Tuesday, November 13, 2012

RIPOTI KAMILI YA UCHSGUZI WA CCM DODOMA HII HAPA



Mwenyekiti
Kura zilizopigwa             2397
Kura zilizoharibika           0
Kura za HALli 2397

Makamu wa Tanzania Bara
Kura zilizopigwa             2397
Kura zilizoharibika           0
Kura za HALli                 2397

Malamu wa Zanzibar
Kura zilizopigwa             2397
Kura zilizoharibika           0
Kura za HALli 2397




WAKATI matokeo ya Ujumbe wa Halmashauri Kuu ya  CCM (Nec), yakiwa yamevuja baadhi ya wapambe wa wagombea walioshinda  wameanza kusherehekea, huku wengine wakitambiana.

Hata hivyo, matokeo hayo yamekuwa machungu kwa baadhi ya vigogo walioanguka wakiwamo mawaziri, wabunge na watu maarufu.

Mwenyekiti  wa CCM, Rais Jakaya Kikwete anatarajiwa kuunda sekretarieti mpya baada  ya uchaguzi wa mwenyekiti na makamu mwenyekiti Bara na Zanzibar  utakaofanyika leo.

Kwa upande wa Zanzibar,

Kura zilizopigwa             2268
Kura zilizoharibika           55
Kura za HALli                 2213
matokeo hayo  yanaonyesha kuwa walioshinda ni pamoja na Mbunge wa Uzini, Mohamed Seif  Khatib; Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Hussein Ali Mwinyi 1576, Waziri  wa Fedha Zanzibar, Omar Yussuf Mzee, Abdulhakim Chasama na  Waziri wa  Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Shamsi Vuai Nahodha 1603.

Wengine   ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan 1525, Khadija  Hassan Aboud 1625, Bhaguanji Mansuria, Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na  Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa  1850 na Khamis Mbeto.


Watu maarufu  walioangukia pua katika uchaguzi huo ni Naibu Waziri wa Ushirikiano wa  Afrika Mashariki, Dk Abdallah Juma Sadallah, mtoto wa Rais Mstaafu,  Abdallah Mwinyi ambaye pia ni Mbunge wa Afrika Mashariki, Mbunge wa Viti  Maalumu, Kidawa Salehe na Naibu Waziri wa Fedha wa zamani, Abdisalaam  Issa Khatib.

Walioshinda Bara

Kura Zilizopigwa    2389
Kura Zilizoharibika  52
Kura halali            2337

Majina ya wajumbe wa Nec  walioshinda bara na kura walizopata katika mabano ni Waziri wa Nchi  Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Stephen Wassira aliyeongoza kundi  hilo kwa kupata kura 2,135, Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na  Teknolojia, January Makamba (2,093), Mwekahazina wa CCM, Mwigulu Nchemba  (2,012), na Katibu wa UVCCM, Martine Shigela (1,824).

Wengine ni  Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Uratibu na Bunge), William  Lukuvi (1,805), Waziri wa Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa, Bernard  Membe (1,455), Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Mathayo David  Mathayo (1,414), Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Jackson Msome (1,207), Katibu  Mkuu wa CCM, Wilson Mukama (1,174) pamoja na Waziri wa Habari,  Utamaduni, Vijana  na Michezo, Fenela Mukangara (984).

Wakati  walioshinda Bara na wapambe wao wakitambiana, majina makubwa  yaliyoanguka katika uchaguzi huo ni pamoja ni Mbunge wa Afrika  Mashariki, Shy-Rose Bhanji, Mbunge wa Nkenge, Assumpter Mshama, Richard  Hiza Tambwe na Mbunge wa zamani wa Muleba Kaskazini, Ruth Msafiri.

No comments: