Monday, October 1, 2012

Wasanii Watakaopanda Jukwaa la Tigo Fiesta Wahudumia Wateja kwenye Duka la Tigo mjini Moshi

Msanii Chin Beez akitoa hiduma kwa wateja walioenda kupata huduma ndani ya Duka la Tigo lililopo barabara ya Mawenzi mjini Moshi leo.

Msanii, Dogo Janjaroo akigawa vipeperushi kwa wateja ndani ya Duka.


Msanii Rose Ree akisaidiana na mtoa Huduma wa  Duka laTigo barabara ya Mawenzi mjini Moshi, Felister Tarimo leo mara baada ya wasanii kutembelea Duka hilo.

Msanii Richie Mavoko akisaidia kutoa Huduma kwa mteja wa Tigo Pesa, Bi. Gloria Mushi kwenye Duka la Tigo lililopo barabara ya Mawenzi mjini Moshi.

Msanii Chin  Beez akimkabidhi simu aina ya Tecno R6 na Tiketi ya kwenda kushuhudia Tamasha la Tigo Fiesta Vibe Kama Lote mteja wa Tigo, Lole Kway. Ndani ya msimu huu wa Tigo Fiesta wateja wanaoenda kupata huduma kwenye maduka wanapata zawadi mbalimbali.


Msanii atakaye uwakilisha mkoa Kilimanjaro kwenye fainali za Tigo Fiesta Supa Nyota 2018, Samson Msweta maarufu kama Samson Classic akiimba kwa staili ya kufokafoka kwenye kinyang'anyiro cha kumpata mwakilishi huo leo kwenye viwanja vya Hugo.

Meza ya Majaji ikiongozwa na Adam Mchomvu(katikati) na kulia, Joh Makini na kushoto ni Evans Lyatuu toka Moshi Fm kwenye kinyang'anyiro cha kumpata mwakilishi wa Tigo Fiesta Supa Nyota toka mkoa wa Kilimanjaro leo.

No comments: