Sunday, November 2, 2014

HAYA NDIYO YALIYOJIRI UBUNGO KWENYE MDAHALO,MAKONDA AMTWANGA WARIOBA MCHANA KWEUPE


Jaji Warioba.

VURUGU zilizoambatana na ngumi kurushwa zimetokea hivi punde katika Ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar es Salaam wakati aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Warioba alipokuwa akitoa mada kwenye mdahalo wa kujadili umuhimu wa kuielewa kwa kina Katiba inayopendekezwa kama ilivyopitishwa na Bunge Maalum la Katiba.
 
Vurugu hizo zimezuka baada ya watu waliokuwa na mabango kuvamia ukumbuni hapo na kusababisha baadhi ya watu waliokuwa wanafuatilia mdahalo huo kuwakabili na kuwapa kichapo.
 Baada ya vurugu hizo, mdahalo huo ulioandaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere na kurushwa moja kwa moja na ITV umesimamishwa kwa muda.

Kwa upande wake Gwiji La masuala ya habari nchini na Mhariri wa Gazeti la Tanzania Daima Edson Kamukara alichukizwa na kitendo cha Makonda haya ndio aliyoyasema kwenye ukrasa wake facebook


SOMA ZAIDI WALICHOKISEMA WADAU JUU YA YUKIO HILO LA TUHUMA ZA MAKONDA KUMPIGA WARIOBA NA CHUPA
Kwa upande wake  Butiku haya ndio haliyoyasema kuhusu Makonda
Tokea nizaliwe sijawai kukasirishwa na hili jambo la Makonda kumpiga na chupa Mzee Warioba. Ni utovu wa nidhamu, ni dharau, ni ujinga, ni utoto, ni ukora, ni u.p.mbavu, ni akili ndogo, ni kukosa hekima na misamiati ya namna hiyo kwa hili jambo la Makonda kumpiga na chupa mzee Warioba. Nilikuwepo kwenye eneo la tukio kwa macho yangu nikashuhudia Makonda akimpiga na chupa mzee Warioba, nimeumia sana sana. CCM lazima waruhusu mawazo mbadala ili kujenga Taifa na kamwe kundi moja lenye mawazo yanayofanana hauwezi kujenga Taifa, lazima kuwepo na mawazo huru kwa pande zote katika jamii. 

Ila nasita kusema kama kweli Makonda katumwa na CCM inawezekana kabisa katumwa na Nape au Sita. Warioba ni Kiongozi mstaafu tena katumikia Tanzania kwa moyo wote hivyo vijana kukosa adamu mpaka kufikia hatua ya kumpiga na chupa ni ujinga wa hali ya juu na vijana wa pande zote lazima tukemee hili jambo. Jeshi la polisi tafadhali mlifanyie hili kazi, na Makonda naomba nikupe ujumbe kuwa vijana hatutakaa kimya lazima tutakufanya kwa njia yoyote ile uweze kumuomba Mzee Warioba radhi na taifa kwa ujumla, Leo umefanya kwa Warioba, Kesho utasita kufanya kwa Mwinyi au Malecela au Mkapa...

Nimeuzunishwa sana na hili jambo....Shame on you Makonda


Ocampo four

Maneno ya Butiku naomba kunukuu "Huu uhuni uliyofanywa na Makonda haukubaliki hata kidogo, kitendo cha kumpiga Warioba na chupa tunaomba serikali iliangalie jambo hili na pia kuhakikisha katika midahalo mingine huyu muhuni asiwepo, Asanteni" mwisho wa kunukuu. 


Maneno ya Butiku baada ya kikao kuisha akiongea na vijana nje ya ubungo plaza

Naomba kunukuu "Kamwe vijana wa CCM msikubali kuchagua viongozi wanaomtuma Makonda kutenda haya, ni uhuni na ujinga wa hali ya juu" alipoulizwa ni nani wako nyuma ya Makonda, bila kusita akasema Membe na Sita

No comments: