Tuesday, December 30, 2014

michezo--PSPF KUWAKUTANISHA WACHEZAJI WA ZAMANI WA YANGA NA SIMBA

SIMBA
MFUKO wa Pensheni wa PSPF umedhamini mchezo wa kirafiki utakaowakutanisha wachezaji waliowahi kuwika katika timu kongwe nchini Simba na Yanga.

Mchezo huo unatarajiwa kufanyika tarehe 1 Januari 2015 katika uwanja wa chuo cha Bandari, Tandika jijini Dar es Salaam, kiingilio kitakuwa bure ikiwa ni zawadi ya mwaka mpya kutoka PSPF. 

Katika mchezo huo baadhi ya wachezaji wa Simba wanaotarajiwa kushuka uwanjani ni Thomas Kipese, George Lucas, Bita John, George Masatu, Mustafa Hoza, Emmanuel Gabriel, Idd seleman. Timu ya Simba inafanya mazoezi katika uwanja wa Leaders uliopo Kinondoni, ipo chini kocha mchezaji Kasongo Athuman. 

Wanaotarajiwa kushuka uwanjani kwa upande wa Yanga ni Peter Manyika, Mwanamtwa Kihwelo, Edibily Lunyamila, Mohamed Husein, Chibe Chibindu, Aboukar Salum, Bakari malima. Yanga wanafanya mazoezi katika uwanja wa kauda ulipo katika makao makuu ya klabu hiyo kariakoo Jijini Dar es Salaam, wakiongozwa na kocha Peter Tino.
Lengo la mchezo huo ni kutoa burudani kwa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam na maeneo ya karibu hususani katika kipindi hiki cha sikukuu za mwisho wa mwaka. PSPF itatumia fursa hiyo kutangaza huduma zake mpya ambazo Mkopo wa Elimu na Mkopo wa Kuanza Maisha. Tunatoa mwito kwa wapenzi wa soka kujitokeza kwa wingi katika mchezo huo ili kuwaona wakongwe waliowahi kutikisha nchi katika anga ya soko nchini

No comments: