Tuesday, December 10, 2013

MAMA NYERERE KUHUDHURIA MAZISHI YA MANDELA



Maria Nyerere ambaye ni mke wa aliyekuwa rais wa kwanza nchini Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, amesema Nelson Mandela ataendelea kukumbukwa kwa moyo wake wa kusamehe na kumtaja kwamba alikuwa ni zawadi ya dunia katika kuleta upendo na maridhiano.
Uhusiano kati ya familia ya Mwalimu Nyerere na ile ya Mzee Nelson Mandela umekuwa ni wa karibu kiasi kwamba familia yake inajiandaa kwenda kuhudhuria katika mazishi yatakayofanyika tarehe 15 mwezi huu.
Source:BBC SWAHILI

No comments: