Thursday, November 28, 2013

MAKAMU WA RAISI AFUNGUA MADHIMISHO YA MIAKA 10 YA TCRA,ATOA NENO


SERIKALI imeahidi kuendelea kutoa ushirikiano na mamlaka ya mawasiliano Tanzania  TCRA ili kuiwezesha mamlaka hiyo iweze kufikia malengo yaliyokusudiwa .

Rai hiyo imetolewa na Makamu wa raisi wa jumhuri ya muungano wa Tanzania Mheshimiwa Mohammed Gharib Bilali katika uzinduzi wa maadhimisho ya miaka 10 ya mamlaka ya mawasiliano Tanzania TCRA.

Katika kipindi cha miaka kumi mamlaka ya mawasiliano TCRA imelifanya Taifa kupiga hatua katika maendeleo kiuchumi.

Pamoja na hayo Bilali amezitaka kampuni za mawasiliano zisambaze huduma zake zote katika maeneo yote hapa nchini kwani serikali kupitia mfuko wa kusambaza huduma za mawasiliano watahakikisha wanatoa huduma wanao nufaika na mfuko huo kwa manufaa ya wananchi.

Hata hivyo ametoa wito kwa makampuni kutoa fursa ya mafunzo na elimu ya kisasa ya mifumo mipya ya mawasiliano kwa wafanyakazi wake ili waendane na kasi ya mabadiliko ya kiteknolojia.
mwishooo

No comments: