Wednesday, December 10, 2014

LHRC WAADHIMISHA MIAKA 66 YA TAMKO LA HAKI ZA BINADAMU ULIMWENGUNI,TUKIO LIKO HAPA


Baadhi ya wanafunzi waliojitokeza katika maadhimisho hayo leo jijini Dar es salaam
 Kituo cha sheria na haki za binadamu LHRC kwa kushirikiana na wadau wengine wa haki za binadamu leo wameadhimisha miaka 66 tangu kuanzishwa kwa tamko la haki za binadamu la ulimwengu  ambalo lilitoka tarehe 10,mwezi wa 12 mwaka 1948,tamko ambalo ndio hasa chimbuko la misingi ya haki za binadamu kote duniani.
Tamko hilo ambalo linaainisha haki za kiuchumi,utamaduni,kiraia n kijamii lilifwatiwa na mikataba miwili ambayo ni mkataba wa kimataifa wa haki za kiraia,pamoja na mkataba wa kimataifa wa haki za kiuchumi,kijamii,na utamaduni 1966.
 Akizungumza katika maadhimishohayo ambayo awali yalitanguliwa na maandamano ya wadau wa haki za binadamu kaimu mkurugenzi wa LHRC Ezekieli Masanja amesema kuwa ipo haja ya serikali kuanza kuweka masimo ya haki za binadamu katika mitaala ya shule za msingi ili kuanza kuwajengea wanafunzi uelewa mapema wa haki za binadamu na jinsi ya kuzilinda,ikiwa ni pamoja na kukuza uelewa wa vijana wa shule juu ya haki za binadamu.


Kwaya mbalimbali zikitoa burudani
 Amesema kuwa pamoja na mambo yote  kufanyika lakini  bado kna haja kubwa ya kuanza kujenge uelewa wa vijanawadogo juu ya haki za binadamu wakiwa shuleni.
Aidha LHRC wametoa tathimini yao ya haki za binadamu kwa Tanzania ambpo bado inaonyesha zipo changamoto kubwa za ulindaji wa haki hizo mfano maeneo kama kiwango cha elimu bado kipo chini kwa watanzania,migogoro hasa ya ardhi bado imeendelea kuwa tatizo kwa watanzania,pamoja na ajali za barabarani na mauaji mbalmbali yameendlea kuwa changamoto kubwa kwa watanzania.


kaimu mkurugenzi wa LHRC Ezekieli Masanja
Burudani


No comments: