Monday, June 23, 2014

HII NDIO STORY MPYA TOKA CHADEMA LEO--BAADHI YA VIONGOZI WAKE WAIBUKA NA KUMTUPIA ZIGO LA UFISADI MWENYEKITI WAO,SOMA KWA UNDANI HAPA

Na Karoli Vinsent 
   

        IKIWA imebakiza mwaka mmoja tu,ili kufikia uchaguzi mkuu mwaka 2015,nacho chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA,kimeingia katika mgogoro mwingine baada ya baadhi ya wanachama wake kuibuka leo na kudai ndani ya chama hicho kuna ufisadi unaoendelea.

         Hayo,yaligundulika leo Jijini Dar es Salaam wakati wa Mkutano na Waandishi Habari na Viongozi wa chama hicho kutoka mikoa mbalimbali,ambao wanafikia 78 vilevile Viongozi hawo ni Wajumbe wa Baraza kuu na mkutano mkuu wa CHADEMA.

        Akisoma maazimio ya viongozi hao,Katibu wa chadema mkoa wa Tabora Athumani Balozi,alisema wamefikia hatua hii kupingana na viongozi wa Juu wa Chama hicho ni kutokana na kile wanachodai ni
Kuchoshwa na Vitendo vya Ufisadi vinavyofanywa na viongozi wakuu wa chama hicho.


    “Matendo ya viongozi wetu ni Unafiki wa Kisiasa ,kiasi cha kutumia Mabilioni ya chama kwenda kummaliza  kisiasa kiongozi mwenzao Zitto Kabwe na kuacha ujenzi wa Chama ukiendelea kuporomoka”

      “Kwenye ujinga huu,hakuna wa kumlahumu zaidi  viongozi wetu wenyewe”alisema Balozi

        Balozi,ambaye ni mjumbe wa Baraza la Mashauriano Kanda ya Magharibi wa CHADEMA,alizidi kusema chama kina endeshwa kifisadi kwani fedha za Ruzuku kutoka kwenye chama hicho, zinakwenda kwenye mifukoni  mwa Mwenyekiti wa chama hicho .

     “Tunasikitishwa sana na Kitendo cha Mwenyekiti wa Mbowe kusema anajilipa madeni aliyokikopesha chama kila siku,kiasi cha Millioni 700 ,sasa tunashindwa kuelewa deni hili ni deni gani lisiloisha?”

     “Na je deni hili alikikopesha chama kwa mkataba gani?na mbele ya nani huo mkataba wa mkopo?taratibu za chama chama za Kukopa za fedha zilifuatwa au matumizi mabaya ya Fedha za Umma”alizidi kusema Balozi.

      Kuhusu mbowe kununua  Magari chakavu ndani chama hicho.
Katibu huyo,Athumani Balozi alisema mbowe anafaa kutokubalika ndani ya chama hicho kutokana na kufanya utapeli wa kununua Magari chakavu ambayo yanafikia Milioni 700,huku akijua ni chakavu na kwamba kabla ya kukiuzia chama alikuwa anayakodisha magari hayo.

       Vilevile ,alizidi kusema wao wamebaini Mbowe kanunua Landcruiser V8 VX 2 kwa pesa za Chama hicho,tena magari mengine ndani ya chama hicho yamesajiliwa kwa jina la MBOWE HOTELS ,huku akijua  kufanya hivyo matumizi mabovu ya Fedha.

        Kuhusu CHADEMA kususia vikao vya Bunge Maalum la Katiba.
Naye, Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Temeke ambaye ni mjumbe wa Halmashauri kuu ya chama hicho Joseph Yona ,alisema kitendo hicho cha ni kuvunja kanuni  za chama hicho.

     “Bunge la Katiba lilikuwa ni mazao ya juhudi zetu sisi wanachadema tuliopambana nchi nzima kuidai katiba”

       “Nashangaa leo chama hichi kimeunda baraza kivuli la Mseto na Vyama tulivyowaaminisha watanzania kuwa vina ushiriki na CCM,huku bila hata kutushirikisha wajumbe wa Baraza la mkutano mkuu,huku wakijua wanaojiunga nao ni CCM B”alisema Yona.

        Yona,ambaye ni mwenyekiti pia Vijana wa Chama hicho mkoa wa Temeke,alizidi kusema chama cha Wananchi CUF pamoja na NCCR na kujiundia umoja unaojiita UKAWA.ni unafiki ambao unakimaliza chama hicho kwani vyama hivyo vinaubia na Chama cha Mapinduzi CCM.


No comments: