Friday, October 5, 2012

Prof. Majimarefu, Nundu wapigwa mweleka

ALIYEKUWA Waziri wa Uchukuzi na Mbunge wa Jimbo la Tanga, Omari Nundu, amebwagwa kwenye kinyang’anyiro cha ujumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC). Katika uchaguzi huo, Nundu aliambulia kura 127 kati ya kura 1,175 zilizopigwa.

Nundu ameangushwa na mpinzani wake mkubwa wa siasa, ambaye aliwahi kuwa Meya wa Jiji la Tanga, Salim Kassim Kisauji, aliyeshinda kwa kupata kura 514. Kura hizo, zilipigwa mara mbili, baada ya awamu ya kwanza kukaribiana kwa karibu na Saumu Bendera, aliyepigiwa kura 446.


KOROGWE VIJIJINI


Habari kutoka Korogwe Vijijini, zinasema, Mbunge wa jimbo hilo, Stephen Ngonyani maarufu (Profesa Majimarefu), ameangukia pua, baada ya kushindwa na mpinzani wake, mchumi Dk. Edmund Mndolwa.

No comments: