Naibu kamishna wa Uhamiaji ambaye pia ni Msemaji wa uhamiaji Afande Abbas Irovya akizungumza na wanahabari jijini Dar es salaam |
Na Karoli
Vinsent
IDARA ya
Uhamiaji nchini imelitaka gazeti la Tanzania Daima kupelekea ushahidi wa Madai
ya Rushwa waliyoishutumu Idara hiyo.
Kauli hiyo
ya Uhamiaji nchini inakuja siku moja kupita baada ya Gazeti la Tanzania Daima
toleo la jumapili tarehe 7 mwezi huu lenye kichwa kikubwa cha Habari “Ufisadi
uhamiaji”ambapo toleo hilo lilisema viongozi wa idara ya uhamiaji wamepokea
rushwa ya sh milioni 2 kwa watu kila mtu
aliyepewa ajira kwenye idara hiyo na kusema katika watu 200 waliopewa ajira
Idarani hapo walitoa pesa hizo ambapo jumla ya fedha zote inafikia Bilioni 2.1
Toleo ambalo linalalamikiwa na uhamiaji |
“Habari kwenye Gazeti la Tanzania Daima toleo la jumapili tarehe 7 mwaka huu
imetusikitisha sana kwani habari haina ukweli wowote tena inamalengo ya
kutuchafua tu,kwasababu mwandishi wa habari hiyo ameshindwa kuweka hata
ushahidi wa moja kwa moja juu ya hao vigogo anaosema kwamba wamechukua rushwa
ya Bilioni 2.1 zaidi ya kusema ni kwa mujibu ya vyanzo vyetu,tena mbaya zaidi
ameshindwa hata kutufwata sisi watu wa uhamiaji ili kupata ukweli yeye kaishia
kuandika Habari ambayo haina ukweli “alisema Irovya
Waandishi wa habari wakisikiliza kwa makini |
I rovya
alizidi kusema idara hiyo inamtaka mwandishi wa Gazeti hilo apeleke Majina ya
hao vigogo wa uhamiaji ambao anaowashutumu ili idara hiyo iwachukulie hatua
kali za kisheria kwani kufanya hivyo kutaweza kuijenga idara hiyo kwa Wananchi,
Aidha Irovya
aliwataka Waandishi wa Habari nchini
kufanya kazi kwa kuzingatia Weledi mkubwa sana ili taarifa zao ziweze kuleta
manufaa kwa jamii,
Huu ni Mwendelezo wa kuzidi kubanwa kwa
Gazeti la Tanzania Daima ikumbukwe karipio hili la Idara ya Uhamiaji limekuja
siku chache kupita baada ya Ofisi ya Msajili wa Magazeti nchini kuliandikia
barua gazeti hilo na kusema liache kuandika habari zenye upotofu kutokana na
moja ya matoleo yake yaliyopita yenye kichwa cha Habari “Rais Kikwete ayalamba
Matapishi yake” pamoja na “Rais Kikwete anywea”
Kwa mujibu ya Barua hiyo ililitaka Gazeti
hilo kukanusha taarifa kutokana na
habari hiyo Kukwaza Rais Jakaya Kikwete,
Baada Barua hiyo kulifikia Gazeti
hili,ndipo Mhariri wa Gazeti hilo katika toleo la leo tarehe 9 mwezi huu,Katika
ukurasa wake wa Kwanza lilikuwa na Kichwa cha Habari “Kumradhi Jakaya Kikwete”
No comments:
Post a Comment