Thursday, August 29, 2013

MAJAMBAZI WAJICHUKULIA PESA BENK KIRAHISI DAR,MLINZI ALIKUWA HANA HATA KIRUNGU,KOVA AKASIRIKA ATANGAZA MILION 100 ATAKAYEWALETA,WENGINE WAMCHOMA DEREVA TAX KISU USIKU HADI KUFA


 

           Watu wanaosadikiwa n majambazi leo jijini dar es salaam wamevamia benk ya HABIBU AFRICAN BENK ILIYOPO KARIAKOO JIJNI DAR ES SALAAM  na kufanikiwa kupora zaidi ya bilion moja ya kitanzania huku waakiondoka kimya kimya bila tatizo lolote

Akidhibitisha kutokea kwa tukio hilo mbele ya waandishi wa habari jijini dar kamishna wa kamda maalum ya dar es salaam SULEMAN KOVA amesema kuwa tukio hilo limetokea majira ya saa tatu aubuhi ambapo majambazi hao waliingia kama wateja na kisha kuanza kuwaweka wafanyakazi wa benki hiyo chini ya ulinzi na kisha kupora fedha zote katika benk hiyo

Amesema kuwa baada ya polisi kufika katika eneo hilo wamegundua kuna mazingira ya uzembe wa uongozi wa benki hiyo ikiwemo mlinzi aliyekuwa akilinda alikuwa hana silaha yoyote hata rungu ya kujihami kitu ambacho amesema kuwa ni makosa makubwa sana,aidha amesema kuwa benki hiyo haikuwa na ulinzi wa uhakkika ikiwemo kamera za cctv ambazo amesema hazikuwepo.

Aidha amesema kuwa jeshi la polisi linamshikilia meneja wa benki hiyo  DANIEL MATEMBA pamoja na mlinzi  ENDRU PETER kutokana na kuonekana kuwa wamepanga njama za tukio hilo kutokana na wao kutokuhangaika kuwazuia wezi hao ambapo amesema kuwa jeshi linawahoji kujua kama wanahusika ama la.

Aidha katika tukio jingine usiku wa kuamkia leo poisi imekamata watu wanne kwa tuhuma za kumchoma dereva tax kisu kifuani hadi kufa maeneo ya OBAMA ROAD jjini dar es salaam

 KAMISHNA KOVA AMMETANGAZA HALI HATARI HUKU AKITOA MILLION 100 KWA YEYOTE ATAKEYELETA TAAIFA ZA WAHALIFU HAO

No comments: