Tuesday, March 12, 2013

WATEJA WATAHADHARISHWA WIZI WA MITANDAO YA SIMU

02 af8ba

Mkuu wa Wilaya ya Mafia Sauda Mtondoo akitoa hutuba wakati wa Semina ya Majukumu ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA)Kanda ya Mashariki  iliyofanyika katika Wilaya yake ya Mafia,semina hiyo ilikuwa na  lengo la kutoa elimu  kwa wannchi wa Wilaya hiyo juu ya Haki na wajibu wa watumiaji wa huduma za Mawasiliano, katikati ni Mkurugenzi wa Watumiaji na watoa huduma za Mawasiliano Dk. Raymond Mfungahema,(Kulia ) Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia Mohamed Kimbule.


 

MAMLAKA ya Mawasiliano nchini, kanda  ya mashariki imetoa rai kwa watumiaji wa mitandao ya  simu za mkononi  kuwa macho na wizi unaofanywa na watu wenye  nia ya kujipatia fedha kwa njia ya  udanganyifu, ambapo  idadi kubwa ya wateja wa  simu wamejikuta wakilalamikia  wizi huo.

Mojawapo mwa udanganyifu ni pamoja na mmiliki wa simu kutumiwa ujumbe unahitaji kutuma fedha kwa ajili ya kulipia gharama za huduma kwa njia mtandao ili hali anayetumiwa fedha  hizo hafahamiki.

Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Watumiaji na watoa huduma za Mawasiliano Dk. Raymond Mfungahema wakati alipokuwa akitoa mada  ya kazi za Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA)   kwa viongozi mbalimbali wa Halmashauri ya Wilaya ya Mfia waliohudhuria katika Semina ya Majukumu ya Mamlaka ya Mawasiliano Kanda ya Masharaiki

 Afisa Utumishi Mkuu,Esuvatie Masinga katika  Semina   ya Majukumu ya Mamlaka ya Mawasiliano Kanda  ya Mashariki, iliyofanyika kisiwani Mafia.

Semina  hiyo iliyofanyika Machi 7a mwaka huu  iliwashirikisha wadau mbalimbalimbali wa mawasiliano  wilayani Mafia, wakiwemo watendaji wa  serikali  wa ngazi ya kitongoji, kata na tarafa na wilaya.

Katika semina hiyo iliyohudhuriwa pia na Mkuu wa Wilaya Mafia, Sauda Mtondoo ambaye ndiye aliyekuwa mgeni rasmi,Masinga  alisema, wizi wa mitandao ya simu ni changamoto iliyo mbele ya wateja ambayo inaweza ikakabiliwa kama kila mmoja atakuwa na ufahamu  wa kubaini  ujanja na mbinu  zinazofanywa na wajanja wachache.

Alisema ili kukabiliana na mbinu na ujanja wa wachache hao, wamiliki wa simu za mkononi wanatakiwa kuwa macho ujumbe wowote  unaozungumzia  utumaji wa fedha iwe kwa njia ya ujumbe mfupi ama mawasiliano ya moja kwa ya simu wa watu wasiowajua.

Amesema,wateja wengi wamekuwa wakitumiwa  ujumbe unaowataka watume fedha kwa watu wasiowajuwa  wakiamini kuwa wanatuma fedha hizo kwa makampuni ya  simu, jambo ambalo si kweli, kwani makampuni yote ya  simu yana namba zao za utambulisho  pindi wanapoendesha zoezi lolote la kihalali.

"Utakuta mmiliki wa simu ya mkononi  anatumiwa ujumbe  unaomtaka atume kiasi cha fedha kwa mtu asiyemjua, huku asitambue anatuma  fedha  hizo kwa ajili ya kulipia  huduma gani. Hili ni tatizo lililo katika  changamoto inayohitaji wateja kubaini aina hii ya wizi  kwa njia ya mitandao ya simu" alisema Masinga.

Alisema, wateja wa simu wana wajibu wa kubaini ujanja wa watu wachache kwa kutilia mashaka ujumbe ama simu  yoyote inayoelekezwa kwao na inayohitaji  fedha kwa kuchukua  hatua ya kuwasiliana na makampuni ya  simu  husika kubaini kama kuna kuna mahitaji ya namna hiyo.

Katika  hotuba yake, Mkuu wa Wilaya Mafia, Sauda Mtondoo aliiomba  TCRA kutilia mkazo suala la uelimishaji  umma pindi  kunapotokea changamoto  za matumizi ya huduma mbalimbali zilizo chini ya mamlaka  ili kuwaongezea uelewa watumiaji.

Alisema, elimu  kwa umma juu ya huduma ngeni inawasaidia kuwaondolea usumbufu wateja  hivyo kwenda na kasi ya utandawazi na kuwaondolea usumbufu  ambao unaweza ukawapa mwanya wajanja  wachache kunufaika.

Aidha alipongeza  hatua ya TCRA kutoa elimu ya matumizi ya ving'amuzi kwa muda mwafaka, jambo lililosaidia  kuwaondolea wateja usumbufu pindi mamlaka hiyo ilipotangaza hatua ya Tanzania  kuacha kuanza kutumia  mfumo wa  kidijitali kwa baadhi ya mikoa  nchini.

"Ni jambo la kufurahisha kwamba TCRA imetoa elimu  kwa umma kuhusu namna ya kuweka antena hizo ili picha ziweze kuonekana  katika maana halisi ya dijitali.Vilevile  faraja kusikia kuwa mamlaka inawasiliana na  watoa  huduma za kurusha matangazo ya dijitali ili waweke vizuri mitambo yao na kuongeza mitambo kule ambako haipo ili matangazo yawafikie watazamaji wengi" ilisema Mkuu  huyo wa wilaya.

Pia aliitaka mamlaka kuyabana makampuni ya mawasiliano ya simu  inayobuni utaratibu wa kujipatia fedha kwa njia za kuwataka watumiaji wa simu za mkononi kuingia katika utumaji wa  fedha kwa njia ya ujumbe mfupi ili hali huduma hiyo siyo lazika kwa wateja.

Alisema hatua ya watumiaji kukatwa fedha kwa  huduma isiyo  ya lazima humuongezea mzigo  mteja na kuwayafaidisha makampuni ya simu jambo  linazua manung’uniko  yasiyo  ya lazima.

Aliitaja mfano wa huduma  hizo za kuchangia fedha ni pamoja na nyimbo za miito ya simu ambayo haina ulazima kwa mteja hivyo kuwaagiza wachangie  bila ridhaa ya  mteja wa simu ya mkononi ni hatua  inayowaongezea mzigo wamiliki wa  simu  za mkononi.

Kwa upande mwingine washiriki wa semina hiyo walipata mafunzo ya mfumo wa anuani za makazi na Posta Kodi iliyotolewa na Patrice Lumumba  ambaye aliwataka wananchi wa wialya hiyo kuwa makini na kujua anuni za makazi yao.

HABARI KWA HISANI YA MJENGWA BLOG

No comments: