Friday, January 17, 2014

USHIRIKIANO WA AFRICA MASHARIKI,SITTA AFUNGUNGA LEO,SOMA ALICHOKISEMA MBELE YA WANAHABARI




              Na Karoli Vinsent
       
            WAZIRI wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta amewashushua Nchi washirika wa Afrika mashariki na kusema kamwe Tanzania haiwezi kuyumbishwa  na watu wanaotaka Madaraka.
            
         Hayo ameyasema leo jijini dare s salaam alipokuwa anazungumza na wanahabari ,ambapo Sitta alisema Serikali ya Tanzania haiweza kuharakisha katika kujiunga na nchi za Afrika mashariki mpaka Wananchi wa Tanzania watakaporidhia kujiunga na umoja huo.

              “Hatuwezi kuharakisha kujiunga na umoja huu wakati  huku mambo ya msingi hatuja kubaliana nao kwasababu viongozi wa nchi hizi wanataka kuharakisha kujiunga na umoja huu ili wapate madaraka,lakini sisi hatuwezi tukafosi kujiunga huku mambo ya msingi ambayo yanatunayataka hayajatimiza yanaachwa.Alisema  Samueli Sitta
Vilevile Waziri Sitta alivitaja  vitu vya Msingi ambavyo Vinaifanya Tanzania kutumia busara Kabla kujiunga na umoja huo.
        

                             Kuhusu sarafu moja AMESEMA ---------

Waziri Sitta, alisema  “ kuhusu sarafu Moja Tanzania inaona ni jambo Jema ila Tanzania tupewe mda hadi kufikia Miaka kumi ili tuwe Sarafu moja ili tuwaandae watanzania kisakrojia  na hiyo sarafu moja”alisema Sitta
           KUHUSU SUAL A LA VIZA
            Waziri Sitta,alisema anashangaa sana nchi hizo yaani Kesha na Uganda pamoja na Rwanda kufosi sana suala la kuingia nchi hizi za Afrika Mashariki bila Viza na kusema Utaratibu huo unainyima Tanzania pesa za Utarii
       “Leo nashangaa sana wenzetu hawa wanaharakisha suala la Viza ,sisi tumewaambia Tanzania bado katika kulikubali hili kwani hili jambo litalikosesha Taifa pesa na matokeo yake nchi ya Tanzania kuyumba kiutalii”
          “Mfano leo mgeni akatoka huko ulaya akafikia nchini Kenya na kukata viza ya nchini Kenya harafu akataka kuja Tanzania kwenye Mbuga zetu maana Mgeni huyo atakuja bure kutokana na kukata viza kenya na kutokuwa na Viza na nchi itakosa mapato ya utalii”alisema Sitta
         Vievile Samweli Sitta akalizungumzia Suala la uhalifu na akasema kwa mfumo huu wa kutokuwa na Viza itapelekea uhalifu kuongezeka sana katika nchi hizi kutokana watu wabaya kuingia kirahisi katika nchi hizi kutokana kutokuwa na viza

       “Nataka niseme leo nchi hizi zinaharakisha sana suala hili kwa maslai yao na sisi Tanzania tumeona suala  hili litapeleka uharifu kuongezeka sana kwa mfano Tanzania  leo haipokei mtu kutoka Nchini Somalia bila kuwasiliana na nchi zenye ubalozi wetu kama Ethiopia lakini kwa mfumo huu. kama ziko nchi katika afrika mashariki zinaubarozi wa Somalia na zikampa kibali basi mtu huyo ataingia kirahisi Tanzania”alisema Waziri Sitta

No comments: