Wednesday, January 28, 2015

SINTOFAHAMU BUNGENI MUDA HUU,KISA NI LIPUMBA


          Kufwatia sakata la mwenyekiti wa chama cha wananchi CUF  profesa  Ibrahim lipumba Jana kukakamwa na kupigwa katika maandamano ya chama chake huko temeke sakata hilo limetua bungeni asubuhi hii na kusababisha bunge kahirishwa kutokana na wabunge wa upinzani kuwasilisha hoja ya kuahirisha shughuli za bunge.kujadadili jambo la dharura lililojitokeza.

           Akiwasilisha hoja hiyo mwenyekiti wa NCCR MAGEUZI JAMES MBATIA ameliomba bunge kutoka na uzito wa jambo hilo na ukizingatia heshima aliyo mayo lipumba na kitendo alichofanyiwa paMoja na kutii amri ya polisi ni kitendo cha kihuni na hakivumilki hivyo bunge lijadili jambo hilo.

Mheshimiwa MBATIA amesema kuwa  Lipumba ni mwenyekiti wa chama ambacho kina wabunge zaidi ya 30 huku bungeni,lipumba ni mwenyekiti wa chama ambacho kinashiriki serikali ya umoja wa kitaifa huko zanzibar,haiwezekani atendendewe kitendo kama kile kilichotokea jana,naomba mwongozo wako spika ili tusitishe mambo ya leo na tujadili jambo hili ambalo ni kubwa na haliwezi kufumbiwa macho
.
Baada ya kuwasilisha hoja hiyo wabunge wa upinzani walisimama ishara ya kuunga hoja mkono hapo ndipo spika makinda alipowataka wakae na swala hilo litapatiwa majibu na serikali hapo kesho.

Baada ya majibu hayo wabunge wa upinzani hawakuridhika na wakaendelea kusimama hadi spika akaamua kulisitisha bunge hadi SAA kumi Leo.


No comments: