Friday, June 30, 2017

TGNP MTANDAO YATOA SEMINA KWA WAKAZI WA KIBO KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA

Mtandao wa jinsia Tanzania TGNP siku ya jana tarehe 30 mwezi juni umefanya semina fupi iliyofanyika maeneo ya Kimara kibo iliyokutanisha baadhi ya wakazi wa kata hiyo lengo likiwa ni kujadili ukatili wa kijinsia uliopo kwenye kata hiyo.
Bi. Agness Lukani akiongoza semina ya ukatili wa kijinsia kwa wakazi wa Kimara Kibo iliyofanyika mapema jana jijini Dar es salaam
Akiongoza semina hiyo iliyodumu kwa takribani masaa mawili dada Agness Lukani aliweza kuibua changamoto mablimbali zinazowakabiri watoto wa kike pamoja wanawake kwa ujumla kutokana na ukatili wa kijinsia. Baadhi ya vijana waliweza kuainisha baadhi ya vitendo vya ukatili vinavyopatikana katika eneo hilo na miongoni mwake ni.

Baadhi ya vijana walioudhuria semina ya ukatili wa kijinsia wakifuatilia kwa makini mafunzo yanayotolewa kwa njia ya Televisheni mapema jana Kimara Kibo jijini Dar es salaam
Vijana wengi kutelekeza familia zao hii inaonyesha ni sababu kubwa kwa wakazi wa eneo la kibo kwa kuwa unakuta kijana anampa mimba binti na hatimaye kukimbia hivyo kumuacha binti huyo kuishi na mimba hiyo kwa tabu mpaka anapojifungua na baadae akiona mtoto kamekua anakuja kudai mtoto wake.

Kupigwa kwa wanawake pia ni miongoni mwa aina nyingine ya ukatili ambayo inapatikana kwenye eneo hilo na mara nyingi unakuta ni wivu wa kimapenzi hii inasababisha mtoto wa kike kupigwa kwa maana nakuwa hana uwezo wa kupigana na mwanaume na mwisho binti anakaa kimya pasipo kutoa taarifa popote hali inyofanya kitendo hicho kuwa endelevu cha yeye kupigwa kila siku.

Tatizo la mimba za utotoni pia limeendelea kuwepo kwa wanafunzi na wasiwanafunzi kutokanana maeneo waliyopo kuwa ni mjini lakini pia shule kuwepo mbali, na uwepo vijiwe vya vijana wasio na maadili mazuri kuendelea kuwarubuni watoto hao kwa kigezo cha kutojua kuwa ni wanafunzi.

Tatizo lingine ni kupiga watoto kupita kiasi hii nayo imeelezwa kuwa ni miongoni mwa ukatili unaopatikana eneo hilo, pale ambapo unakuta mtoto anakosea mzazi anashindwa kumkanya au kutafuta njia mbadala ya kumrekebisha na kuona suruhu kwake ni kumpiga hali inayofanya kumuumiza mtoto na sio kumrekebisha kama anavyodhani.

Baadhi ya mabinti walipaza sauti zao na kusema kuwa wanaume wao huwa wanashindwa kuweka usawa na kuwanyanyasa wao kwa kigezo cha kuwa na hali ni ngumu na kuwaomba wenzi wao wavumilie, Lakini inapotokea wamepata pesa nyumbani hawaonekani, na ikitokea wamerudi nyumbani wakiwa wamelewa hali inayowanfanya kushindwa kuwaelewa wakati wanakuwa pamoja kwenye shida ila raha wanakula na wengine.

Baada ya kupata mafunzo yaliyotolewa kwa kupitia Televisheni ilifikia muda wa majadiliano, kujadili walichojifunza kupitia kipindi walichokiangalia kwenye Televisheni

Na mwisho wakazi hao wa kibo waliweza kuafikiana kuwa waadilifu kwa familia zao na kumchukulia mtoto wa mwenzako ni wakwako kuweza kumkanya endapo atakosea ili kuweza kupunguza mimba za utotoni na aina nyingine za ukatili wa kijinsia. Na kuendelea kupongeza jitihada zinazofanywa na mtandao wa jinsia TGNP kuwapa elimu ya kuepuka vitendo vya ukatili wa kijinsia.

                         

                         

WIZARA YA MAMBO YA NDANI:- WATUHUMIWA 16 WA KIBITI SURA ZAO ZIMESHAPATIKANA

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Eng. Hamad Yussuf Masauni ametangaza kuwa, Jeshi la Polisi linawaska watuhumiwa 16 wa mauaji ambayo yamekuwa yakiendelea kufanyika katika maeneo ya Kibiti, Mkuranga na Rufiji Mkoani Pwani kwa muda mrefu sasa.


Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Masauni amesema kuwa watuhumiwa hao wanafahamika na tayari jeshi la polisi lina picha za watuhumiwa wote ambao wanasakwa.

“Nchi yetu ipo katika changamoto ya matukio katika maeneo ya Kibiti na Rufiji, ambapo matukio haya wakati mwingine yanaripotiwa ndivyo sivyo na vyombo vya habari na kusababisha hofu kwa wananchi. Sisi kama serikali lazima tuwatoe hofu wananchi wetu. Tuwaombe wanahabari mfikishe ujumbe sahihi zaidi.

“Jana tulifanikiwa kuwadhibiti wahalifu wawili kabla hawajatekeleza uhalifu wao, kwa hiyo jeshi letu linafanya kazi vizuri sana. Suala la kumaliza uhalifu wa Kibiti ni la lazima wala sio la mjadala tena.

“Maandalizi ya mkoa Mpya wa Kipolisi wa Rufiji yamekamilika na Kamanda wa Polisi wa Mkoa huo tayari ameshateuliwa,” alisema Masauni.

TAASISI YA LECRI CONSULT YAWAPA VIJANA ZAIDI YA 100, MBINU ZA KUPAMBANA NA CHANGAMOTO ZA AJIRA

Taasisi inayotoa huduma na ushauri wa kisheria na masuala ya haki za watoto na vijana ya  Lecri  Consult. Leo tarehe 30 ya mwezi juni imewakutanisha vijana zaidi ya 100 waliomaliza  vyuo vikuu mbalimbali hapa nchini lengo likiwa ni kuwajengea uwezo wa kujitambua na kutambua fursa zilizopo mbele yao.
Mkurugenzi Mtendaji ambaye pia ni Mwanasheria wa Lecri Consult Bi. Edna Kamelek akiongea na wageni walioudhuria kwenye semina ya uwezeshaji vijana  iliyofanyika mapema leo jijini Dar es salaam

Akifungua semina hiyo mkurugenzi mtendaji wa Lecri Consult Bi. Edna Kamalek alisema kuwa semina hii imelenga kwa vijana waliomaliza vyuo ambao hawana ajira ili kuweza kuwajengea uwezo kutatua changamoto zao na kuwapa ujasiri pindi wanapohitajika kwenye usahili.

“Na kwa wale vijana waliopenda kujiajiri tunawajengea uwezo wa kujisimamia na kuendesha biashara zao binafsi” alisema mkurugenzi

Lakini pia kwa wale vijana ambao tayari wameshapata ajira wanapewa elimu, miiko na maadili ya kazi ili kuweza kuboresha ufanisi wao na wasifanye kazi kwa mazoea.
Naibu Mkurugenzi ofisi ya Waziri mkuu uamasishaji vijana na uwezeshaji vijana kiuchumi Bi. Esther Riwa kiongea na wageni waalikwa kwenye semina wa uwezeshaji vijana mapema leo jijini Dar es salaam
Akitoa elimu hiyo kwa vijana Naibu Mkurugenzi ofisi ya Waziri mkuu uamasishaji vijana na uwezeshaji vijana kiuchumi Bi. Esther Riwa alisema kuwa tatizo kubwa ni mitaala tuliyonayo  haimjengi mtoto akimaliza aje kupata ajira. “lakini pia tatizo lingine ni kutofuata maono vijana wengi huchagua masomo kwa kufuata mkumbo au kwa kushinikizwa na wazazi au walezi wao na mwisho wake kushindwa kufikia malengo waliyojiwekea ” alisema Bi Esther

Alisisitiza pia vijana wengi mitazamo yao ni kwamba wakimaliza kusoma moja kwa moja kuajiriwa na hivyo kushindwa kuzitafuta fursa za kujiajiri kwa kutumia rasilimali zilizopo hapa nchini kama kama ardhi kuwekeza kwenye kilimo, bahari, mali asili nk.


Bi. Estha alisema kuwa  vijana wengi wanapenda kuingia kwenye ujasiliamali  lakini hawana mbinu za kibiashara na matokeo yake ufanya biashara zenye kipato kidogo hali inayofanya kushindwa kufikia malengo yaliyowekwa na serikali ya kuondokana na umasikini. Na kwa kupitia semina vijana wataweza kuzinduka na kuziangalia fursa zenye matokeo mazuri hivyo kupunguza wimbi la umasikini kwa taifa.
baadhi ya wageni waalikwa walioudhuria kwenye semina ya uwezeshaji vijana iliyofanyika mapema leo jijini Dar es salaam
Bi. Estasia Ngowi akitoa mrejesho baada ya kupata nafasi  ya kuhudhuria tena kwenye semina ya uwezeshaji vijana iliyofanyika mapema leo jijini D
ar es salaam
Baadhi ya vijana walioudhuria semina hiyo

MWALIMU WA SEKONDARI AFUMANIWA AKIFANYA MAPENZI NA MWANAFUNZI WAKE DARASANI


Mkuu wa Wilaya ya Wanging'ombe, Mkoani Njombe, Ally Kasinge(pichani) ameagiza kushikiliwa kwa Makamu Mkuu wa shule ya sekondari Wanike, iliyopo katika wilaya hiyo baada ya kukamatwa akifanya mapenzi na mwanafunzi wake darasani usiku.

Kasinge ametoa agizo hilo baada ya kuwepo taarifa ya kuwepo kwa watu wanaotaka kumsaidia mwalimu huyo kuvuruga ushahidi kwa kupanga na wanafunzi wenye ushahidi huo kuongea tofauti na tukio.

"Kuanzia wanafunzi waliotimuliwa wahojiwe na polisi na wale wanafunzi wengine waliotajwa pia wahojiwe na polisi na mwalimu mwenyewe pia aendelee kushikiliwa .Huyo ambaye anatuhumiwa aendelee kushiliwa na polisi mpaka tupate majibu, kwa sababu akibaki nje ataendelea kutengeneza mazingira ya kutengeneza mtandao wa kutaka kumsaidia na kupotosha ushaidi" alisema Mkuu wa Wilaya Ally Kasinge

Mbali na hilo shule ya sekondari ya Wanging'ombe pamoja na Wanike zimepandishwa hadhi na sasa zitapokea wanafunzi wa kidato cha tano, walimu wa shule hizo wameweka wazi kuwa shule hizo zinachangamoto ya walimu wa sayansi ambao ni wachache ukilinganisha na walimu wa masomo ya sanaa.

Merck Launches “Merck More Than a Mother” Media Recognition Awards 2017

Merck Launches “Merck More Than a Mother” Media Recognition Awards 2017

Merck More Than a Mother” Media Recognition Awards are for journalists , media students and bloggers  alike

·         Merck announces the start of their East - African “More than a Mother” Media awards  for the first time in Tanzania
·         Merck seeks to raise awareness about the prevention of infertility in the country
·         “Merck More than a Mother“ Media Awards  will improve awareness of journalists as well as their recognition in creating a culture shift in  the stigma around infertility in Tanzania

– Merck, a leading science and technology company, has launched media recognition awards dubbed the Merck More than a Mother Media Recognition Awards in order to award journalists and media students in East Africa who have done compelling, educative and informative stories that have shaped the conversation on infertility in Africa. The importance of  journalism and the media today cannot be overlooked thus Merck thought it prudent to initiate a media competition to appreciate the good work being done by journalists and media students in the East African Region.

Speaking during the launch, Dr. Rasha Kelej the Chief Social Officer of Merck emphasized: “I created this campaign after I had seen women who suffered violence and discrimination due to their infertility. Infertile women in Africa suffer a lot due to their conditions, worst of all is that they are sometimes physically assaulted ostracized and even abandoned due to their infertility; this has to stop hence I believe the media can do a great job in ensuring that such stories are told so that these women can find the respect and the help they deserve, media is an essential player and critical partner to create any culture shift.”

The aim of the Awards is to raise awareness about the critical role the media can play in breaking the stigma around infertility. It also aims to change the culture of discrimination and abuse of infertile women while educating the public about infertility prevention, management and male infertility. In addition, the campaign aims to encourage men to discuss their infertility condition openly, support their wives through the journey of testing and treatment.
Merck emphasized in a statement circulated to the press: “We are happy to introduce these awards.. We believe that improving access as well as awareness to regulated and equitable fertility care is important, but it is even more important to intervene to decrease stigmatization and social suffering arising from this condition”.

“The media awards is the right step in making sure that fertility related stories are given good coverage and reported accurately and positively so that those who are suffering in silence can come out and seek help through medication or counseling. I am proud to be associated with this initiative and I look forward to the competition”.

Tom Mshindi, one of the judges emphasized: “I appreciate the role Merck is playing in combating the issue of infertility especially in rural Africa. This is an initiative that I fully endorse now that the media has also been incorporated in the greater goal of ensuring that stigmatization associated with infertility and its  related complications  are seriously addressed at all levels in society”.
Renee Ngamau who is also a judge in the competition stated, “As a woman this is an Initiative that I fully connect with and I firmly believe in the idea behind Merck More than a Mother campaign. The media must now take a front row in telling the stories of these women thus ensuring that we ease their suffering”.

The stories targeted are those of infertile women sharing their suffering and abuse by their husbands, families or communities due to their condition. It is very critical to share these stories with the public to build advocacy of the need to change such behavior and break this taboo in general. It will also provide a platform for those who have sought treatment to advise others on the journey and support those undergoing infertility treatments.

MERCK urged the Tanzanian health stakeholders, media and students alike to participate fully in the competion in order to reduce the stigma of infertility, create awareness and define interventions to improve access to better fertility care in Africa. “Let you voice heard and let’s work together to create a culture shift.

 “Journalists should not only see this as  competition with  reward prizes, but also as an opportunity to be agents of change in the whole issue of infertility. It is definitely a big problem, thus stories need to be told and retold about it so that people are conversant with the suffering of women, men and families who are affected with infertility.”
Award winners will be picked by a judging panel which consists of experts from diverse professional backgrounds including journalists, communications experts and media managers, will walk away with cash prizes as high $5,000.  The categories are divided into two mainly Journalists & students and into subcategories of multimedia   print   radio & online.

The prize awards for journalists will include Multimedia story - USD 5000, print 1500, radio 1500 and Online USD 1500. For students; Multimedia will win USD 3000, print 1000, radio 1000 and Online USD 1000.

The Award is open to print, video broadcast, photo journalists and media students whose stories appear in newspapers, websites, blogs and television and that target the public.

TGGA YATOA SOMO JUKWAA LA UWEZESHAJI WANAWAKE KIUCHUMI KISARAWE

 Katibu Tawala wa Wilaya ya Kisarawe, Mtera Mwampamba (kulia) akipata maelezo kutoka kwa Kamishna wa Chama cha Tanzania Girl Guides (TGGA) Makao Makuu, Rose  Majuva kuhusu kazi zinazofanywa na chama hicho ikiwemo kuwapa uwezo wanawake wa kujitambua na kujiamini alipokwenda kuzindua Jukwaa la Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi wilayani humo.

Majuva aliwaasa wanawaje kuacha kutumia mikopo ya benki kuchezea ngoma bali waitumie kujiendeleza kibiashara na kuwa na tabia ya kulipa kwa wakati mikopo hiyo. Pia aliwaeleza mbinu mbalimbali za kufanya biashara na miiko yake.
 Wananchi wakisikiiza kwa makini maelezo kutoka kwa Mkufunzi wa TGGA, Valentina Gonza jijsi ya kutengeneza jiko la kutumia mwanga wa jua kupikia vyakula mbalimbali kwa gharama nafuu wakati wa maonesho yaliyofanyika wakati wa uzinduzi wa jukwaa hilo mjini Kisarawe.

 Girl Guides wa TGGA, wakitengeneza Green House ya kupanda matunda na mbogamboga majumbani waliposhiriki uzinduzi wa Jukwaa la Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi wilayani Kisarawe. Kutoka kushoto ni Rachel Baganyire kutoka Uganda, Michelle kutoka Rwanda na Happy Mshana wa Makao Makuu ya TGGA, Dar es Salaam.
 Kamishna wa Makao Makuu ya TGGA, Rose Majuva (kulia) akisoma maadili ya kiongozi anavyotakiwa awe wakati wa uchaguzi wa viongozi wa Jukwaa la Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi Wilaya ya Kisarawe.
 Mkufunzi wa TGGA, Makao Makuu Dar es Salaam, Ruth Namatanga akigawa karatasi ya kupigia kura kwa Wajasiriamali wakati wa uchaguzi wa viongozi wa Jukwaa hilo.
 Mkufunzi wa TGGA, Makao Makuu Dar es Salaam,Rehema Kijazi akigawa karatasi ya kupigia kura kwa Wajasiriamali wakati wa uchaguzi wa viongozi wa Jukwaa hilo.
 Mkufunzi wa TGGA, Makao Makuu Dar es Salaam, Valentina Gonza akigawa karatasi ya kupigia kura kwa Wajasiriamali wakati wa uchaguzi wa viongozi wa Jukwaa hilo.
 Mkufunzi wa TGGA, Makao Makuu Dar es Salaam, Ruth Namatanga akikusanya kura kwa Wajasiriamali wakati wa uchaguzi wa viongozi wa Jukwaa hilo.
 Baadhi ya viongozi wa TGGA wakihesabu kura wakati wa uchaguzi huo
 Viongozi wa TGGA wakiwa kwenye banda lao wakati wa maonesho yaliyofanyika wakati wa uzinduzi wa Jukwaa hilo mjini Kisarawe
 Katibu Tawala wa Wilaya ya Kisarawe, Mtera Mwampamba (kulia),  akiangalia kiroba cha mkaa uliotengenezwa kiasili kwa kutumia taka mbalimbali alipokuwa akitembelea  mabanda ya wajasiriamali kabla ya kuzindua Jukwaa hilo. Kushoto ni Gifti Mbaraka wa banda hilo la Vijana Wasiriamali Wakulima Kisarawe. Katikati ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kisarawe, Mussa Gama.
 Mwampamba akiangalia bidhaa mbalimbali za wajasiriamali
 Girl Guides kutoka Madagascar akijitambulisha wakati wa mkutano wa Jukwaa hilo. Kutoka kulia ni Rachel Baganyire kutoka Uganda na Michelle kutoka Rwanda. Vijana hao wapo nchini kwa miezi sita katika programu ya kubadilishana uozefu katika masuala ya utamaduni, uongozi na ujasiriamali
Mkufunzi kutoka Makao Makuu ta TGGA, Happy Mshana akielezea jinsi alivyopata uzoefu alipoiwakilisha TGGA kwenye mafunzo ya kubadilisha uzoefu nchini Madagascar

Thursday, June 29, 2017

KAULI YA SIRRO ALIPOTEMBELEA KIBITI ALIPOCHOMWA MOTO MWENYEKITI WA KIJIJI


Siku moja baada ya kuripotiwa mauaji ya Mwenyekiti wa Kitongoji na Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Mangwi kilichopo Kata ya Mchukwi wilayani Kibiti katika Mkoa wa Pwani, IGP Simon Sirro ametembelea kijijini hapo kutoa pole kwa wafiwa.
Aidha, IGP Sirro amewataka wananchi kijijini hapo kutowafumbia macho wahalifu wanaotenda mauaji hayo akiwataka kushirikiana na Jeshi la Polisi kwa kutoa taarifa za wahalifu hao.

BARAZA LA WAZEE CHADEMA LA TOA TAMKO KWA MZEE MWINYI...


Baraza la Wazee wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), limetoa kauli kali kwa rais mstaafu, Ali Hassan Mwinyi, kufuatia kauli aliyoitoa kwenye Sala ya Eid el Fitr, Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam, Jumatatu iliyopita Juni 26.

Katika sala ya Eid, mzee Mwinyi alisema anamkubali sana rais Magufuli kwa jinsi anavyoinyoosha nchi, na kusema kama isingekuwa kubanwa na katiba, alitakiwa aachwe atawale milele.


Kwa kauli moja, wazee hao wamewataka wazee wenzao wa CCM, kukaa na mzee Mwinyi na kumuonya kuhusu kauli zake hizo, huku wakiwataka pia wazee wa CCM, kukaa na Rais Magufuli na kumuonya Mwinyi kwa sababu matamshi yake ni kinyume kabisa na katiba.


Kwa upande wake, Profesa Baregu, alisema mzee Mwinyi amewahi kusema nchi inavyoongozwa ni kama gari lisilo na usukani, akahoji iweje abadilishe mawazo yake na kuanza kuzungumza lugha tofauti, akijifanya anamkubali Rais Magufuli?

Naye Arcado Ntagazwa, alisema wananchi wote wanampongeza Rais Magufuli kwa sasa lakini hawajui matokeo ya maamuzi anayoyafanya leo kesho yatakuwaje na je, kesho atatoa maamuzi gani?

DC LYANIVA ATOA SIKU MBILI KWA WADAIWA SUGU KULIPA ZAIDI YA BILION 6.

Mkuu wa Wilaya ya Temeke Felix Lyaniva kufanya oparesheni maalum kwa wadaiwa sugu Julai Mosi mwaka huu.


Akizungumza leo jijini Dar es Salaam DC Lyaniva ameeleza kuwa zoezi hilo litalenga kukusanya kodi kwa wale wadaiwa sugu ambao wamekuwa wakidaiwa na Halmashauri hiyo kwa muda mrefu.

DC Lyaniva ametaja idadi ya wadaiwa sugu kuwa ni 142 ambapo wadaiwa wa leseni za biashara wakiongoza kwa idadi kubwa ya wadaiwa 69, ushuru wa huduma 52 na wadaiwa sugu kwa upande wa masoko wakiwa ni 21.

Jambo ambalo limepelekea halimashauri hiyo ya wilaya ya Temeke kutofikia malengo ya makusanyo ya kodi ya shilingi bilioni 29 ambapo wamefanikiwa kukusanya bilioni 23 pekee huku zaidi ya bilioni 6 zikibakia kwa wadaiwa sugu.

DC Lyaniva amesisitiza kuwa kwa wasiolipa kabla ya tarehe mosi ya mwezi Julai mwaka huu watachukuliwa hatua kali za kisheria, hivyo ni vyema wakatimiza wajibu huo haraka iwezekanavyo na kufafanua kuwa kwa umuhimu wa jambo hilo ofisi zitakuwa wazi mpaka siku ya jumapili.

TGNP MTANDAO WATOA SEMINA KWA WANANCHI JUU YA HAKI YA UHURU WA KUJIELEZA.

Mtandao wa Jinsia nchini Tanzania(TGNP) watoa semina kwa wananchi na wanaharakati juu ya kutambua haki yao ya msingi ya uhuru wa kujieleza(Freedom of speech).

Afisa mipango na Mwanasheria toka Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu Bi. Happines Michael akitoa mawasilisho kwenye semina iliyoandaliwa na Mtandao wa Jinsia Tanzania(TGNP) Mabibo jijini Dar es salaam

Akitoa mafunzo hayo ndani ya ukumbi wa Mtandao huo, Mabibo jijini Dar es salaam Afisa Program na Mwanasheria toka Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu, Bi. Happines Michael amesema ni muhimu kwa wananchi wote kuitambua haki hii kwa maana ni haki yao kikatiba na inatambulika kimataifa, hivyo wananchi wasiwe na hofu pindi wanapoidai haki yao na wanapotaka kutoa maoni yao ila wasivuke mipaka.

Bi Happines amewambia wananchi na wanaharakati walioudhuria kwenye semina hiyo kuwa kila mwananchi ana haki ya kutafuta kutoa au kupokea taarifa toka katika jamii yake pindi anapohitaji bila kikwazo chochote maana ni haki yake ya msingi kikatiba na inatambulika kimataifa kupitia  mikataba ambayo nchi imeingia, kama vile Tamko la haki za binadamu katika ibara ya 19 na mkataba wa kimataifa wa haki za kisiasa na kiraia katika ibara ya 19.
baadhi ya wageni walioudhuria kwenye semina ilifanyika makao makuu ya Mtandao wa Jinsia nchi Tanzania (TGNP) wakifuatilia semina hiyo kwa makini
"Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, Ibara ya 18 haki hii inalindwa kwa raia kupewa uhuru wa kujieleza, kutafuta na kupokea taarifa toka kwa wengine, pamoja na haki ya kusoma Magazeti, kusikiliza Matangazo na kushiriki kwenye mijadala ya Umma au binafsi".alisema Hapiness.
Aidha alizitaja baadhi ya sheria kandamizi ambazo zimewekwa ndani ya nchi na zimekuwa zikinyima uhuru wa wananchi katika kujieleza, kutafuta na kupokea taarifa kuwa ni sheria ya magazeti ya mwaka 1976, Sheria ya usalama wa Taifa ya mwaka 1970, Sheria ya utangazaji ya Tanzania ya Mwaka 1993, na hata sheria za hivi karibuni kama ya makosa ya mtandaoni ya mwaka 2015 bado zinawanyima raia wakiwemo wasanii, Wanahabari na hata wanasiasa uhuru wa kujieleza na kupokokea taarifa toka kwenye vyombo mbali mbali ikiwemo intanet.
Baadhi ya wageni na wanaharakati wakifuatilia semina iliyofanyika mapema jana jijini Dar ers salaam
"Kwa sasa nahisi mmeona kuna baadhi ya waandishi wanashindwa kutoa baadhi ya taarifa kuhofia maisha yao, wasanii nao wanashindwa kutunga baadhi ya nyimbo zenye kukosoa kwa kuhofia kukamatwa yote kutokana na sheria hizi kandamizi.".alisema Afisa.

Hata hivyo aliwataka Wananchi/Wanaharakati kupaza sauti zao pindi wanapoona uhuru huu unakosekana katika jamii kwani Kituo cha Sharia na Haki za Binadamu kimekuwa kikichukua hatua mbali mbali zikiwemo kufungua kesi dhidi ya taasisi au shirika ambalo linakandamiza  haki hiyo na kuitaka serikali ibadilishe au kurekebisha sharia hizo maana zinakwenda kinyume Demokrasia.

                             

                             

MALINZI, AVEVA, KABURU, MWESIGWA WAPANDISHWA KIZIMBANI KISUTU




Rais wa TFF, Jamal Malinzi na Katibu Mkuu wa TFF, Mwesigwa Celestine wamepandishwa kizimbani leo jijini Dar es Salaam.

Pamoja na viongozi hao wa TFF, viongozi wawili wakuu wa Simba, Rais Evans Aveva na makamu wake, Geofrey Nyange ‘Kaburu’ nao wamepandishwa kizimbani baada ya wote wanne kushikiliwa na kuhojiwa na Takukuru, jana.

Taarifa za awali zilieleza kuwa Malinzi na Mwesigwa walikuwa wanatuhumiwa kwa matumizi mabaya ya ofisi na utakatishaji.

Lakini jana jioni, Mwanasheria wa Malinzi, Alloyce Komba akasema hakuwa amejua walikamatwa kwa sababu zipi na hakuambiwa.

Mbali na hivyo, Komba alitaka wapewe dhamana kwa kuwa ni wanatu wanaofahamika na wanatakiwa kwenda kwenye usaili wa kuwania uongozi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).

Wednesday, June 28, 2017

Kampuni ya Tigo ilivyowafuturisha watoto wa kituo cha yatima cha Umra Magomeni

Baadhi ya wafanyakazi wa kampuni ya Tigo wakiwa kwenye foleni kushiriki futari pamoja na watoto wa kituo cha Umra Orphanage kilichopo Magomeni Jijini Dar es Salaam
Watoto wa kituo cha Umra Orphanage kilichopo Magomeni wakipata futari iliyoandaliwa na kampuni ya Tigo mwishoni mwa wiki iliyopita jijini Dar Es Salaam.

Watoto wa kituo cha Umra Orphanage kilichopo Magomeni wakiwa katika foleni kupata  futari iliyoandaliwa na kampuni ya Tigo mwishoni mwa wiki iliyopita jijini Dar Es Salaam.


Baadhi ya wafanyakazi wa kampuni ya Tigo wakiwa kwenye foleni kushiriki futari pamoja na watoto wa kituo cha Umra Orphanage kilichopo Magomeni Jijini Dar es Salaam
Watoto wa kituo cha Umra Orphanage kilichopo Magomeni wakipata futari iliyoandaliwa na kampuni ya Tigo mwishoni mwa wiki iliyopita jijini Dar Es Salaam.

CUF KUIFIKISHA KORTINI WAKALA WA USAJILI, UFILISI NA UDHAMINI (RITA)

Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi(CUF), Maalim Seif Sharif Hamad, akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, kuhusu madai ya muendelezo wa hujuma dhidi ya chama hicho zinazofanywa na ofisi ya msaji wa vyama vya siasa nchini. Kulia ni Mbunge wa Viti Maalumu wa chama hicho, Seveline Mwijage.

TGGA YAKABIDHI VYETI KWA WALIOHITIMU MAFUNZO YA MWANAMKE KUJIAMINI, KUJITAMBUA NA KUWA JASIRI

 Viongozi na walimu wa Chama cha Tanzania Girl Guides (TGGA), wakishangilia baada ya kumaliza mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kujiamini, kujitambua na ujasiri katika kambi iliyofanyika hivi karibuni  eneo la Mombasa, Dar es Salaam. Zaidi ya 36 kutoka mikoa mbalimbali walishiriki kwenye mafunzo hayo. Pia katika mafunmzo hayo yaliyofanyika kwa wiki moja yalihudhuriwa na viongozi kutoka nchi za Uganda, Rwanda na Madagascar

Mgeni rasmi katika hafla ya kufungakambi hiyo yalifanywa na Katibu Mkuu wa TGGA Tanzania, Grace Shaba, ambaye aliwaasa kuyatumia vizuri mafunzo hayo kwenda kuanzisha kambi za kuwafundisha wanachama mikoani wanakotoka. 
 Baadhi ya wahitimu wa mafunzo hayo wakiruka kwa furaha
 Katibu Mkuu wa TGGA, Grace Shaba akimkabidhi cheti mmoja wa walimu waliohitimu mafunzo hayo.
 Grace Shaba akimkabidhi m cheti mmoja wa wahitimu kutoka Chuo Kikuu cha Dodoma, Jestina Philip
 Grace Shaba akimkabidhi cheti Makamu Mwenyekiti wa TGGA Mkoa wa  Lindi, Sharifa
 Grace Shaba akimkabidhi cheti Happy wa Makao Makuu ya TGGA Dar es Salaam

 Mwalimu wa Girl Guides , Valentina akikabidhiwa cheti
 Kiongozi wa Girl Guides wa TGGA, Makao Makuu, Rehema Kijazi akipokea cheti kutoka kwa Katibu Mkuu wa chama hicho, Grace Shsba. Katikati ni Kamishna Rose.
 Michelle kutoka Rwanda akifurahi baada ya kukabidhiwa cheti
 Kiongozi wa Girl Guides kutoka Madagascar akipokea cheti
 Katibu wa TGGA Mkoa wa Lindi, akipokea cheti
 Kiongozi kutoka Tanga, akipokea cheti
 Twarhiya Hussein kutoka Lindi  mtoto pekee aliyehitimu mafunzo hayo na kufanya vizuri, akipokea cheti cha shukrani kutoka kwa Katibu Mkuu wa TGGA, Grace Shaba.

 Rachel Baganyila kutoka Uganda akifurahi kupokea cheti
 Ni wakati wa kucheza ngoma