Saturday, March 1, 2014

REPORT MAALUM----ROSTAM AZIZI ARUDI UPYA,SASA AVAMIA GAZETI LA MWANANCHI,APORA WAFANYAKAZI WAHAMIA KWAKE,WAHARIRI MAKINI WA MWANANCHI WAMEACHA KAZI,SASA WAPO TAYARI KWENDA NEW HABARI.SOMA REPORT YOTE HAPA



 
   Na karol vicent   
       
BAADA ya kuwa kimya kwa muda mrefu,mfanyabiashara maarufu Nchini,Rostam Azizi ameanza kujipanga upya kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2015,kwa kuamua kuimarisha kampuni yake ya Magazeti ya New Habari(2006LTD),Huku akingoa kikosi cha wahariri wa Kampuni ya Mwananchi ,mtandao huu umebaini.
          
      Rostam tangu ajiuzulu nyadhifa zake zote hapa nchini amekuwa kimya huku akitajwa kutumia mda mwingi nje ya nchi  kwa ajili ya kuangalia maendeleo ya biashara zake.
      
          Taarifa za kuaminika ambazo mwandishi wa mtandao huu amezipata na pia zimethibitishwa na vyanzo mbalimbali ndani na nje ya kampuni ya Mwananchi ,zinaeleza kuwa Rostam sasa ameanza mikakati mzito wa kuimarisha kampuni yake ya magazeti ya NewHabari na kuivuruga Kampuni ya Mwananchi.

          
   Taarifa,hizo zinasema mpaka wiki iliyopita  watu walikuwa wamethibitisha kuacha kazi na kuchukuliwa na Kampuni ya Rostam ni pamoja na Dennis Msacky ambaye alikuwa Mhariri Mtendaji wa Gazeti la Mwananchi.
     
         Msacky amekuwa akitajwa kama kiungo muhimu cha mafanikio ya Gazeti Mwananchi kabla ya malalamiko ya hivi karibuni kutoka kwa Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Samweli Sitta kumshutumu Mhariri huyo kujiingiza katika Masuala ya Kisiasa.

         Wengine ambao wamekwisha kutoa Barua za kuacha Kazi ni Edwini Mjwahuzi ambaye alikuwa ni Mpiga picha Mkuu wa Kampuni ya Mwananchi na pia huyu naye amekuwa akitajwa kuwa ni kiungo muhimu wa mafanikio ya Gazeti hilo.

           Kwa Mujibu wa vyanzo vyetu vinasema .katika mkakati huo Rostam ameweza kumchukua  mhariri wa Habari wa Mwananchi,Samsoni Mfalila ambaye naye ametajwa kuwa na uwezo mkubwa.

       Taarifa hiyo inazidi kusema kwamba yuko pia mpiga picha  mwingine  Fidelis Felix naye anakwenda kwenye kampuni hiyo na kujiunga na kikosi cha Rostam kutoka Mwananchi.

        Chanzo hicho kinasema Mbali na wahariri hao,pia katika kikosi hicho yumo Meneja usambazaji msaidizi Erasto Matasia  ambaye naye amekabidhi barua ya kuacha kazi kwenye Gazeti la Mwananchi.

       Vyanzo hivyo vinasema mpaka sasa  wahariri hao walikuwa bado hawajaripoti moja kwa moja kwenye kampuni ya New Habari,lakini mwisho wa safari yao ni kwenye kampuni hiyo yenye mako makuu sinza kijiweni.

      Rostam,ambaye alikuwa mbunge wa Igunga alijuzuru ubunge huo na kutokana na kile alichokisema siasa za Tanzania zimejaa siasa Uchwara,Taarifa hizo zinasema sasa wahariri watatu pamoja na Mpiga picha mmoja wanasuburi muda wao waliotoa kampuni ya Mwananchi uweze kukamilika ndipo waondoke.

         Chanzo hicho kinasema kikosi hicho cha wahariri kilichoondoka ni kidogo kwani kunaorodha nyingine ya watu muhimu ya takribani 16 kwenda kwa Rostam,watu hao watatoka kwenye kitengo cha picha,uzalishaji gazeti mitamboni,fedha,chumba cha habari na utengenezaji gazeti(Graphics).

            Rostam ambaye pia anatajwa kwa sasa kununua hisa kwenye kampuni ya Airtel Kenya na ujenzi wa bomba la mafuta kutoka Lamu hadi juba,sudani kusini,anapanga kuifanyia New Habari kuwa kubwa zaidi nchini kuliko Mwananchi.

                      TIDO APAMBANA KUNUSURU JAHAZI
      
       Lakini,katika mkutano wake na wafanyakazi uliofanyika mwanzoni wa wiki  iliyokwisha jana,Mkurugenzi Mtendaji wa MCL.Tido Mhando aliwaasa wafanyakazi waliobaki wasiwe na wasiwasi na wasiwe kama na kutangatanga njia kama wafugaji wanaotafuta malisho.

         Tido ambaye pia aliwananga wanaohama kuwa akiwaita kama Makanjanja wanaotafuta Fedha za Mafisadi,alitangaza haraka kujaza nafasi zilizoachwa wazi na wahariri hao waliondoka.

           Kwa upande wa Mhariri mtendaji wa Mwananchi ilichukuliwa na mhariri kutoka gazeti la michezo la Mwananspoti Frank Sanga iliyoachwa wazi na Msacky huku Reginald Miruko akijaza nafasi ya mhariri wa Habari iliyoachwa wazi na Mfalila.

         Chanzo hicho kilisema kiliongeza na kusema kwamba Tido na Mhariri Mtendaji Mkuu wa Mwananchi,Bakari Machumu wamekuwa wakijipanga kuhakikisha Kampuni hiyo haiyumbi katika kipindi hiki kigumu.

           Taarifa za Kuaminika ambazo Mwandishi wa Mtandao huu amezipata kuwa mkurugenzi huyo wa Mwananchi Tido naye kwa upande wake mkataba wake unakaribia kumalizika na Duru hizo zinasema atarajiwa kwenda Kampuni ya Azam.

                           MSACKY ATAJWA KUENDESHA UASI

       Hata hivyo,hii si mara ya kwanza kwa Mwananchi kukimbiwa na kundi la waandishi wakiongozwa na Msacky,mara ya kwanza ilikuwa mwaka 2007 walipokimbilia kampuni ya Kampuni ya Gurdian.

       Katika kipindi hicho Msacky aliondoka na mahariri mwengine aliyekuwa nguzo ya kampuni hiyo Sakina Datoo lakini, Baadaye msacky alirejea tena Mwananchi na kuacha wafuasi wake (kasoro Mjwahuzi)Gurdian.
   
       Katika hatua Nyingine Mwandishi wa Mtandao huu amezipata kutoka kwa Kampuni ya New Habari ambao ni wachapishaji wa Magazeti ya Mtanzania,Rai nguvu ya hoja.The African,gazeti la michezo la Dimba pamoja na Bigwa,zinasema Uongozi wa Kampuni hiyo teyari umeanza kuwaambiwa waandishi wake ambao wanatoa mchango mdogo katika ufanyaji kazi na wale wenye elimu ndogo wajiaandae kufukuzwa.

         Mwandishi wa Gazeti la Mtanzania ambaye akutaka jina lake litajwe kwenye Mtandao huu kwa kile alichokisema yeye sio msemaji wa Kampuni hiyo alisema kwa sasa kampuni yake imekuwa inaanza kufuatilia ufanyaji kazi wa kila mwandishi na kusema kwa sasa kampuni hiyo itawafukuza kazi na kupunguza waandishi wa habari.

No comments: