Friday, May 30, 2014

JUKATA WATOA TATHMIN YAO JUU YA UCHAGUZI WA MALAWI NA AFRICA YA KUSINI.SOMA HAPA

Mwenyekiti wa JUKATA DEUS KIBAMBA akizungumza na wanahabari mapema leo jijini dar es salaam
        Jukwaa la katiba Tanzania JUKATA leo limetoa tathmini  yake juu ya chaguzi mbili zilizofanyika katika nchi za Malawi na Africa ya kusini mwezi uliopita huku wakionyesha kuipongeza sana nchi ya Africa ya kusini kwa kufanya uchaguzi wa haki na huru tofauti na nchi ya Malawi
        
        Akizungumza leo jijini dare s salaam mwenyekiti wa jukwaa  hilo DEUS KIBAMBA amesema kuwa wao kama jukwaa waliweka kambi katika nchi hizo mbili,kwa lengo la kuangalia uchaguzi huo
Kaimu mwenyekiti wa jukata HEBRON MWAKAGENDA
          KIBAMBA anasema kuwa ni wazi kuwa hali ya nchi hizo mbili kiuchumi ni tofauti sana jambo ambalo pia limechangia kufanya chaguzi zao pia kutofautiana sana,ikiwa ni pamoja na tume ya uchaguzi ya Malawi kuonyesha kuwa haikuwezeshwa kiswasawa katika kusimamia uchaguzi huo jambo ambalo nchini Africa ya kusini halikuwa hivyo.
        
         “Tume ya uchaguzi ya Africa ya kusini imeonyesha kuwajali sana wapiga kura hadi kufikia hatua ya kuwajali walemavu ambao wasingeweza kufika vituoni na kuwafwata walipo ili wapige kura.”amesema KIBAMBA
          
         Kuhusu hamasa ya wananchi ya kupiga kura JUKATA wamesema kuwa wananchi wa Africa ya kusini walikuwa na hamasa sana tofauti na wale wa Malawi jambo ambalo limechangiwa na hamasa pia iliyofanywa na serikali kwa ujumla.
Wanahabari wakisikiliza kwa makini
             Akizungumzia  swala la rais wa Malawi kufuta matokeo na kutangaza uchaguzi kurudiwa  JUKATA wamesema kuwa wameshangazwa sana na hali hiyo ambapo wameipongeza sana mahakama ya nchini Malawi kwa kuonyesha ukakamavu wao katika kupingana na matakwa ya rais banda na kuamuru matokeo yahesabiwe tena ambapo amesema kuwa kama hilo lisingefanyika basin chi ya Malawi ingeingia katika machafuko makubwa sana.

No comments: