Thursday, October 18, 2012

FID Q NA JUX WAACHA VIBE LA TIGO FIESTA MUSOMA

 Wasanii Fid Q na Jux usiku wa kuamkia jana waliacha alama ya Vibe la Tigo Fiesta  kwenye uwanja wa Karume mjini Musoma.

Wasanii hao kwa wakati tofauti wakiwa kwenye steji waliweza kuteka hisia za mashabiki waliofurika uwanjani hapo. Msanii Fid Q ndiye aliyefungua pazia la Tigo Fiesta mjini Musoma mkoani Mara, Kwa mkoa huo wasanii wanaopendwa zaidi ni wa mtindo wa kufokafoka (Hip Hop) ndipo Fid Q alipopewa jukumu la kuanza na kuamsha shangwe kubwa na hasa alipomaliza kwa wimbo wake ujulikanao kama FRESH.
Nae Juma Jux ambaye ni "Fundi" wa nyimbo Laini aliweza kuwaimbisha mashabiki mwanzo hadi mwisho aliposhuka kwenye jukwaa hilo kwa nyimbo zake JUU, ZAIDI na UTANIUWA na nyingine nyingi kwa kweli huyu ndio msanii aliyeweza kuimba na mashabiki kwa pamoja.

Tamasha hilo linatarajiwa kuendelea mjini Muleba ijumaa hii kwenye uwanja wa Zimbihire.
Msanii Fareed Kubanda maarufu kama Fid Q akiwa kwenye jukwaa la Tamasha la Tigo Fiesta Vibe Kama Lote lililofanyika uwanja wa Karume mjini Musoma usiku wa kuamkia jumatatu.






No comments: