Wednesday, December 4, 2013

UFISADI MKUBWA,OFISI YA WAZIRI MKUU YAINGIA KWENYE KASHFA NZITO,MILION MBILI ZAIBIWA HUKO MBARALI



Na Karoli Vinsent
     Ofisi ya Waziri Mkuu (Tamisemi) imeingia kwenye kashfa ya ufisadi wa Sh2.3 mil za Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali baada ya viongozi wa CCM wilaya hiyo kuitaja waziwazi kwamba wanahusika katika kashfa hiyo ilitokea mwaka 2011/12.
  ENDELEA HAPO------


     Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Mbarali, Mathayo Mwangomo alimweleza Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana aliyetembelea wilaya hiyo jana kwamba Ofisi ya Waziri Mkuu ni moja ya kikwazo kitakachosababisha CCM iwe na hali ngumu wilayani humu kutokana na kuchelewesha kuchukua hatua za wahusika wa ufisadi huo.

       Mwangomo alisema zipo dalili kwamba fedha hizo zilichakachuliwa kwa ushirikiano wa viongozi waliokuwapo mwaka huo na kwamba mpaka sasa hakuna hatua zilizochukuliwa.

      Suala la ufisadi Mbarali liliitikisa halmashauri hiyo kwani madiwani sita walishahojiwa kwenye kamati ya maadili ya CCM kwa tuhuma za kushirikiana na watendaji katika kutafuna fedha hizo

    Alisema hoja zote zilizotolewa atazifuatilia kwa karibnu na kwamba lazima zitatuliwe kabla ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwakani,

      Vitendo vya ufisadi ndani ya halmashauri nyingi hapa nchini vimekuwa sana huku Mamlaka zikiwa zinayafumbia macho vitendo hivi.hii imekuja baada ya ripoto za mkaguzi wa fedha CAG kuonyesha ufisadi katika halmashauri nyingi hapa nchini huku zengine zikiwa zimepewa hati chafu kutokana na ufisadi unaoendelea katika halmashauri hizo lakini jambo la kushangaza viongozi ambao wanapelekea ufisadi huwa wanaamishwa kazi kutoka katika halmashauri moja kwenda nyingine,
           
     Duru za kisiasa zinasema kitendo cha kuwahamisha viongozi wanaopelekea ufisadi ni kuficha uhovu na pia ni dalili za kulinda mafisadi hao

No comments: