Monday, November 24, 2014

ANNA MAKINDA AANZA KAZI,TIZAMA MALUMBANO YA LEO HAPA,


MHE  MAKINDA 

Mbatia: Naomba kuwasilisha hoja, ofisi yako ilipokea ripoti maalamu kuhusu Escrow na umiliki. Taarifa hii ilikua siri mpaka itakapowasilishwa bungeni na turiarifiwa taarifa ya PAC haijakamilika na tumepata taarifa ripoti hiyo inagawiwa kama njugu na baada ya kutoa taarifa polisi wamefanikiwa kumkamata mtu mmoja na inavyoonekana taarifa hio imeibiwa na ina muhuri wa katibu mkuu na kwa mujibu wa maelezo taarifa hio imeibwa. Katiba ya jamhuri 1977 linaainisha bunge lina mamlaka ya kusimamia fedha za umma, kitendo cha kusambazwa mitaani wakati bado haijatolewa rasmi inadhiirisha kuna watu wamejipanga kushusha heshima ya bunge. Kwa kua kumekua na jitihada nyingi zinazolenga kuzuia bunge kushindwa kufanya kazi yake, kwa kutumia kanuni ya 51 naomba kutoa hoja bunge lisitishe shughuli zake za sasa na kujadili ripoti hio

Makinda: Hamna hoja hapo na kaeni msome kifungu cha 51, ofisi ya bunge imeshirikiana na polisi ili muhusika asitoke mpaka aeleze mAshine gani zimetumika naikithibitika amefanya atapata kifungo cha miaka mitatu. Tukipata taarifa ya polisi tutachukua hatua na hamna ubabe hapa ninaoufanya.
Order paper imebadilishwa hivyo litajadiliwa humu ndani, nchi inaendeshwa kwa taratibu na kazi inaendelea hivyo hatuwezi kujadili kitu ambacho hakijaishwa.

MIONGOZO MINGI SANA

Mnyaa: Jambo aliloliomba mbatia na mjadala huu ni mpana na halihusiani tu na kusambazwa nyaraka na wengi wameshachafuliwa ikiwemo na wewe kuchukua dola 1,000,000/=, kwa heshima tunaomba uruhusu mjadala huu angalau kwa nusu saa.

Tundu Lissu: Mheshimiwa spika, nashukuru kwa fursa na kwa kuwa ni suala la kikanuni, ni vizuri turidhike kama hOja ya Mbatia ina haja kujadiliwa ama laa. Kanuni ya 51: Umeridhika na hili suala na ndio maana umempa nafasi Mbatia, tunajadili yanayotokea na vizuri jambo lizungumzwe ili hii hali isafishwe.

Makinda: Naheshimu profession yako lakini pia na wewe uheshimu taratibu, polisi wanaendelea na wakimaliza spika atapanga.

Ole Sendeka: Kamati itawasilisha lakini jambo hili jambo hili linahitaji kutendewa haki, nna mashaka, bunge litapata muda gani kusoma ripoti. Ripoti ipatikane kwa wabunge rasmi ili siku ya kuwakilisha tuweze kujadili

Makinda: Tunafanya utaratibu mpate ripoti mapema

No comments: