Wednesday, October 22, 2014

BAADA YA WAHISANI KUSITISHA KULETA MISAADA TANZANIA,DK SLAA AIBUKA NA KAULI NZITO,SOMA ALICHOKISEMA HAPA

Na Karoli Vinsent

        HUKU ikiwa nchi Wahisani hususani Uingereza,Swiden na zengine zikiwa zimesitisha Misaada kwa Serikali ya Tanzania kwa kile wanachodai ni kuchoshwa na Vitendo vya Ufisadi vinavyofanywa na Watendaji wa Serikali ya Rais Jakaya Kikwete  kwenye Akaunti ya Escrow ambapo zaidi ya Bilioni 400 zimeibiwa.
    
             Naye Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Dokta Wilbroad Slaa ameibuka na kumvaa Rais jakaya Kikwete na kusema yeye ndio anafaa kulaumiwa na Watanzania kwa kitendo chake cha kuwakumbatia mafisadi ndani ya serikali yake na kushindwa kuwachukilia hatua.

           
             Hayo yamesemwa  Mda huu wakati wa Mahojiano kati ya Mwandishi wa Mtandao huu na Katibu huyo Mkuu wa Chadema Dokta Wibroad Slaa,ambapo amesema kuhusu kitendo cha nchi wahisani ambao wamekuwa wakuisaidia Tanzania kufanya maamuzi hayo,yanatokana na Rais Kikwete kuwakumbatia mafisadi hata wakati wa kampeni za Uchaguzi mwaka 2010 aliwanadi kwa wananchi ili washike uongozi.
       
           “Wahisani mpaka wamefikia hapo na wamechoka kama sisi tulivyo choka na ufisadi kwani hata hizo pesa zinazoliwa zinatokana na kodi za nchi yao, na nchi yeyote inayojali pesa za walipa kodi haiwezi kufanya hata siku moja kama wanavyofanya serikali  hii,na haya yote ni uzembe ambayo yanatokana na kuongozwa na viongozi wasiokuwa na hofu ya mwenyezi Mungu na wala sakata la ufisadi Tanzania sio geni kwani ni utamaduni usiozoeleka”alisema Dokta Slaa
       
              Dokta Slaa alizidi kusema Watanzani wataumia mara mbili kwanza ni kwakukosesha fedha za Maendeleo kutoka kwa marafiki  wahisani na pili  fedha zimepotea na kutokana na ufisadi,  na Ufisadi huo  wa Akaunti ya Esrow unatokana na Serikali  kuwa jueri na serikali ambayo inawalinda mafisadi na kutowachukulia hatua mafisadi,
     
          Vilevile Dokta Slaa alimtupia Lawama Spika wa Bunge la Muungano Anna Makinda kwa kitendo chake cha kuwapuuza wabunge wa upinzania ambao walitaka iundwe tume maalum ili kuchunguza sakata ka ufisadi kwenye Akaunti ya Escrow ambapo Dokta slaa alisema kufanywa hivyo kwa spika ni wazi ni kulinda mafisadi.
     
         Kuhusu misamaha ya kodi inayotolewa na serikali  ambayo imefikia trillion 1.5 Dokta Slaa alisema angekubaliana na serikali kwamba ingewasemehe mama lishe au watanzania masikini lakini anashangaa kwanini serikali inawasemehe makampuni makubwa kodi ambayo yanaingiza mamilioni ya fedha na kusema kitendo cha serikali kusamehe kodi kutazidi kuifanya Tanzania kuwa masikini.
Kuhusu ununuzi wa Hedkopta ya jeshi ambayo umelenga kwa ajiri ya uchaguzi ndani ya ccm mwakani
   
        Slaa alisema yeye mwenyewe amekamata barua ambayo ilitoka jeshini kwenda  kwa nchi ya Ufaransa na kusema barua hiyo imeonesha ubabaishaji mtupu

        “Serikali yetu inanunua hedkopta kutoka ufaransa kwa njia ya ufisadi,ambao ufadi huu unafanana na ule wa kununua ndege ya Rais pamoja na rada,kwanza kununua hedkopta kwa ajiri ya jeshi letu ni jambo jema,lakini lugha iliyotumika kwenye barua niliyoikamata sio nzuri kwani imesema hivi kwamba hizo helkopta zifike kabla ya uchaguzi mkuu  kwahiyo jina la jeshi linatumika kwa ajiri ya kukisaidia chama cha mapinduzi”alisema Dokta Slaa 

No comments: