Monday, December 2, 2013

MAMIA WAFURIKA KUSHUHUDIA BONANZA LA WAZI LA MASUMBWI NDANI YA KITUO CHA MABASI CHA MWENGE .

 Hawa ni wazee wa zamani ambao sasa ni walimu wa mchezo wa Ngumi, Wakati wao ndio walikuwa Mabondia Wakubwa
Wapigangoma wa Kikundi cha Ngoma ya Mchiriku cha Jagwa wakitumbuiza katika Bonanza la Masumbwi 
endelea chini hapo------
 Mwimbaji wa Kundi la Jagwa akitumbuiza vilivyo katika Bonanza hilo la Masumbwi.
 Afisa habari wa Shirikisho la Ngumi Tanzania Salim Mwiduka akitoa ufafanuzi wa jambo wakati wa Bonanza la wazi la ngumi.
 Mwenyeji wa Maandalizi ya Bonanza la Ngumi Kessy Juma akiwa anafungua Bonanza hilo.
 Mwenyekiti wa kamati ya Tuzo za ngumi Said Masanga akielezea juu ya Tuzo hizo za ngumi.
 Mjumbe wa Shirikisho la Ngumi wanawake Bi. Aisha George Vaniatis akiwa anafuatilia mpambano

Kulia ni Mwalimu mkongwe wa Mchezo wa ngumi bwana Rashid au anafahamika kwa jina la 
Super D

 Mpambano wa kwanza kati ya Gervas Rogiansion aliyevaa gloves nyekundu akipambana vikali na mpinzani wake John Christian aliyevaa Gloves za rangi ya bluu , ambapo John Christian aliibuka mshindi kwa Makonde mawili kwa moja.
 Umati wa watu waliojitokeza kutazama Bonanza la wazi la Ngumi katika kituo cha mabasi cha Mwenge
 Mashabiki wa Ndondi wakishangilia
 Mpambano wa pili  kati ya Haruna Swanga  aliyevaa gloves nyekundu aliyepambana vikali na na mpinzani wake Kulwa Makenzi  aliyevaa Gloves za rangi ya bluu , ambapo Haruna Swanga aliibuka mshindi kwa kumtandika mpinzani wake makonde matatu kwa sifuli.

 Mpambano wa tatu  kati ya George Costantino   aliyevaa gloves nyekundu aliyepambana vikali na na mpinzani wake Hamadi Furahisha   aliyevaa Gloves za rangi ya bluu , ambapo Hamadi Furahisha  aliibuka mshindi kwa kumtandika mpinzani wake makonde mawili kwa moja.
 Leonard Machichi aliyevaa gloves nyekundu akiwa anajikimu kukwepa ngumi kutoka kwa mpinzani wake Abuu Bakari wakati wa mpambano huo
 Abuu Bakari akipokea kipigo cha nguvu kutoka kwa mpinzani wake Leonard .. ambapo hali ilikuwa mbaya sana kwa Abuu
 Mwamuzi wa Mpambano huo Michael Mwamkenja akisimamisha mpambano huo katika Mzunguko wa pili baada ya Bondia Abuu kunyosha mikono juu ishara ya kushindwa .
 Leonard Machichi akitangazwa mshindi wa pambano hilo kali ambalo wanaliita RDT
 Makamu wa Raisi mpya wa Shirikisho la Ngumi za Ridhaa Tanzania Lukelo Anderson au Man Power akiwa anatoa Neno la Shukurani Mara baada ya mpambano huo kuisha.
 Kutoka Kushoto ni Bi. Zuena Kipingu ambaye ni Mjumbe wa Maendeleo ya Vijana na wachezaji katika Shirikisho la ngumi za Ridhaa Tanzania,Mutayoba Rwakatale Katibu wa maandalizi hayo, na Bondia Haruna Swanga. 
Picha zote na Dar es salaam yetu.


No comments: