Wednesday, February 26, 2014

MEYA A DAR ES SALAAM AONYESHA WASIWASI WAKE JUU YA RASIMU YA PILI YA KATIBA

MEYA MASABUR ..

  Mwenyekiti wa jumuia ya serikali za mitaa nchi Didas Masaburi amelalamikia kitendo cha kutojumuishwa kipengele kinacho husiana na serikali za mitaa katika katika rasimu ya katiba mpya inayotarajiwa kujadiliwa hivi karibuni bungeni mjini Dodoma.




          Masaburi ameongeza kuwa wao kama ALAT wanampango wa kukutana na wajumbe wa bunge la katiba pamoja na waziri wa TAMISEMI ili kufikisha malalamiko yao

   Aliongeza kuwa kama kipengele chenye kuhiusisha serikali za mitaa akitowekwa watazunguka nchi nzima ili kufikisha ujumbe kwa wananchi.

     Masaburi alisisitiza kutohusisha serikali za mitaa ni kitendo cha kuwapokonya madaraka wananchi na wao kama ALAT hawatakubaliana na jambo hilo.

      Pia, aliiomba serikali kuigamfano kwenye nchi zingine za Afrika Mashaliki kwa kuweza kugatua madaraka hadi kwenye serikali za mitaa.
        

No comments: