Wednesday, November 6, 2013

SERIKALI YATAKIWA KUWA WAZI JUU YA MATUMIZI YA KODI ZA WANANCHI

Na Karoli Vinsent

           SHIRIKA lisilo la Kiserikali la Action Aids Linalohusika na maswala ya Utafiti ndani na nje ya Tanzania Limetaka Serikali ya Tanzania kuwaambia watanzania jinsi ya matumizi ya kodi wanazokusanya kutoka kwa wananchi.

               Hayo yalisemwa leo jijini Dar es salaam na Mkurugenzi wa tasisi hiyo, Wamilika Gama alitaka Serikali  ya Tanzania kuwaambia wananchi juu ya mtumizi ya Kodi wanayokusanya kutoka kwa wananchi.

         “Tunaiomba serikali watuambi sisi wananchi matumizi ya kodi  wanayokusanya kutoka kwa wananchi maana tunahakia ya kuuliza kwasababu tunaoa kodi atujui zinafanya nn maana kodi nyingi zinakusanywa kilia kona ila sisi wananchi awatuambii wanafanyia nn?”alihoji Gama

         Vilevile mkurugenzi huyo alishangaa wananchi watanzania kukaa kimya kuhusu suala hili la kodi
“kuna kodi zinakusanywa kwenye vijiji kule ila akuan wananchi anayehoji kodi hizi zinafanya nn,na leo mwananchi akihoji ataonekana mtu wa ajabu sana,lakini anahaki ya kuhoji kama mwananchi kwakuwa yeye ndio ,mlengwa mkubwa”alimalizia Gama

            Kwa upande wake Ofisa Mipango wa taasisi hiyo Stivin Alocye,naye aliitaka serikali ya Tanzania kuacha kumtwisha mzigo mwananchi kwenye kodi badara yake wangeegemea zaidi kwenye mashirika zaidi na taasisi binafsi pamoja na makampuni ya simu amayo yamekuwa yakipata faida nyingi huku Serikali haiambulii kitu

NDUGU MSOMAJI TUNAOMBA RADHI KWA HABARI AMBAYO HAINA PICHA

No comments: