Tuesday, June 17, 2014

WANAOCHEZA UCHI KWENYE CLUB WAMCHEFUA KAMISHNA KOVA,SASA WAPIGWA MARUFUKU LEO,ASEMA OLE WAKO---



ONYO KUHUSU CLUB ZINAZOCHEZESHA NGOMA AINA YA BUNYEROBUNYERO KINYUME CHA SHERIA
Jeshi la Polisi Kanda Maaluum ya Dar es salaam limetoa onyo kali kuhusu ngoma mpya ilyoibuka hivi karibuni katika club za usiku ambazo ngoma hizo ni za aibu na kinyume cha maadili.Hakuna tofauti kubwa kati ya ngoma ya Bunyerobunyero na vigodoro ila tofauti yake ni maeneo.  
KAMISHNA KOVA
     Vigodoro hufanyika mitaani sehemu ambazo ni makazi ya watu wa hali ya kawaida wakati hufanyika katika club maarufu za usiku ambazo huhudhuriwa na watu wenye kipato cha kati na cha juu. Onyo hili linatolewa kwa sababu huu ni mtindo ulioko sehemu mbali mbali za jiji la D’Salaam. 
MFANO HUU HAPA
  Uchunguzi unafanyika na endapo itabainika ngoma hizo kuendelea kuchezwa basi Jeshi la Polisi pamoja na halmashauri za miji itakuchukua hatua mbali mbali za kisheria ikiwa ni pamoja na kuzifungia club hizo.

No comments: