Thursday, June 26, 2014

TIGO NA HUAWEI WAFANYA MAAJABU MENGINE MUDA HUU,SASA "SMARTPHONES" BEI SAWA NA BURE,NUNUA URUDISHIWE HELA YAKO

Mkuu wa kitengo cha internent wa TIGO  bw DAVID ZACHARIA akizungumza na wanahabari muda mchache uliopita
 Kampuni ya mawasiliano ya TIGO Tanzania leo imetangaza kuingia katika ushirikiano na kampuni ya technologia ya HUAWEI ili kuwawezesha wateja wa kampuni hiyo ya simu nchini kuweza kupata simu za kisasa "SMARTPHONES " kwa bei nafuu.
Akizungumza na wanahabari jijini Dar es salaam muda mchache uliopita mkuu wa kitengo cha internent wa tigo bw DAVID ZACHARIA amesema kuwa ushirikiano huo unawapa   wateja fursa ya kuweza kumiliki simu aina ya HUAWEI  Y330 kwa bei ya punguzo ya shilingi 130,000 na HUAWEI Y530 kwa shilingi 195,000 tu.
Ndio aina ya simu ambazo zitakuwa zinauzwa
 Kwa mujibu wa Bw ZACHARIA wanunuzi wa simu hizi mbili watapata kifurushi cha bure cha thamani ya shilingi 30,000 katika mwezi wa kwanza baada ya kununua ambapo kifurushi hicho kinajumuisha dakika 600 za muda wa maongezi,sms 8000,za bure na 1.5 GB za  data za internent.na katika miezi sita inayofuata mteja atakayenunua kifurushi cha mwezi cha shilingi 15,000 atarudishiwa kiwango sawa na alichonunulia,ambapo amesema   inamaanisha kuwa baada ya baada ya miezi sita mteja atakuwa amerudishiwa zaidi ya shilingi 120,000.
Akizungumza katika mkutano huo wa waandhishi wa habari meneja chapa wa kanda ya Africa  mashariki na kusini toka HUAWEI  AZALEA DU amesema kuwa HUAWEI  Y 330 ni simu za kisasa zinazolenga vijana ambapo kampuni yake inafarijika sana kuwapatia wateja wa tigo fursa ya kuitumia.
Mwakilishi kutoka HUAWEI akizungumza na wanahabari katika makao makuu ya TIGO TANZANIA
Ofa hii inakuja ikiwa ni miezi michache tangu kampuni ya tigo kutangaza kuwapa wateja wake uwezo wa kutumia FACEBOOK buree kabisa kwa lugha ya Kiswahili ambapo wateja wake wameonekana kuifurahia sana .

No comments: