NAIBU Waziri
wa Habari na Michezo Amosi Makala amepingana hadharani Rais Jakaya kikwete kuhusu sakata la
kulifungia Gazeti la mwanahalisi.
Hayo
yaligundulika wiki hii katika vikao vya bunge vinavyoendelea mkoani Dodoma
katika kipindi cha maswali na majibu,ambapo mbunge wa Mbinga Mashariki kapteini
John Komba(CCM) alipokuwa anauliza swali kuhusu utaratibu uliotumiwa na
serikali katika kuyafungia magazeti ya mtanzania pamoja mwanahalisi.
“kwanini Serikali ilitumia nguvu katika kuyafungia
magazeti ya Mwanahalisi pamoja na Mtanzania wakati tayari serikali ilikuwa
imeshawaonya wahariri hao na hao
wahariri wa magazeti hayo wakakubali kosa na kuomba Radhi”aliuliza Komba
ENDELEA HAPO--------
Naibu Waziri
wa Habari na Michezo Amosi Makala alipokuwa
anajibu swali hilo ambalo likuwa tofauti na mkubwa wake wa kazi Rais Kikwete
ambapo alisema Serikali haiku kurupuka
katika kulifungia Gazeti la
Mwanahalisi kwani Makala nyingi zilizokuwa zimeandikwa kwenge hili gazeti hilo
zilikuwa za kichochezi.
“Serikali
haikukurupuka kufungia gazeti hilo kwani makala nyingi zilikuwa za kichochozezi
kwa mfano makala ilyokuwa inasema Waziri Sophia Simba ni Muhuni na nyingine
Zilikuwa zinawashutumu baadhi Maofisa wa Serikali kuhusika na utekaji
unaoendelea hapa nchini”alizidi kufafanua Makala
Uchunguzi
uliofanywa na Habari24 umegundua majibu ya
Naibu Waziri huyo ni Tofauti na majibu aliyatoa Rais Jakaya Kikwete alipokuwa kwenye Mkutano
na waandishi Nchini Ethopia ambapo, alisema watu wanahoji na kuishutumu
Serikali yake kulifungia gazeti la mwanahalisi wakati wamesahau Gazeti hilo
lilikuwa linaandika Habari ambazo zinawataka wanajeshi watanzania kuhasi serikali yao habari hiyo iliandikwa na Gazeti
la Serikali .
Wachambuzi
wa Masuala ya Habari waliozungumza na Habari24 walisema utofauti huo wa majibu
hayo. Unaonyesha kuwa Serikali haikuwa na hoja wala mantiki yeyote katika
kulifungua Gazeti hilo kwani hakuna uthibitisho wa ukweli wowote kuwa Gazeti
hilo lilikuwa limeandika habari za jeshi kuasi Serikali,bali ni ubabe ambao
umekuwa unafanywa serikali katika kuyafungia magazeti hilo.
Ripoti
mbalimbali Duniani ikiwemo ya Shirikisho la waandishi habari Duniani
(CPJ)ililiweka Tanzania sio Sehemu Salama kwa waandishi wa Habari, katika
ripoti hiyo kuna vipengele ambavyo vinaishutumu serikali ya Tanzania kwa kushindwa kuwapa ulinzi
Waandishi wa Habari katika majukumu yao ya kila siku na ripoti hiyo ikaonyesha
waandishi wa habari wa Tanzania wameacha kuandika habari za uchunguzi kwa
kuhofia kufungiwa gazeti magazeti yao pamoja na usalama wa maisha yao.
No comments:
Post a Comment