Sunday, November 23, 2014

PICHA YA ESCROW IMENOGA--KUTOKA CUF MUDA HUU SOMA WALICHOTANGAZA

Mwenyekiti wa cuf IBRAHIMULIPUMBA akiwasili makao makuu ya chama kukutana na wanahabari mapema leo
Chama  cha wananchi CUF leo muda huu kimewataka waziri mkuu wa Tanzania mh MIZENGO PINDA,mwanasheria mkuu wa Tanzania jaji Fredrick werema,waziri wa nishati na madini profesa SOSPETER MUHONGO,pamoja na katibu mkuu wa wizara ya  nishati na madini bwana ELIAKIM MASWI kuachia ngazi mara moja au kufukuzwa kazi kutokana na wao kuonekana wazi kuwa wanautetea ufisadi wa mabilioni ya escrow unaoendelea nchini.


         Akizungumza na wanaandishi wa habari mapema leo makao makuu ya chama hicho mwenyekiti wa CUF profesa IBRAHUIM LIPUMBA amesema kuwa viongozi hao wamekuwa mstari wa mbele kuonyesha wazi kuwa hawako tayari kuona wahusika wa ufisadi huo wakiadhibiwa hivyo hawana sifa ya kuendelea kuiongoza nchi kwani hawana maslahi kwa wanachi huku akiitaka TAKUKURUI nao kuwachunguza viongozi hao kama wanahusika na ufisadi huo.
Hapa akizungumza na wanahabari
“hivi karibuni tulimsikia waziri mkuu akiwadnaganya watnzania kuwa fedha zilizopo kwenye account ya tegeta ESCROW sio mali ya umma bali ni mali ya kampuni binafsi kauli ambayoni ya uongo na yakujaribu kuficha maudu hayo”amesema lipumba

       Aidha CUF wameitaka TAKUKURU kuwakamata mara moja vigogo JAMES RUGEMALIRA ambaye mtandao huu pia umesharipoti kuhusika kwake pamoja na HARBINDER SINGH SETH na kuwafungulia mashtaka ya rushwa mna wizi wa mali ya tanesco kwani hawa ndio wahusika namba moja wa kuzigawa pesa hizo kama zao.

           Aidha lipumba ametaka pia mkuruygenzi wa tanesco pamoja na bodi nzima ya tanesco kufutwa mara moja kwa kuwa haikutimiza wajibu wake wa kulinda maslahi ya shirika wanaloliongoza.

         Katika hatua nyingine chama hicho kmesema kitafanya maandamano ya nchi nzima baada tu a mjadala huo kumalizika bungeni kuwashinikia viongozi waliohusika kuwajibika na pia kuwapongeza wabunge waliosimamia kuonyeshwa kwa ufisadi huo.


No comments: