Friday, October 3, 2014

HABARI ILIYOTIKISA JIJI---MWAKYEMBE ATAKA KUIFANYA DAR ES SALAAM KAMA ULAYA,SOMA ALICHOKIFANYA MUDA HUU

Mmiliki wa kamouni hiyo ambayo imeamua kujenga tren hizo za kisasa nchini kutoka marekani katikati na wenzake wakionyesha picha ya treni hizo ambazo sasa zitafanya kazi jijini dar es salaam
 Serikali ya Tanzania kupitia wizara ya uchukuzi leo imeingia katika historia nyingine baada ya kusaini mkataba na kampuni ya SUMOJA kwa ajili ya kujenge tren za kisasa ambazo zitafanya kazi katika jiji la Dar es salaam tren ambazo kwa sasa zinatumika katika mataifa yaliyoendelea duniani.
ROBERT SHUMARKER ambaye ndiye kampuni yake iliyojitoa kujenga tren hizo za kisasa jijini Dar es salaam akizungumza na wanahabari muda huu ambapo amesema kuwa kauli mbiu yake ni LEO yani kazi inaanza leo
  Mmiliki wa kampuni hiyo kutoka marekani ambaye naye pia ni mmarekani akizungumza na wanahabari muda huu makao makuu ya wizara ya uchukuzi ROBERT SHUMAKER amesema kuwa ameamua kujitolea kulisaidia taifa la Tanzania kuhakikisha kuwa linapata usafiri wa haraka na makini ambapo amesema kuwa zoezi la ujenzi wa vituo na njia unanza mara moja kwani hakuna muda wa kupoteza katika hilo ambapo mradi huo unatarajiwa kugharimu dolla million 35.
Waziri wa uchukuzi nchini Tanzania mh HARISON MWAKYEMBE akizungumza nna wanahabari muda huu jijini dar es salaam juu ya ujio wa treni hizo ambao amesema kuwa ni mkombozi wa foleni za jiji la Dar es salaam
 Aidha waziri wa uchukuzi mh HARISON MWAKYEMBE amesema kuwa mkataba huo ni matunda ya juhudi za rais wa Tanzania MH JAKAYA KIKWETE katika kufungua milango ya wawekezaji duniani kuja kuwekeza hapa Tanzania.ambapo amesema kuwa treni hizo zitaanza kujengwa njia ya pugu na zinatarajiwa kukamilika ifikapo mwanzoni mwa mwaka kesho.

No comments: