Sunday, October 19, 2014

MANGULA, NAPE WAONGOZA KONGAMANO LA MAADHIMISHO YA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE YA VIJANA WA CCM VYUO VIKUU , LEO


Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Philip Mangula akihutubia Jumuia ya Wanafunzi wa Vyuo vya Elimu ya Juu katika Kongamano la Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere, lililoandaliwa na Vijana wa CCM wa Vyuo Vikuu, kwenye Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam, leo, Oktoba 19, 2014.

Katibu wa NEC, Irikadi na Uenezi, Nape Nnauye akimpongeza Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara), Mzee Mangula baada ya kuhutubia katika kongamano hilo. Kulia ni Katibu Mtendaji Mkuu wa CCM mkoa wa Vyuo Vikuu, Christopher Ngubiagai
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akihutubia katika Kongangamano hilo la Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere. Nape amewataka wasomi kutofumbia macho matatizo ndani ya CCM, badala yake wakati wakisifu  mema wawe mstari wa mbele kuyafichua na kuyakemea mapungufu ili chama kiende na wakati
Katibu Mtendaji Mkuu wa CCM mkoa wa Vyuo vya Elimu ya Juu, Christopher Ngubiagai akizungumza wakati wa kongamano hilo la Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere.
Mwenyekiti wa CCM tawi la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam,, Theodora Malata akizungumza mwanzoni mwa kongamano hilo
Washiriki wakisikiliza kwa makini mada mbalimbali zilizokuwa zikitolewa wakati wa kongamano
Katibu Mwenezi wa CCM mkoa wa Dar es Salaam, Juma Simba akizingumza kwenye kongamano hilo.
Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Philip Mangula na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye wakiwa na viongozi wengine meza kuu baada ya kuwasili ukumbini.(Picha na Bashir Nkoromo)

No comments: