Monday, October 8, 2012

sumaye alonga

      Waziri mkuu wa jamhuri ya muungano wa tanzania bw Fredrick sumaye amesema chama cha mapinduzi kimetawaliwa na rushwa katika jumuhiya zake mbalimbali unaofanyika nchi nzima.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini dar es salam bw sumaye amesema moja ya mambo yaliyomfanya ashindwe katika uchaguzi wa kamati ya NEC huko hanan ni hila na ruswha zilizotawala katika uchaguzi huo ambao mpinzani wake mh Marry nagu alitangazwa kuwa mshindi katika uchaguzi huo.

   Katika hatua nyingine bw sumaye amekanusha uvumi uliokuwa ukienezwa mitaani kuwa baada ya ya kuanguka katika uchaguzi huo ameingia katika mazungumzo na chama cha democrasia na maendeleo chadema  na kudai kuwa yeye ni mwanachama hai wa CCM na hawezzi kukihama chama hicho kwa kushindwa katika uchaguzi

 Bw Sumaye ameongeza kuwa kushindwa kwake katika uchaguzi huo ni moja kati ya changamoyo na inamfanya akae chini na kujiandaa upya na ushindani wa kisiasa uliopo hivi sasa

No comments: