Monday, July 1, 2013

ZIARA YA OBAMA KUANDAMANA NI USHAMBA --MKUU WA MKOA WA DAR ES SALAAM AMESEMA HAYO

Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam Mhe,Meck Sadick alipokuwa akizungumza katika kipindi kilichokuwa kikionyeshwa Live na Televishion ya Taifa  (TBC ) alisema kuwa wote wanaopanga kuandamana leo kwanza haitaruhisiwa na pia kuandamana ni Ushamba aliyasema hayo pale alipo ulizwa swali na Mtangazaji aliekuwa anamfanyia mahojiano kuhusu Maandalizi ya kumpokea Rais wa Marekani Barrac Obama na njia ambazo atapitia rais huyo kipindi atakacho kuwepo nchini kwa siku mbili.Swali lilikuwa hivi Mheshimiwa Mkuu wa mkoa je unataarifa zozote au kama kuna maombi ambayo yamekufikia kwamba kuna watu ama vikundi vinavyotaka kuandamana kama walivyofanya Waandamanaji Afrika kusini majibu ya mkuu huyo wa mkoa yalikuwa "Kwanza niseme tu Kuandamana ni Ushamba na kwa nini mtu aandamane wakati wa ziara ya Rais Obama" akaendelea kwa kusema "Maandamano yeyote yale kimsingi huwa ayana maana yeyote ile kwa sababu hata ukiandamana haitakusaidia zaidi ya kukupotezea mda sisi tunatoa wito kama kuna watu wenye nia hiyo tunawaomba waache na wajitokeze tu kumpokea mgeni kwa Amani lakini tukiona kunaviashilia vyovyote vya maandamano tutawakamata".Rais Obama anatarajiwa kufika majira ya saa 8:40 mchana na Barabara atakazopitia wakati akitoka uwanja wa Ndege zinatarajiwa kufungwa kuanzia saa 6:30 mchana.

No comments: