Monday, January 13, 2014

VITA YA URAISI 2015 KADINAL PENGO AINGILIA KATI,AKEMEA WANAOTANGAZA NIA MAPEMA



NA Karoli Vinsent

      ASKOFU Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, amekemea wanasiasa wanaojitangaza kuwania uongozi kabla ya wakati na kuweka bayana kwamba, anashukuru kutokuwa mwanasiasa kwa kuwa mwanasiasa mara nyingi akisema ukweli anaweza kupigwa risasi.

ENDELEA-------


       Pengo alitoa kauli huku ikiwa imebaki mwaka mmoja tu kuelekea kwenye Uchaguzi Mkuu mwakani, hayo yalisemwaJumamosi iliyopita jijini Dar es Salaam alipotoa neno la utangulizi wakati wa ufunguzi wa Ibada ya Shukrani iliyoandaliwa na Wanawake Wakatoloki Tanzania (WAWATA), siku ambayo alionyesha wasiwasi wake kuhusu umoja na upendo katika dhamira ya wanaotaka serikali tatu ndani ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

     “Napenda kulisema hili wazi kwamba si kwa sababu mimi ni mwanasiasa... nilishawaeleza tangu zamani siasa na mimi tusingeenda pamoja. Wangekuwa wameshanipiga risasi zamani maana yake mwanasiasa ukisema ukweli huwezi kudumu,” alisema Pengo ambaye alionekana kuzungumza kwa hisia na uchungu.

      Alisema ni hatari kwa mustakabali wa taifa kwa kila mwanachama katika chama chochote kile kuanza kutamka kabla ya chama hakijatamka kuhusu nafasi za kugombea uongozi wa serikali kupitia chama husika.

     Kauli hiyo ya Pengo imekuja siku chache baada ya Waziri mkuu aliyejiuzuru na pia ni Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa, kuonyesha nia iliyojificha, Januari Mosi, mwaka huu nyumbani kwake kwamba anaweza kuwania nafasi ya juu ya uongozi nchini.

     Lowassa alikuwa Waziri Mkuu kabla ya kulazimika kujiuzulu kwa shinikizo la Bunge kutokana na kuhusishwa katika kashfa ya zabuni ya umeme wa dharura, iliyotolewa kinyemela kwa Kampuni ya Richmond Development LLC.

    “Tuombee vyama vyetu vya siasa umoja na upendano, walau ndani ya vyama kama sio chama kwa chama..  hiyo (chama kwa chama) labda inaweza kuwa baadaye lakini ndani ya vyama kuwe na umoja na upendano. Watu katika chama kimoja wangoje chama kinasema nini na kinateua nani wawe wagombea wa uongozi wa taifa letu,” alisema Pengo.

    Akizungumzia kuhusu serikali tatu, alisema kwa sasa mazungumzo na dhamira ya wanaotaka serikali tatu hayatokani na nia njema na upendo bali yanatokana na tofauti na manung’uniko kutoka pande mbili za Muungano, hali inayoashiria kutokuwapo nia njema..
umefika mahala, kiongozi wa kidini anatamka kwenye nyumba ya ibada;  
   
   “  Msiwachague wale wenye kutoa kofia na fulana”. Mwingine anatamka; “ Msiwachague watakaotuletea vita.”  
Katika mifano hiyo miwili ya kauli ni dhahiri, kuwa bila kutaja ni akina nani wenye kutoa  kofia na fulana waumini wameshawajua ni akina nani. Na bila kuwataja hao ‘ watakaotuletea vita’ waumini wameshawajua ni akina nani.  Hayo mawili hayawezekani yakawa ni mafumbo magumu kwa waumini kutoka kwa viongozi wa dini.

      Wachambuzi wa masuala ya kisiasa waliozungumza na Mwandishi wa mtandao wanasema kauli aliyoisema Askofu Pengo ni ya ukweli mtupu kutokana na hari ya vita ya kusaka urais mwaka 2015 ikiwa imshika kasi.
Wachambuzi hao ni John Jambele ambaye kwa upande wake alisema “kitendo cha viongozi  wetu kupita makanisani au misikitini na kuanza kutoa fedha ni sawa kabisa ila tuatashangaa viongozi hawa tena baadaye waibuke na kuanza kugombea urais tutashangaa sana kwani hata mwalimu Nyerere alisema ukiona mtu yeyote anatumia nguvu na kumwaga pesa ila hapate Urais uje hatufai hata kidogo”alisema Jambele

       Duru za kisiasa zinasema Mvutano wa wasaka Urais ndani chama cha Mapinduzi CCM uwenda kikaingia kwenye mgorogoro mzito kutokana na baadhi ya wanachama kuutaka urais kwa udi na uvumba huku wengine wakitumia mamilioni ya pesa ili wapate urais.

No comments: