini kwa mara moja kutokana mapato yao kuwa mazuri.

Amesema pamoja na mafanikio hayo bado changamoto hazikosekani ambapo amesema kuwa moja ya changamoto hizo ni pamoja na kuwa na wanachama ambao wamekuwa sio wanachama hai ambao wamekuwa wakishindwa kuchukua mkopo  na kurudisha kwa wakati jambo ambalo limekuwa ni chanagamito kubwa kwa chama chao

Hadi mtandao huu unaondoka katika eneo la tukio chama hicho kilikuwa katika uchaguzi wa viongozi wao wapya na hapa ni viongozi mbali mbali wa chama hicho wakipongezana baada ya kuchaguliwa kukiongoza chama hicho

KAMA ULIKOSA MANENO YA TIBAIJUKA BAADA YA KUFIKA JIMBONI KWAKE





Prof. Tibaijuka akizungumza na wananchi hao,  aliwataka wasisikitike kwa kuvuliwa kwake nafasi ya uwaziri kwani aliyetoa ndiye aliyetwaa.

           Alisema binafsi hajutii kuvuliwa cheo hicho kwani kama angekuwa na tamaa ya cheo asingetoka Umoja wa Mataifa (UN) ambako alilazimika kuacha cheo ili akawatumikie wananchi wa jimbo la Muleba.

       “Najua wengi wenu mmeumizwa na masuala ya sakata la Escrow, niwaombe yasiwaumize vichwa kwani Bwana alitoa na Bwana ametwaa. Jina lake lihimidiwe,” alisema Prof. Tibaijuka.

          Prof. Tibaijuka alisema kimsingi, suala la yeye kupokea fedha kutoka kwa James Rugemalira halina utata kwani fedha hizo zilitolewa kuwasaidia kuwalipia karo baadhi ya wanafunzi wanasoma kwenye shule zake, hivyo hawezi kuwa mbinafsi kama ilivyotafsiriwa na baadhi ya Watanzania.

           “Watanzania tumejaa ubinafsi, kila mtu anafikiria kila anafanya jambo anategemea kupata posho, na niwahakikishieni mimi sina uchu wa ubinafsi wala tamaa za vyeo kwani kama ni cheo nilichoacha UN kilikuwa kikubwa zaidi,” alisema akimaanisha ni cha ukamishna mkuu wa makazi.

HISTORIA MPYAAA--ZITTO KABWE NA LIPUMBA JUKWAA MOJA FUNGA MWAKA


MKUTANO WA KIHISTORIA MTWARA MJINI

NI VIWANJA VYA MASHUJAA MTWARA MJINI 31/12/2014 SAA NANE MCHANA.
Professa Ibrahim Lipumba bingwa wa uchumi duniani ambaye pia ni mwenyekiti mwenza wa ukawa KUUNGURUMA pamoja na

 Zitto Zuberi Kabwe Mwami Luyaga(MB) ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya PAC KUZUNGUMZA pamoja na
Wabunge watano wa JMT wanaotokana na Umoja wa katiba ya wananchi UKAWA WATAONGEA siku hiyo.
Kivutio kikubwa siku hiyo ni ZITTO KABWE akiwa pamoja na mchumi NGULI wa dunia Profesa LIPUMBA katika jukwaa moja.
Safari ya UKOMBOZI ina anzia MTWARA sehemu muhimu katika uchumi wa kisasa kutokana na upatikanaji wa GESI na MAFUTA.
ZITTO aliyejizolea umaarufu wa kufanya tafiti za kisomi ana Shahada ya uzamili ya sheria na biashara ni MSOMI kijana.
Prof LIPUMBA ana Shahada ya udaktari wa falsafa (PhD) maeneo yake ya utaalamu ni(a)Maendeleo ya uchumi (b) Uchumi wa Kilimo (c)Biashara za Kimataifa na Fedha(d) Uchumi Mpana (Macroeconomics) ni M/kiti wa JOPO la Maprofesa bingwa wa uchumi duniani.
Taarifa zilizopo ZITTO KABWE na Professa LIPUMBA kuzunguka nchi nzima baada ya MTWARA.
ZITTO kufafanua wizi wa Escrow kwa kuwataja majina wezi wote na viwango vya fedha walivyochukua
Professa LIPUMBA kueleza namna TANZANIA inaweza kuondokana na umasikini kama itafuata ushauri wake.
HII NI TAREHE 31/12/2014 SAA 8:00 MCHANA VIWANJA NI MASHUJAA MTWARA MJINI