Thursday, June 26, 2014

breaking newzz---TUNDU LISSU AVUNJA UKIMYA WA CHADEMA KWA MARA YA KWANZA ATOA YA MOYONI KUHUSU KINACHOENDELEA CHADEMA,APANGUA HOJA ZA WAKINA YONA--USIKOSE IPO HAPA PEKEE

                                                          Na Karoli Vinsent

       SIKU moja kupita Baada ya watu, wanaojiita Viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA,kuandamana mpaka kwenda kwa Mkaguzi mkuu wa Hesabu za Serikali “CAG” pamoja na kwa Masajili wa vyama vya kisiasa nchini,kuwashtaki viongozi wa Juu wa chama hicho kwa madai ya matumizi mabaya ya Fedha.

       Nae,mwanasheria mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Tundu Lissu,ameibuka na kuwataka wanachama wa chama hicho kuwapuuza watu hao,kwa madai  kuwa chadema iliwafukuza uanachama na sasa hivi wanatumiwa  na Viongozi wa kutoka chama cha Mapinduzi ili kukidhofisha chama hicho kikuu cha upinzani nchini.


        Kauli huyo ya Tundu Lissu,ameitoa muda huu wakati wa mahojiana na Mwandishi wa Mtandao huu kwa njia ya simu kutoka mjini Dodoma kwenye Vikao vya Bunge vinavyoendelea huko, ili kutaka kujua kauli ya chama kuhusu tuhuma hizi,ambapo alisema chama hicho akiamui mambo bila kuwashirikisha wajumbe wa juu wa chama hicho na pia chadema ilishwafukuza viongozi hao kutokana na kutumiwa na CCM.

        “Kwanza nataka niwambie wanachama wa chama cha Demokrasia na Maendeleo chadema ,kwamba madai wanayosema matapeli hao hayana ukweli wowote na kwanza chama kiliwafukuza uwanachama, mda mrefu,na chama chetu kinafanya mambo kwa kuzingatia katiba na sheria vilevile kuwashirikisha wajumbe Kamati kuu ya chama”alisema Lissu.

        Kuhusu madai ya matumizi mabaya ya Fedha ndani ya chama hicho. Tundu lissu alisema anashangaa sana kwa madai hayo kwani chama hicho kila shilingi 10 inayotumia ndani ya chama hicho,inapitishwa na kamati kuu ya Chama hicho ,na tena kamati kuu hiyo inakutana kila baada ya miezi mitatu kukagua.huku kama kukitokea matatizo kwenye matumizi ya Fedha kamati hiyo inawajibu ya kumwajiisha kiongozi yeyote ambaye atakuwa mesababisha matumizi.

         Lissu,ambaye ni Mbunge wa Singida Mashariki alizidi kusema endapo chama kingekuwa kinafuja pesa ingeonekana wazi katika ukaguzi unaofanywa na mkaguzi wa Hesabu za Serikali,ambapo chama hicho mala zote inapoguliwa haijawai kutokea ufisadi wowote.

        Kuhusu tuhuma wanazodai kwamba Magari ndani ya Chama hicho yamesajiwaliwa kwa  jina Mwenyekiti wa Chama Freeman Mbowe.

     Lissu, ambae ni wanasiasa mjuzi wa juu wa masuala ya Sheria nchini alisema madai wanayosema magari yamesajiliwa kwa Jina la MBOWE HOTER sio kweli badala yake chama hicho kilikuwa kinatumia magari ya Mbowe kabla hajauziwa chadema.

        “Ngoja niwaeleze ukweli wanachadema kuhusu uongo huu unaoenezwa na hawa wasaliti,kwanza hakuna gari lolote limesajiliwa kwa jina Mbowe,bali yale magari makubwa yaliyokuwa yanatumiwa kipindi cha kampeni yalikuwa ya Mbowe,tena sisi wenyewe wajumbe wa Mkutano mkuu kwenye uchaguzi wa mwaka 2005”

      “Tulimpigia magoti Mbowe tukampigia magoti mbowe tukamwomba magari ndio akatupa magari yale makubwa ,akatupa kwa moyo mmoja na tukayatumia kwenye uchaguzi ule tena baadae sisi wenyewe wajumbe wa mkutano mkuu  akiwemo na huyo msaliti Yona tuliazimia kuyanunua  magari hayo kwa moyo mmoja,nashangaa leo watu wanavyomtukana mbowe kiasi hichi?alizidi kuhoji Lissu
Kuhusu madeni ambayo mbowe ameikopesha Chadema ambayo hayaishi.

        Mwanasheria huyo mkuu wa Chadema Tundu lissu,alisema viongozi hao ni watu wasio kuwa na Fadhila kwa kwenyekiti wa Chama hicho Freeman Mbowe kutokana na Kazi kubwa aliyoifanya kwenye chama hicho pamoja na Demokrasi ya Nchini kwa kumchafua Kiasi hicho.

       “Jamani hawa watu wananini na Mbowe kwasababu tangu mwaka 2005 kamati kuu ya chadema ilimwangukia mbowe na kumuomba hatukopesha Fedha na kweli mbowe alitukoposha milioni 520,kutoka mwaka huo chama kilimrudishia mbowe milioni 160,tena Mbowe akatusamehe hiyo pesa iliyobaki sasa hayo madai kwamba mbowe anaiba pesa za Ruzuku kwa kisingizia cha kulipa Deni alilotukopesha sio kweli”alisema Lissu.

         Madai ya Katibu mkuu wa Chadema Wilbrod Slaa kuchukua Milioni 160 kwa mwaka huku wajumbe wa juu wakichukua sh 0.
Mwanasiasa huyo, machachari alisema huo ni miongoni mwa uongo ambao chama hicho unafanyiwa kwa lengo la kuua Demokrasia nchini ambayo ilianza kuonyesha kustwawi miaka ya hivi karibuni.

        “Kwanza ngoje niweke sawa hili kwanza mnamo Mwaka 2010 sisi wajumbe wa Mkutano mkuu tulimuomba Dokta  Slaa agombea Nafasi ya Urais na achane na nafasi ya ubunge,yeye akasema endapo akikosa nafasi hiyo itakuwaje,sisi wenyewe wajumbe wa” mkutano mkuu tukamwambia tutakupa pesa ya mshahara wa Ubunge milioni 7 kwa mwezi,maana yake kwa mwaka anapata milioni 84 sio uongo wa 160,hivi walitaka katibu mkuu hawe masikini?alihoji Lissu

       Kuhusu kutofanyika Mkutano mkuu wa Wajumbe wa Chama hicho
Tundu Lissu,alisema ni kweli mkutani mkuu haujafanyika kipindi cha mwaka mmoja sasa ambapo ni kinyume na katiba ya chama.ila sababu ya kutafanya hivyo iko wazi ni kwamba hujafika mkutano mkuu kwa sababu mwezi wapili huo ungetakiwa ufanyike tulikuwa kwenye bunge la katiba na akasema kwa sasa chama kiko mbioni kuitisha mkutano huo.

      Kauli hii ya Lissu imekuja siku moja ikiwa Baadhi ya viongozi wakiongozwa  Joseph Yonna ambaye anajiita ni Mwenyekiti wa Chadema mkoa wa Temeke na Mjumbe wa Halmashauri kuu ya chama hicho pamoja na Athumani Balozi ambaye naye amejipachika cheo ambacho hakipo cha ukatibu wa Chadema kutoa mkoani Tabora.

        Ambapo waliandamana Jana mpaka ofisi ya Mkaguzi mkuu wa Hesabu za serikali CAG Ludovick S.L.Utouh,pamoja Msajili wa Vya Kisiasa kwa madai ya Mwenyekiti Freeman Mbowe Pamoja kutumia pesa vibaya za Chama na kuvunja kanuni za Chama.


No comments: