Monday, January 26, 2015

ESCROW--NCCR MAGEUZI WATAKA RUGEMALIRA NA KINA TIBAIJUKA WAKAMATWE MARA MOJA


Katibu mkuu wa NCCR-MAGEUUZI,ndugu, MOSENA NYAMBABE akizngumza na wanahabari mapema leo
          Chama cha NCCR-MAGEUZI kimeshangazwa na hatua za kuwapeleka mahakamani watu kadhaa ambao wanahusika katika kupokea mapesa ya ESCROW huku mtoa rushwa akiranda mitaani bila kukamatwa kwa kosa la kutoa rushwa.

Akizungumza na wanahabari leo mapmaa jijini Dar es salaam katibu mkuu wa chama hicho MOSENA NYAMBABE amesema kuwa chama chake kinapenda kujua ni kwanini wanaotuhumiwa kupokea rushwa za amana ya TEGETA ESCROW wanafikishwa mahakamani lakini anayetuhumiwa kutoa rushwa kupitia amana ya TEGETA ESCROW ambaye ni JAMES RUGEMALIRA hachukuliwi hatua yoyote hususani ya kupelekwa mahakamani.

Aidha amesema kuwa pia watua ambao wamewajibishwa na wengine kujiondoa wenyewe kama profesa ANNA TIBAIJUKA,ENDREW CHENGE,WILLIAM NGELEJA,VICTOR MWAMBALASA na DANIEL YONA , PAUL KIMITI na wengine waliotajwa kupokea pesa hizo wanastahili kukamatwa na kufikishwa mara moja mahakamani kwani nao ndio chanzo cha tatizo hilo.

Aidha chama hicho kimesema kuwa kinasikitishwa na hatua ya chama cha mapinduzi CCM kuwafumbia macho mafisadi hadi hapo wananchi wanapowafichua na ndipo nao huibuka na kuchukua hatua kitu ambacho kinaonyesha kuwa chama hicho kina ajenda ya siri na wahujumu uchumi wa Tanzania.




No comments: