Thursday, July 4, 2013

LULU ALIVYOFUNGUKA KUHUSU YEYE NA KANUMBA



 
        Kwa mara ya kwanza muigizaji wa filamu, Elizabeth Michael aka Lulu jana alifanya interview ya kwanza tangu atoke gerezani January mwaka huu. Lulu aliye na muonekano wa ‘udada’ zaidi alihojiwa jana kwenye kipindi cha Take One cha Clouds TV kinachoendeshwa na Zamaradi Mketema.
Ifuatayo ni sehemu ya maswali aliyokuwa akiuliza mwanadada LULU na mtangazaji huyo.
 
                          Mipango yako ya usanii niaje?
      Nazindua filamu yangu hivi karibuni inaitwa ‘foolish age’ chini ya kampuni ya prime promotions ambao ndio wanani- manage kwa sasa
 
                  Kuna tetesi kuwa kuna bwana alikudaka ulivyotoka jela na kukupa gari na nyumba, vipi ni kweli?
(Huku akicheka) Tatizo sisi watanzania tuna dhana kuwa ukiona kuwa mwanamake kafanikiwa kuna mwanaume, ila ukweli hamna mtu yoyote aliyenifanyia kitu isipokuwa kampuni yangu ya ndo imenisadia kwa mambo yote hayo.
 
           Kuna movie umefanya tangu utoke?
Yap, inaitwa mapenzi ya Mungu,
 
Umemshirikisha mama kanumba?
Yeah, saivi tupo kama familia, na kuna vitu vingi sana tumeviongelea pale
 
Ukikaa na mama kanumba humkumbuki kanumba?
Aaaah, namkumbuka
 
Unamiss nini kwake?
Mmmh, busara zake
 
Mliwezaje kuweka siri ya mapenzi yenu kwa muda mrefu hivyo?
Tulikubalina, siunajua tena mapenzi ni makubaliano na hatukupenda watu wengi wajue ndio maana
 
            Mlikaa sana kwenye uhusiano?
Mmmh, (Huku akisita) yaah, ila unajua sipendi sana kuyaongelea haya mambo bado, ila ya tulikaa muda mrefu.
 
                    Plan zako ni nini?
Kukuza talent yangu zaidi, na nataka kuwa icon katika tasnia yangu unajua tukiona Geneviev tunajuma ni mnigeria, nataka kuwa kama hivyo nab ado najipanga ili nianze hiyo safari.
 
                  Kwanini ulinenepa ullipokuwa jela?
Labda  kwasababau nilimuachia Mungu kila kitu. Na ukweli jela kumenifanya nimjue Mungu vizuri na nikajikuta nina amani
 
                  Mahusiano yako na kanumba yalianzaje?
Nomba nisiongelee hilo jambo kwa sasa, ila nitaongelea siku ikifika maana nikiongelea sitamaliza. Naomba niliongelee pale nitakapokuwa tayari.
Hayo ni baadhi ya maswali aliyokuwa akiulizwa mwanadada lulu na Zamaradi Mketema.

No comments: